Damascus: Waasi wa HTS wauzingira mji wa Homa nchini Syria

Damascus: Waasi wa HTS wauzingira mji wa Homa nchini Syria

Waislam wa shia na sunna adui yetu Ni yahudi na kafiri

Tuache kuchinjana sisi kwa sisi
Sasa Adui yao namba Moja ni wao wenyewe.

Ikitokea Assad ameanguka usishangae kusikia Hezbollah na Iran wamekuwa Marafiki wa Israel kama Syria mpya haitakuwa kama Jordan.

Iran Ndio nchi ya Kwanza ya Kiislam middle east kuitambua Israel mwaka 1948.
 
Inasemekana ameachana na Siasa kali na amesema anataka Serikali inclusive kila Dini na kila Dhehebu litashirikishwa katika Utawala wake.

Hata kile Kilemba kakitupa.
Haui wakristo au bado anaua?
 
Wewe kwasasa ndio mbishi kuanzia Quruani nzima iko kwenye Internet kuna Islamic Chanel kwenye Internet kuna Historia ya Dini nzima ya Kiisilamu hadi jinsi Dhehebu la Shia lilivyopatikana sasa wewe unataka kumdanganya nani Shehe?!
Sheikh Imhotep!

Acha ubishi! Umesema elimu yote ya uislamu kwa sasa ipo kwenye internet basi niletee kitabu cha Imam Suyutwi cha Houjatum mudhakkiriina.
----------
Kwenye internet Qur'an ipo nzima kimatini, na kitarjum yaani kuibadilisha Qur'an kutoka kwenye lugha yake ya asili ya kiarabu kwenda kwenye lugha isiyo ya kiarabu, ila siyo kitafsiri.

Aya moja ya Qur'an inafafanuzi mpaka 40, utakuta wapi kwenye internet? Na hapo prngine ni tafseer ya kitabu kimoja tu hujaenda kwenye kitabu kingine.

Hiyo dini nzima kwenye internet unaikutia wapi?
--------------
Mawahabi wameonesha kupingana na Salaf us Salih na Ahlu sunnah wal Jama'a (ambapo hapa nawazungumzia sunni) kwenye nyanja tofauti.

Mpaka kufikia kuandikwa vitabu na wanazuoni wa kisunni kuonya juu ya fitna zao.

Vitabu kama Umara Al Baladil Haraam. Kilichoandikwa na mwalimu wa wanawazuoni huko Makka, Mufti wa madheheb ya Shafii, Sheikh Ahmad Bin Zayni Dahlan aliyekufa mwaka 1304 Hijiria sawa na mwaka 1887, Vitabu kama Fitnatul Wahabiyya (Fitna ya Mawahabi) n.k

Imam Naswawi ambaye ni mwanawazuoni wa kisunni anasema katika suratul fatwir aya ya 6 anasema mahawabiya wote ni Junudi Shayatwiin, jeshi la mashetani.

Kwa uchache ndiyo hivyo! Wewe si muislam na si sunni, hivyo huna cha kunifundisha mimi muislam ambaye ni sunni.

Na sunni huwezi kumsikia akigombana na Shia, au Ibadh n.k

Au kugombana na mkristo. Au kuchinja wakristo, Sunni hizo tabia hawana!

Sasa umkute wahabi aliyeiva kwenye itikadi utamkoma! Atakuona wewe ambaye si muislam hapa duniani umekuja kwa bahati mbaya! Yaani Imhotep hao unaowafurahia wakikudaka ndiyo mwisho wa kuchat hapa Jf.

Na Muislam ambaye hafuati msingi wa itikadi yao amepotea! Ukikaa vibaya muislam mwenzake huyo huyo wahabi atakupa jina la wewe ni mshirikina, kuchinjwa ni lazima. Yaani atamchinja muislam mwenzake.

Wewe endelea kusheherehekea na magaidi wenzako hao Isis.
 
Haya mambo ni makubwa hutoyaelewa, utaishia ku Google Google na kuleta ubishi kwa mambo ambayo hauna uelewa nayo!

Sunni itikadi yao Mungu hayupo mbinguni, bali mamlaka yake kayaweka mbinguni na hakuna kilichomfunga. Yaani kaepukana na mambo 6. Mungu hayupo juu(1) ya, au chini(2) ya, au kuliani (3) mwa, au kushoto(4) mwa, au mbele (5) ya, au nyuma (6) ya!

Wahabi itikadi yao Mungu yupo juu mbinguni!

Wahabi itikadi yao Mungu ana mkono, mguu n.k

Sunni itikadi yao Mungu hamithiliki na chochote kwa maana chochote hakifanani na Mungu na kaepukana na (jism) yaani sifa ya kuwa na mkono au mguu!

Sunni itikadi yao Mtume bado yu hai mpaka kaburini kwake pamoja na mitume mengine.

Wahabi itikadi yao Mtume ameshakufa! Yaani kama mpeleka barua, kapeleka barua na kazi yake imeshakwisha.

------------------
Mpaka hapo wanafanana?
Hance Mtanashati njoo upate darasa kwanza hapa
 
Hizo drones zinashambulia kutoka wapi kwa waasi au uturuki?
Kuna Waasi wa Kisunni waliojipenyeza karibia na Damascus halafu wanarusha Drone ndogo ndogo zenye Milipuko na kushambulia.
Source: Kanal 13
 
Vitabu mara nyingi ni Biashara mtu anaweza asitengeneze Soft Copy lakini hoja ya Sunni Shia imefafanuliwa vizuri Mitandaoni.
Doh!

Laa haula!!

Yaani Imam Suyutwi kitabu afanye biashara achukue maokoto!

Wakati ulimwengu wa kiislamu unamuita mujaddid.

Mtume Muhammad s.a.w anasema kwa kila baada ya miaka 100 anatokea mtu ambaye anaihuisha hii dini, anaifanyia upya!

Zama za Imam Suyutwi hiyo miaka 100 iliangukia zama zake. Wanawazuoni wanasema hii hadithi inamhusu yeye. Hivyo yeye ndiye aliyehuisha hii dini, ndiye mujaddid.

Huku Sheikh Imhotep anasema Imam Suyutwi kutoa vitabu ni kufanya biashara.

Umeshinda aisee! Mjadala wetu uishie hapa!
 
Wewe kwasasa ndio mbishi kuanzia Quruani nzima iko kwenye Internet kuna Islamic Chanel kwenye Internet kuna Historia ya Dini nzima ya Kiisilamu hadi jinsi Dhehebu la Shia lilivyopatikana sasa wewe unataka kumdanganya nani Shehe?!
We acha ujinga wewe hivi unafahamu mana ya Shia? Qur'an inaongelea hivi Qur'an 6.159

﴿إِنَّ الَّذِينَ فَرَّقُوا دِينَهُمْ وَكَانُوا شِيَعًا لَّسْتَ مِنْهُمْ فِي شَيْءٍ ۚ إِنَّمَا أَمْرُهُمْ إِلَى اللَّهِ ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا كَانُوا يَفْعَلُونَ﴾
[ الأنعام: 159]

Hakika walio igawa Dini yao na wakawa makundi makundi, huna ukhusiano nao wowote. Bila ya shaka shauri yao iko kwa Mwenyezi Mungu; kisha atawaambia yale waliyo kuwa wakiyatenda.

Indeed, you ˹O Prophet˺ are not responsible whatsoever for those who have divided their faith and split into sects. Their judgment rests only with Allah. And He will inform them of what they used to do.

Shia ni ku split into sects. We unadhani Qur'an ina Sunni, Shia, Ibadhi n.k

Kwa Allah hakuna wewe Shia au Sunni au Ibadhi ni kufata mafunzo ya Mtume Muhammad. Hizo Sect ni ujinga mtupu, sijui wameziogotea wapi, tumebaku mimi Shia au Sunni au Ibadhi wapi uislam ulileta haya kwenye Qur'an.

Uislam ni kuamini Mungu na Mtume Muhammad, kusali, kutoa zakaa, kufunga mwezi wa Ramadhani na kwenda Hijah mwenye uwezo wake. Hapo hakuna Ibadhi au Shia au Sunni.

Mimi namini ku split sect ni trick za wayahudi walichochea kwenye uislam, ili kuleta fitna kwenye Uislam siku za mbele kama tuonavyo sasa
 
Yaani Imam Suyutwi kitabu afanye biashara achukue maokoto!
Usiniingize kwenye Theolojia ya Kiislamu lakini ninachokwambia ni kwamba Internet imesheheni mambo mengi kuhusu Dini zote ikiwemo ya Kiislamu mambo kama Ushia na Usunni yamewekwa wazi.
 
We acha ujinga wewe hivi unafahamu mana ya Shia? Qur'an inaongelea hivi Qur'an 6.159

﴿إِنَّ الَّذِينَ فَرَّقُوا دِينَهُمْ وَكَانُوا شِيَعًا لَّسْتَ مِنْهُمْ فِي شَيْءٍ ۚ إِنَّمَا أَمْرُهُمْ إِلَى اللَّهِ ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا كَانُوا يَفْعَلُونَ﴾
[ الأنعام: 159]
Niondolee Sarakasi zenu zilizowafanya Leo hii muwe kama Vichaa na wenye kuchapwa na Dola mbali mbali.
 
Usiniingize kwenye Theolojia ya Kiislamu lakini ninachokwambia ni kwamba Internet imesheheni mambo mengi kuhusu Dini zote ikiwemo ya Kiislamu mambo kama Ushia na Usunni yamewekwa wazi.
Sawa!

Sasa hivi jihad yenu imefikia wapi? Mmeshateka mji?

Na mmempata Arab Zelensky! Naye anatinga magwanda kama Zelensky!
 
Back
Top Bottom