Dalili moja ya mtu mshamba ni kujua kuongea 'kilugha'

Dalili moja ya mtu mshamba ni kujua kuongea 'kilugha'

Mkuu, fahamu hata kiswahili ni kilugha fulani hivi.
kwa mantiki yako nawe ni mshamba unayepaliilia bustani ya ujinga.
Kwa taarifa yako ushamba ni mazoea yanayofanywa na mtu yeyote kwenye mazingira yasiyokubalika kufanywa hivyo na wakazi wa eneo husika!
Kwa mfano, ukienda nchi za ulaya, hata uwe umezaliwa kariakoo, ukakulia postai Dar es salaam, lakini ukinunua kitu ukatupa kifungashio barabarani, mbali ya kwamba ni uchafu kwao, ila tena ni ushamba, wakati kwa wabongo ni kawaida tu.
Hili neno ushamba ni pana mno!
Kinyume chake ni neno USTAARABU!
Sijui kama unafahamu kwamba
kugombana.
Kuiba.
kukata foleni kwenye huduma fulani.
Kugombania daladala.
Kufungua mziki kwa sauti kubwa
Misifa ya kijinga.
Kujidai ni mtoto wa mjini.
Na ushamba mwingine kibao kwa aina zake, wote ni huohuo mmoja.
Lakini lugha kwa yenyewe haiwezi kunasibishwa na ushamba.
Samahani lakini.
Umeongea vyema lakini hata bongo kutupa kifungashio barabarani ni uchafu wala si jambo la kusema ni kawaida. Sasa basi hizo dalili zote ulizotaja za kukosa ustaarabu ni rahisi sana kuzikuta kwa mtu anayejua kilugha. Ndiyo maana nasema, kujua kilugha ni dalili moja kubwa sana ya ushamba.
 
Tudefine ushamba kama hali ya mtu kutojua utamaduni wa mjini au wa kisasa unataka nini. Mtu mshamba ni kazi sana kuendana naye au kuelewana naye.

Ni kazi sana kuishi na mtu mshamba au kufanya naye makubaliano. Hata ukioa au kuolewa na mshamba utapata taabu sana humo ndani. Ni vema kuwatambua na kuwaepuka.

Sasa basi, kuna dalili nyingi za kumtambua mtu mshamba, lakini kwa Tz dalili moja ya wazi ni mtu kujua kuongea kilugha. Ukiona mtu anaongea kilugha, taa ya hatari iwake kichwani mwako. Si wote wanaoongea kilugha ni washamba, lakini hilo ni moja ya dalili kuu za mtu mshamba.
Kuna Mzee anaitwa Ngugi Wa Thiong'o, mwandishi wa vitabu kama 'petals of blood na 'Wizard of the crow'. Hembu Google hilo jina uone ushamba wake.
Anaanza kuandika vitabu vyake kwa lugha ya asili ya Kikuyu, ila vinaishia kwenye lugha mbalimbali za kimataifa kama hivyo nilivyokutajia, na vinauzwa karibu ulimwenguni kote.
 
Navyopenda kuongea kilugha😂😂😂hata kwenye kamchezo ketu kalee nikinoga nakimwaga,, hapana raha naipata km kuongea lugha yangu mama,
 
Tudefine ushamba kama hali ya mtu kutojua utamaduni wa mjini au wa kisasa unataka nini. Mtu mshamba ni kazi sana kuendana naye au kuelewana naye.

Ni kazi sana kuishi na mtu mshamba au kufanya naye makubaliano. Hata ukioa au kuolewa na mshamba utapata taabu sana humo ndani. Ni vema kuwatambua na kuwaepuka.

Sasa basi, kuna dalili nyingi za kumtambua mtu mshamba, lakini kwa Tz dalili moja ya wazi ni mtu kujua kuongea kilugha. Ukiona mtu anaongea kilugha, taa ya hatari iwake kichwani mwako. Si wote wanaoongea kilugha ni washamba, lakini hilo ni moja ya dalili kuu za mtu mshamba.
Wewe ndio mshamba. Kiswahili, kiingereza, kireno., kijerumani etc "vilugha" vya wazaliwa wa maeneo hayo. Lugha unayodhani ni ya maana ni kilugha cha watu wengine. Hacha uzuzu.
 
Wewe ndio mshamba. Kiswahili, kiingereza, kireno., kijerumani etc "vilugha" vya wazaliwa wa maeneo hayo. Lugha unayodhani ni ya maana ni kilugha cha watu wengine. Hacha uzuzu.
Kama unajua kilugha uwezekano wa kuwa mshamba ni mkubwa sana.
 
Ushamba ni kuiga lugha za watu, mtu anajikunja na Kifaransa mpaka anashika pua ili atamke vizuri. Chukuwa neno la Kifaransa Tomb, inamaanisha kuanguka, sasa congugate wanavyosema uone utakavyohangaika. Mtu mstaarani ni yule anaetumia lugha yake ya asili anapokutana na watu wa asili yake. Mzungu mstaarani ni yule anaetumia kiswahili akiwa hapa Tz.
 
Back
Top Bottom