Pre GE2025 Dar: Abdul Nondo atekwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Pre GE2025 Dar: Abdul Nondo atekwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Abdull Kazi

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
337
Reaction score
296
Screenshot_20241201_090450_X.jpg

Mwanasiasa Abdull Nondo wa Chama Cha ACT Wazalendo amechukuliwa asubuhi ya Leo na wati waliomvamia akiwa kituo Cha basi Mbezi.

Katika purukushani hiyo wahusika walidondosha pingu na sasa hatma yake haijulikani mpaka wakati huu

====

UPDATE

JamiiForums imewasiliana na Naibu Katibu wa Habari na Uenezi wa ACT Wazalendo Shangwe Ayo ambapo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, akieleza Nondo alikuwa ametokea Kigoma baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa kumalizika, ambapo wakati anashuka kwenye basi Stendi ya Magufuli watu wasiyojulikana watatu walimfuata kukawa na purukushani Nondo akijitahidi kujinasua lakini walifanikiwa kumchukua na kuangusha pingu walizokuwa wameenda nazo pamoja na begi alilokuwanalo Nondo

Matukio mengine ya utekaji kuwahi kufanyika nchini haya hapa: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana

Shangwe ameeleza pia gari lililomteka Nondo ni Land Cruiser nyeupe yenye namba za usajili T 249 EMV. Taarifa za awali walizitoa kwa mashuhuda ambao walikuwa wanamfagamu Nondo, baada ya kufungua begi lake kulikuwa na note book ambayo nayo ilithibisha kumilikiwa na Abdul Nondo

Pia shuhuda aliyekuwa eneo la tukio amesema gari hilo lililokuja kumteka Abdul Nondo lilikuwa na watu 4, wawili wakiwa na bunduki na wawili wakiwa mikono mitupu, watu walipoenda kuangalia kuna nini na kujaribu kuhoji waliwanyooshea bastola na hivyo watu kubaki wanaangalia tukio hilo likitokea na Abdul Nondo akawa ametekwa! Katika purukushani hizo kwa maelezo ya shuhuda mbali na pingu na bengi la Nondo, ilianguka pia inadaiwa simu ya moja ya watekaji ambavyo vyote vilikabidhiwa kwa Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Magufuli.

WhatsApp Image 2024-12-01 at 10.16.52_c5008028.jpg
 
Mwanasiasa Abdull Nondo wa Chama Cha ACT Wazalendo amechukuliwa asubuhi ya Leo na wati waliomvamia akiwa kituo Cha basi Mbezi.

Katika purukushani hiyo wahusika walidondosha pingu na sasa hatma yake haijulikani mpaka wakati huu
Katika purukushani hiyo wahusika walidondosha pingu na sasa hatma yake haijulikani mpaka wakati huu🥺🥺🥺
 
Mwanasiasa Abdull Nondo wa Chama Cha ACT Wazalendo amechukuliwa asubuhi ya Leo na wati waliomvamia akiwa kituo Cha basi Mbezi.

Katika purukushani hiyo wahusika walidondosha pingu na sasa hatma yake haijulikani mpaka wakati huu
Kwahiyo katika hiyo purukushani watu wameshindwa kumsaidia kweli? Au ulikuwa ukamataji wa kimya kimya? Nitashangaa kama Nondo alishindwa kuoiga hata kelele na kilasiku anashinda kwenye mitandao na tips za kuepuka kutekwa anazifahamu vizuri
 
Hivi utaratibu wa kumkamata mtuhumiwa si uko wazi Kwa mujibu wa Sheria?

Huyo Nondo ni Katibu wa Chama, ina maana ana address yake kwamba anaishi wapi

Mnafika Kwa mjumbe wa nyumba 10 kwenye Mtaa anaoishi kisha mnaenda kumchukua.

Hiyo kumvizia stendi na kumkamata kama jambazi inazua taharuki kwamba huenda ni Wasiojulikana

Hebu Viongozi wa hayo makundi sijui ni Usalama ama Polisi Idara ya Usalama, warudie kusoma miongozo ya kazi zao.

Najua mnatekeleza majukumu yenu, lakini fuateni Sheria na taratibu za kazi zenu
 
Hivi utaratibu wa kumkamata mtuhumiwa si uko wazi Kwa mujibu wa Sheria?

Huyo Nondo ni Katibu wa Chama, ina maana ana address yake kwamba anaishi wapi

Mnafika Kwa mjumbe wa nyumba 10 kwenye Mtaa anaoishi kisha mnaenda kumchukua.

Hiyo kumvizia stendi na kumkamata kama jambazi inazua taharuki kwamba huenda ni Wasiojulikana

Hebu Viongozi wa hayo makundi sijui ni Usalama ama Polisi Idara ya Usalama, warudie kusoma miongozo ya kazi zao.

Najua mnatekeleza majukumu yenu, lakini fuateni Sheria na taratibu za kazi zenu
Huko kumteka kwenda kumtesa....kumtisha misimamo yake au ndio kumuua kabisa....huko sio kukamata kawaida......
 
Back
Top Bottom