DAR: Akram Aziz akamatwa, afikishwa Mahakama ya Kisutu. Ana makosa 75!

DAR: Akram Aziz akamatwa, afikishwa Mahakama ya Kisutu. Ana makosa 75!

Naichukia hao Wahindi toka enzi za EPA na Richmond. Siwezi geuka kuwa mtetezi wao hata siku moja.
Ndipo akili zako zilipoishia, kwani EPA walijilipa? Acheni upoyoyoyo baada ya kuichukia CCM unawachukia watanzania wenzako, kisa tu wana Asili ya Asia!!
 
So kweli kabisa. Wengi wanaotaka tuamini wamefanikiwa hawasemi wametumia njia gani kupata hayo mafanikio.
Kufanikiwa kwa sababu ya kuwa jangili sio mafanikio....kuiba hela za wananchi kwa rushwa na ufisadi sio mafanikio.
Leo hii wengi waliotumia nafasi zao kwa dhuluma wanaona sifa tuwanyenyekee kama role model wa mafanikio.
Naamini katika haki. Kila mtu avune anachopanda. Ukweli peke yake ndio utatuweka huru
Kwani huyo Jiwe na Bashite wanatajirika kwa hela gani?
 
Wabongo bwana, watu mmeshataifishiwa 1.5 Tilioni hiyo hamjui kama hela, sijui mnajua nia aina ya utawala au demokrasia? Watu wanawachanganya kwa sinema za kutungwa, ili kuwapumbaza akili na kuwaaminisha kuwa ile milioni 50 kwa kila kijiji anayo Akram!!
 
Watanzania tuamke!!! Mazingira haya yametengenezwa tu, kama taarifa ya mwanzo ilivyosema kua "askari wamemkamata akiwa na vibali sahihi, ila wakaamua kuondoka navyo vibali vyote original na kukataa kuacha copy ofisini kwake". Hapa kama kawaida, serekali inatuhamisha toka maswala fulani kutupeleka kwengine. Tumeshafanywa kama watoto wa chekechea sasa!!!

Watanzania lini tutapata akili jamani ya kuchanganua mambo na ukweli????? Tulishuhudia YUSUF MANJI alikamatwa na akafikishwa mahakamani kwa kukutwa na NYARA ZA SEREKALI, MIHURI YA JESHI, VITAMBAA VYA SARE ZA JESHI. Case iliishia wapi?????? Nani anaehoji mpaka sasa kuhusu hio tuhuma zake au case alizoshitakiwa nazo?????? Kama kweli angeachiwa huru????

Inasikitisha sana kuona mtu akitetea uonevu unaofanywa na askari kwa raia, na uongo tunaopewa raia na serekali yetu, kama huu na iliopita.

Na inasikitisha zaidi kuona wafanya biashara wakubwa wakionewa mpaka kufikia hatua wanafunga biashara zao na watanzania wenzetu kibao wanakosa ajira.
Mkuu kuna vibari vya kuwinda tembo?
 
Watanzania tuamke!!! Mazingira haya yametengenezwa tu, kama taarifa ya mwanzo ilivyosema kua "askari wamemkamata akiwa na vibali sahihi, ila wakaamua kuondoka navyo vibali vyote original na kukataa kuacha copy ofisini kwake". Hapa kama kawaida, serekali inatuhamisha toka maswala fulani kutupeleka kwengine. Tumeshafanywa kama watoto wa chekechea sasa!!!

Watanzania lini tutapata akili jamani ya kuchanganua mambo na ukweli????? Tulishuhudia YUSUF MANJI alikamatwa na akafikishwa mahakamani kwa kukutwa na NYARA ZA SEREKALI, MIHURI YA JESHI, VITAMBAA VYA SARE ZA JESHI. Case iliishia wapi?????? Nani anaehoji mpaka sasa kuhusu hio tuhuma zake au case alizoshitakiwa nazo?????? Kama kweli angeachiwa huru????

Inasikitisha sana kuona mtu akitetea uonevu unaofanywa na askari kwa raia, na uongo tunaopewa raia na serekali yetu, kama huu na iliopita.

Na inasikitisha zaidi kuona wafanya biashara wakubwa wakionewa mpaka kufikia hatua wanafunga biashara zao na watanzania wenzetu kibao wanakosa ajira.
Toa mfano wa mfanyabiashara mkubwa alie fungasha!
 
Kipindi cha bwana yule waliachwa wakafanya wanayotaka cc tunakula nyama ya ngo'mbe wao hawakuijuwa ni kupiga mnyama wanayemtaka mbugani awe na vibali halal asiwe na vibali hakuna wakuuliza,nakumbuka ukikamata watu kama hao unapigiwa simu na mkuu wako ana kwambia (kwani ungewaacha ungeathirika nini)maneno kama hayo yalikatisha tamaa katika kipindi cha bwana yule,ndiyo maana tukiona yanayofanywa hadi sasa wapingaji wakubwa ni watu wenye fedha na wengine wamo ndani ya serikari na chama chao kwa ujumla
 
Mkuu kuna vibari vya kuwinda tembo?
Wewe sio Kuwanda tembo, ni vibali vya kununua meno ya tembo. Acha kuchanganya mambo. Hayo meno serikali ikisha yakamata kutoka sehemu yoyote haramu, huyapiga mnada. Huyo Akram alinunua serikalini hayo meno 4, na hizo rifle ni siraha za kuwindia wanyama kwenye mapoli ya akiba jamani. Tufike sehemu tukiona utoto tunaujua na kuupuzia.
 
Tupe hiyo taarifa ya serikali kupiga mnada wa meno ya tembo kwa Akram,ni lini mkuu,na wapi? Una supporting documents kutetea hoja yako? Kama huna utakuwa unapuyanga tu,pia usiwe na mtazamo hasi eti anaonewa!
 
Mkuu kuna vibari vya kuwinda tembo?
Tanzania sheria inaruhusu kuwinda tembo, ila kwa watalii tu, yani kwa kibali cha uwindaji wa kitalii na malipo ni kwa Dollar$ tu. Na serekali imeweka bei maalum kisheria kwa uwindaji huo.
Screenshot_2018-10-31-16-47-13-1.jpg
Screenshot_2018-10-31-16-47-18-1.jpg
Screenshot_2018-10-31-16-47-24-1.jpg
 
Kweli mteja ni mteja!nikupe ukweli nyie wanasheria msingesema ukweli zaidi ya maneno kama hayo
 
Wewe sio Kuwanda tembo, ni vibali vya kununua meno ya tembo. Acha kuchanganya mambo. Hayo meno serikali ikisha yakamata kutoka sehemu yoyote haramu, huyapiga mnada. Huyo Akram alinunua serikalini hayo meno 4, na hizo rifle ni siraha za kuwindia wanyama kwenye mapoli ya akiba jamani. Tufike sehemu tukiona utoto tunaujua na kuupuzia.
Vibali vya kupiga tembo vipo, kama visitishwa sasa hivi hilo ni jambo lingine ila nakuthibitishia nimefanyakazi kwenye hiyo industry, msidanganywe kafala namna hii.

Kinachowapata hawa watu kwa sasa ni KARMA.
 
inabidi nitafutu mtu wa kunielekeza maana na aina za utakatishaji fedha, maana imekuwa kesi ya kila siku nisije jikuta nakosea na mimi.
 
Back
Top Bottom