Pre GE2025 Dar: Abdul Nondo atekwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Pre GE2025 Dar: Abdul Nondo atekwa na Watu wasiojulikana katika mazingira ya utatanishi Kituo cha Mabasi cha Magufuli

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mwanasiasa Abdull Nondo wa Chama Cha ACT Wazalendo amechukuliwa asubuhi ya Leo na wati waliomvamia akiwa kituo Cha basi Mbezi.

Katika purukushani hiyo wahusika walidondosha pingu na sasa hatma yake haijulikani mpaka wakati huu
Atakuwa anapelekwa Burundi kwa nguvu.Tuliambiwa tuhame tukaleta ubishi.Tutahamishwa mmoja baada ya mwingine.Tutarudishwa wakati wa kuhesabu kura na kusaini matokeo tu.
 
1. Milishindwa kupiga picha wahusika?
2. Mlishindwa kupiga picha gari lao?
3. Hakuna alie weza hata kuchukua video ya tukio?
4. Walikua na silaha za moto?
5. Walikua wangapi?
6. Mlishindwa kuwahoji?
7. Mlishimdwa kuwazuwia wasimchukue?
 
Mwanasiasa Abdull Nondo wa Chama Cha ACT Wazalendo amechukuliwa asubuhi ya Leo na wati waliomvamia akiwa kituo Cha basi Mbezi.

Katika purukushani hiyo wahusika walidondosha pingu na sasa hatma yake haijulikani mpaka wakati huu
Duh CCM wanatakaje? Siku akipatikana IGP mwenye akili ndio itakua mwisho wa CCM
 
Pole sana ndugu yetu Abdul, mwenyezi Mungu akupiganie wakuachilie salama.

Lakini Abdul kwa level aliyofikia, alitakiwa awe hata na ka vitz jamani, sass watu wanakuja kukutekea stand, tena stendi ya mbezi shamba.
 
1. Milishindwa kupiga picha wahusika?
2. Mlishindwa kupiga picha gari lao?
3. Hakuna alie weza hata kuchukua video ya tukio?
4. Walikua na silaha za moto?
5. Walikua wangapi?
6. Mlishindwa kuwahoji?
7. Mlishimdwa kuwazuwia wasimchukue?
Jibu ni hapana kwa maswali yote.Lsbda,kwenye udaku,udakuzi na ajali ndiyo tutakuletea fotografia zote bila chenga muhishimiwa mbonge!🙏
 
Huko kumteka kwenda kumtesa....kumtisha misimamo yake au ndio kumuua kabisa....huko sio kukamata kawaida......
Ingekuwa Nchi zenye msimamo, huu Uhuni usingeruhusiwa

Lakini pia Viongozi wa hivyo vikosi kazi vyao wangekuwa wanawajibishwa

Angalia ishu ya Trump kufanyiwa lile shambulio, hadi Mkuu wa Idara aliitwa kuhojiwa kisha akaamua mwenyewe kujiondoa kwenye nafasi yake

Shida ya hawa Viongozi wetu, wanafanya kazi Kwa maelekezo ya Maboss wao
 
Hivi utaratibu wa kumkamata mtuhumiwa si uko wazi Kwa mujibu wa Sheria?

Huyo Nondo ni Katibu wa Chama, ina maana ana address yake kwamba anaishi wapi

Mnafika Kwa mjumbe wa nyumba 10 kwenye Mtaa anaoishi kisha mnaenda kumchukua.

Hiyo kumvizia stendi na kumkamata kama jambazi inazua taharuki kwamba huenda ni Wasiojulikana

Hebu Viongozi wa hayo makundi sijui ni Usalama ama Polisi Idara ya Usalama, warudie kusoma miongozo ya kazi zao.

Najua mnatekeleza majukumu yenu, lakini fuateni Sheria na taratibu za kazi zenu
Sasa kama anaetakiwa kuwakumbusha hizo taratibu zao nankuwachukulia hatua ndo huyo huyo anaewatuma hapo unategemea nini
 
Sasa kama anaetakiwa kuwakumbusha hizo taratibu zao nankuwachukulia hatua ndo huyo huyo anaewatuma hapo unategemea nini
Hakuna accountability kabisa kwenye hii Nchi

Na bahati mbaya Wananchi wenyewe hatujaamka kuwawajibisha hawa watu

Anatendewa jirani unasema huyo sio Mimi

Kesho anatendewa mtoto wa mjomba ako, utasema sio Mimi

Keshokutwa unachukuliwa wewe mwenyewe ndiyo una ona umuhimu wa kuwawajibisha hao watu

Wanachokifanya ni Uhuni na ni kinyume na Sheria za Nchi
 

Mwanasiasa Abdull Nondo wa Chama Cha ACT Wazalendo amechukuliwa asubuhi ya Leo na wati waliomvamia akiwa kituo Cha basi Mbezi.

Katika purukushani hiyo wahusika walidondosha pingu na sasa hatma yake haijulikani mpaka wakati huu
Tunamaliza uchaguzi haya yanatokea, mbona tunaenda kubaya
 
Humu coment nyingi ni za kulaumu, niwaambie kwenye Historia ya Dunia hainyoeshi kokote kule ambako mabadiliko yalitokea kupitia kulalamika.

Keybord woriour tuendelee kulaumu kama ilivyo jadi yetu.

Na pia niwatikie kulaumu kwema
 
Tanzania bado ni nchi ya kimasikini kuanzia akili , kipato na maarifa

Kiongozi Mkubwa Kama huyo anakamatwaje kizembe namna hiyo.

Anashindwa kutembea na ulinzi mkubwa wa silaha .

Anapandaji mabasi ya Abiria

Anakamatwaje bila hata kuwapiga Picha wahusika.

MTU Kama Abdul Nondo ambaye huwa anatambulika hadi Kwa vyama washirika huko ulaya Leo hii anakamatwa style hii


Ni vizuri Kama Chama Kama Wananchi na Taifa tukapaza sauti zetu kuyapinga haya mambo ambayo hayana utu wala hekima.


Rais -unauwezo wa Kutoa kauli maana hawa watu wanaofanya huu mchezo hawatoki uraiani.

Yupo wapi Thadeo ole Mushi ambaye kaondolewa kimagumashi.
 

Mwanasiasa Abdull Nondo wa Chama Cha ACT Wazalendo amechukuliwa asubuhi ya Leo na wati waliomvamia akiwa kituo Cha basi Mbezi.

Katika purukushani hiyo wahusika walidondosha pingu na sasa hatma yake haijulikani mpaka wakati huu
Mimi nafiri government ingetoa tamko kua km mazingira yanautata na kunawatu wanaweza zuia wafanye kinachowezekana,wananchi wanahofia kufanya maamuzi kwakua hawana backup ila km kuna utata wananchi wanaruhusiwa kuingilia kati,sehemu km stand ya mbezi wapo watu wengi wanaoweza zuia but wanahofia usalama wao pia
 
Back
Top Bottom