KWELI Dan Friedkin ana hifadhi ya ardhi kubwa Tanzania

KWELI Dan Friedkin ana hifadhi ya ardhi kubwa Tanzania

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Aprili 27, 2023, akaunti ya Mtandao wa Twitter inayotumia jina la MainLandAfrica iliweka chapisho linalodai kuwa Bilionea wa Marekani Dan Friedkin amekodisha takriban Ekari 6,000,000 za ardhi nchini Tanzania.

Chapisho hilo lilienda mbali zaidi kwa kudai kuwa Friedkin ni mmiliki wa Ekari zingine 25,000 za ardhi zinazounda pori la Akiba la Mwiba.

IMG_7879.jpeg

Wanaojua kuhusu huyu jamaa watupe details anafanya biashara gani na ardhi kubwa kiasi hicho?
 
Tunachokijua
Dan Friedkin alizaliwa 1965, ni mfanyabiashara na bilionea wa Marekani, mmiliki na Mkurugenzi Mtendaji wa The Friedkin Group na kampuni yake tanzu ya Gulf States Toyota, ambayo ilianzishwa na baba yake, Thomas H. Friedkin. Pia ni mmiliki na Rais wa klabu ya soka ya A.S. Roma.

Kwa mujibu wa Jarida la Forbes, hadi kufikia Februari 2023, makadirio ya utajiri wa Dan Friedkin ni dola bilioni 5.7.

Pamoja na hayo, Dan Friedkin ni mwekezaji katika kampuni ya usimamizi wa mahoteli ya kifahari ya Auberge Resorts na mfuko wa uhifadhi, Friedkin Conversation Fund.

Uwepo wao Nchini Tanzania
Friedkin Conservation Fund ni shirika linaloshughulika na masuala ya mazingira, uhifadhi na utalii. Shirika hili limesajiliwa Marekani. The Friedkin Conservation Fund of Tanzania ambayo ni sehemu ya umiliki wao limeanzishwa nchini Tanzania kama shirika lisilotengeneza faida.

Katika tovuti yao rasmi, Shirika hilo limeandika;

"Shughuli zetu Tanzania zimesukumwa na dhamira yetu katika uhifadhi wa mazingira na moyo wa hisani. Tumewekeza mabilioni ya shilingi katika jamii ili kuzisaidia kukuza uchumi na kusaidia nchi hii nzuri tunayoipenda sana"

Aidha, Shirika hilo limeonesha makao yake makuu kuwa Jiji la Arusha limetaja mambo 3 ambayo ni dhamira yake kuwepo nchini ambayo ni;
  1. Kusaidia Serikali ya Tanzania na wananchi wa wake kwa juhudi zao za kuhifadhi mtandao wa maeneo yaliyohifadhiwa.
  2. Kuhirikisha jamii za vijijini katika uhifadhi wa urithi wao wa asili na kuwawezesha kupunguza baadhi ya hali zinazochangia umaskini.
  3. Kufuatilia, kutafiti na kuwezesha mipango katika matumizi endelevu ya maliasili.

Uhifadhi wa Ardhi
Kwa mujibu wa tovuti ya Tanzania Invest, Friedkin Conservation Trust inahifadhi takriban ekari milioni 6.1 zilizoko kaskazini mwa Tanzania. Aidha Ekari 300,000 za hifadhi za Friedkin huruhusu wageni kutembelea na kuona wanyama kwenye mbuga ya Serengeti.

Madai haya yanathibitishwa pia na Blog hii inayohusianishwa na Taasisi hiyo. Aidha, Mwaka 2017, Mtumiaji mmoja wa JamiiForums aliwahi kuweka chapisho ambalo pamoja na mambo mengine lilikuwa linaonesha uwepo wa Taasisi hii kwenye hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Mwaka 2015, Friedkin Conversation Trust iliipa Tanzania Tsh Bilioni 231.55 ili kulinda mazingira na kukuza utalii.

Kazi zao nchini Tanzania zinatajwa kuanza miaka ya 1989 na Thomas Friedkin, Baba mzazi wa Dan Friedkin aliyefariki Machi 14, 2017 akiwa na umri wa miaka 81.

Hata hivyo, ingawa vyanzo kadhaa, ikiwemo makala katika jarida la Forbes inayosema kwamba taasisi inayomilikiwa na familia Freiedkin – yaani Friedkin Conservation Fund (friedkinfund.org) – imekodisha ekari milioni 6 za pori la Tanzania kwa lengo la kuzilinda, wawakilishi wa bilionea huyo walikanusha madai hayo.

"Friedkin Conservation Fund ni shirika la misaada lisilo la faida ambalo wadhamini wake ni Watanzania, na Dan Friedkin akiwa mfadhili ili kusaidia uhifadhi wa wanyamapori na maendeleo ya jamii," alinukuliwa akisema mwakilishi huyo.

Aidha, Septemba 4, 2023, Mwiba Holdings Limited na Thomas Dan Friedkin walitoa taarifa nyingine inayokanusha madai ya kumiliki eneo linalofikia ekari milioni 6 nchini Tanzania.

Sehemu ya taarifa yao iliyotolewa kwa umma ilisema jumla ya eneo lote lililopangishwa kwa kampuni ya Mwiba Holdings Limited wilayani Meatu ni kiasi cha ekari 171,604 - na si ekari milioni 6 kama inavyodaiwa na wale waliowaita kuwa ni wazushi.

Aidha, taarifa hiyo ilibainisha kuwa Kampuni ya Mwiba Holdings haimiliki eneo lolote kwenye maeneo ya hifadhi nchini Tanzania na kuwa haijaingia mkataba wowote (moja kwa moja au kupitia kwa mtu au taasisi nyingine) na Serikali ya Awamu ya Sita.

img_8412-jpeg.2738973

Barua ya ufafanuzi ya Mwiba Holdings Limited na Thomas Dan Friedkin
Mikataba yote ya UPANGAJI na UWEKEZAJI imekuwepo kwa muda mrefu na iliongezewa muda mwaka 2018 na 2019 wakati wa utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Hivyo, madai ya Thomas Dan Friedkin kuwa na hifadhi ya ardhi Tanzania yana ukweli japokuwa sio kwa kiasi cha ekari milioni 6 kama zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Aprili 27, 2023, akaunti ya Mtandao wa Twitter inayotumia jina la MainLandAfrica iliweka chapisho linalodai kuwa Bilionea wa Marekani Dan Friedkin amekodisha takriban Ekari 6,000,000 za ardhi nchini Tanzania.

Chapisho hilo lilienda mbali zaidi kwa kudai kuwa Friedkin ni mmiliki wa Ekari zingine 25,000 za ardhi zinazounda pori la Akiba la Mwiba.


Wanaojua kuhusu huyu jamaa watupe details anafanya biashara gani na ardhi kubwa kiasi hicho?
Huwa ninasema kila siku haijawahi kutokea mzungu kumpenda mwafrika hata siku moja. Huu tunaoita uhisani ni njia ya kupita tu kuchukua wanachokitaka katika ardhi ya Afrika.

Hakuna msaada anaopata mwafrika kwa mzungu zaidi ya maumivu.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Kila siku mnasema tuna mapori yapo yapo tu kumbe yamenunuliwa
Ni sawa tu kama mtu mweusi anamkatalia mweusi mwenzake kujenga kanyumba kwao kisa aliukana uraia ila mzungu anapewa ardhi yote hiyo kisa eti anawasaidia kuweka mazingira Safi

Kweli tuna akili za matope
Leo mzungu anakuambia naipenda Tanzania unachekelea
 
View attachment 2696387

HUYU MZUNGU NI MUWEKEZAJI WA MWIBA GAME RESERVE ANA HEKARI KARIBU 25.000 NDANI YA HIFADHI YA MBUGA ZA WANYAMA.

Na ana mpango wa kuchukuwa karibu Hekari 6 Milioni za Ardhi nchini mwetu Tanzania. Wa-Tanzania amkeni itafika siku nchi yetu yote imeuzwa na wawekezaji tutakuwa Wananchi hatuna ardhi ya kuishi kazi kwenu. Tanzania itakuwa kama nchi ya Zimbabwe siku zijazo ninatabiri hivyo.
Umeambiwa amekodisha (lease) sijui unaelewa..?
 
Wote hao wanaomiliki mapori sijui ya akiba,sijui vitalu vya uwindaji,sijui misitu sijui Nini,sijui mashamba makubwa.Sijui mahotel makubwa mbugani au beach
Hawa wanufaika na mambo mengine kabisa tofaut na hayo waliyosajiliwa nayo ambayo ni kiini macho.
Kwa sababu sisi tumelala hatuna macho.
Hawa wanafanya
1.Wanachimba madini kwa Siri maporini huko madini mengi yapo mbugani.
2.Wanadili na hazina za kale zikiwemo sites na ishu za mercury ya miamba.
3.Madawa ya kulevya
4.Silaha za magendo,
Mizigo inatoroshewa kwenye airport hizo za porini kwa private charter au wanatumiaa submarine ndogo usiku zinaibukia kwenye meli zilizopo deep sea.
Eti mzungu anatoka ulaya anakuja kulima nyanya,sijui parachichi Morogoro.
Hizo hotel za mbugani au beach nyingi ni meeting place za kufanyia wao biashara.
Zipo hotel mswahili uingii au Bei kubwa asiyomudu mswahili.Hizo Bei ni geresha tu ili kulimits watu hasa watz wasiyagundue wayafanyayo.
 
View attachment 2696387

HUYU MZUNGU NI MUWEKEZAJI WA MWIBA GAME RESERVE ANA HEKARI KARIBU 25.000 NDANI YA HIFADHI YA MBUGA ZA WANYAMA.

Na ana mpango wa kuchukuwa karibu Hekari 6 Milioni za Ardhi nchini mwetu Tanzania. Wa-Tanzania amkeni itafika siku nchi yetu yote imeuzwa na wawekezaji tutakuwa Wananchi hatuna ardhi ya kuishi kazi kwenu. Tanzania itakuwa kama nchi ya Zimbabwe siku zijazo ninatabiri hivyo.
aisee na tupo tu
 
Wazungu siyo washamba wakija huwa wanachunguza maeneo huwenda waligundua eneo hilo lina utajiri hapo chini
Kwa hiyo baadae utasikia ile mikataba ya nchi kupata asilimia 0.4 ya faida itakayopatikana

Aliye tuloga
 
Ahsante kwa taarifa. mnajitahidi kuuzima mjadala wa bandari...
Mjadala wa bandari umekaa vibaya sana hauzimiki kirahisi kwasababu hata hao wanao usifia mchana usiku ndio wanao chochea kuni.

Meki ma wodi.
 
Mwiba Holdings Company ya American Billionaire aitwaye Dan Friedkin anamiliki 6 milion acres (24,281 km square) katika Hifadhi za Taifa Magharibi mwa Ngorongoro na Kusini mwa Manyaroa National park ambako ni njia na wanyama wa kuhama yaani pofo, punda milia etc.

Ukubwa wa Tanzania in 945,000 km square.
Piga hesabu, 24,281/945,087X100 = 3% approx.

Kwa hivyo, Mr. Dan Friedkin anamiliki 3% ya ardhi bora ya Tanzania. Huyu ni mtu mmoja tu, je hao wengine na makampuni yao ni vipi.....

Ifike mahali Tanzanians tuhoji accountability ya ARDHI yetu. Ni kiasi gani ardhi yetu SALAMA, iko leased, sold na kwa mpango upi na faida gani.

Tunamtaka Controller and Auditor General (CAG) atupatie audited data za ardhi yetu kwa ripoti itakayotoka next time. CAG asiishie tu kukagua ofisi za serikali kwa mambo madogomadogo wakati ardhi imekwishauzwa na kuna siku tutakuja kutimuliwa na wenye ardhi.

Wamasai walikwishafukuzwa, huu ni mfano bora na wa uhakika.

NAWASILISHA.
 
Mwiba Holdings Company ya American Billionaire aitwaye Dan Friedkin anamiliki 6 milion acres (24,281 km square) katika Hifadhi za Taifa Magharibi mwa Ngorongoro na Kusini mwa Manyaroa National park ambako ni njia na wanyama wa kuhama yaani pofo, punda milia etc.

Ukubwa wa Tanzania in 945,000 km square.
Piga hesabu, 24,281/945,087X100 = 3% approx.

Kwa hivyo, Mr. Dan Friedkin anamiliki 3% ya ardhi bora ya Tanzania. Huyu ni mtu mmoja tu, je hao wengine na makampuni yao ni vipi.....

Ifike mahali Tanzanians tuhoji accountability ya ARDHI yetu. Ni kiasi gani ardhi yetu SALAMA, iko leased, sold na kwa mpango upi na faida gani.

Tunamtaka Controller and Auditor General (CAG) atupatie audited data za ardhi yetu kwa ripoti itakayotoka next time. CAG asiishie tu kukagua ofisi za serikali kwa mambo madogomadogo wakati ardhi imekwishauzwa na kuna siku tutakuja kutimuliwa na wenye ardhi.

Wamasai walikwishafukuzwa, huu ni mfano bora na wa uhakika.

NAWASILISHA.
Ulikuwa hujui?
 
Mwiba Holdings Company ya American Billionaire aitwaye Dan Friedkin anamiliki 6 milion acres (24,281 km square) katika Hifadhi za Taifa Magharibi mwa Ngorongoro na Kusini mwa Manyaroa National park ambako ni njia na wanyama wa kuhama yaani pofo, punda milia etc.

Ukubwa wa Tanzania in 945,000 km square.
Piga hesabu, 24,281/945,087X100 = 3% approx.

Kwa hivyo, Mr. Dan Friedkin anamiliki 3% ya ardhi bora ya Tanzania. Huyu ni mtu mmoja tu, je hao wengine na makampuni yao ni vipi.....

Ifike mahali Tanzanians tuhoji accountability ya ARDHI yetu. Ni kiasi gani ardhi yetu SALAMA, iko leased, sold na kwa mpango upi na faida gani.

Tunamtaka Controller and Auditor General (CAG) atupatie audited data za ardhi yetu kwa ripoti itakayotoka next time. CAG asiishie tu kukagua ofisi za serikali kwa mambo madogomadogo wakati ardhi imekwishauzwa na kuna siku tutakuja kutimuliwa na wenye ardhi.

Wamasai walikwishafukuzwa, huu ni mfano bora na wa uhakika.

NAWASILISHA.
Hatuna viongozi tunamadalali
 
hivi ni kweli huyu mzungu kapewa hii ardhi wakati sisi wengine hapa hapa tunaitafuta hiyo ardhi hatupewi? mwezetu amewapa nini au ametumia njia zipi? na anawekeza kitu gani na kwa masharti yepi?
 
Nilikuwa namsikia Lissu anazungumzia hii issue, kumbe kweli
 
Back
Top Bottom