TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Kama MTU anatekwa Katikati ya mji, kitovu cha Nchi! Anauwawa na mwili wake unatupwa Jirani tu hapa, je tuko salama kama Nchi?? Who's next? Tunajuaje usalama WA VIONGOZI wetu kama upo? Ununio na magogoni sio mbali, ununio kuna VIONGOZI wakubwa Sana wanaishi huko, je usalama wao ukoje?? Haya wacha tuone who's next....
Mkuu wakati wanapitisha sheria za kuwalinda wakishafanya mauwaji hukujuwa consequences zake?

Mimi wala sishangai.
 
Anaandika Boniyai kutoka Account yake ya X
View attachment 3090046
View attachment 3090047

======


Ali Mohamed Kibao Ameuawa

Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu umekutwa hospitali ya Mkoa wa Kinondoni,Mwananyamala katika chumba cha kuhifadhia maiti mwili wake ukiwa UMEHARIBIWA VIBAYA SANA.

Mwili wa ALI MOHAMED KIBAO ulikutwa umetupwa jana alfajiri maeneo ya UNUNIO (jirani na viwanja vya NSSF) ukiwa na majereha makubwa sehemu za usoni kiasi ndugu zake walipata tabu kuutambua kirahisi.

ALI MOHAMED KIBAO alikamatwa na watu wanao dhaniwa kuwa ni askari wa Jeshi la Polisi eneo la TEGETA, mbele ya Jengo la KIBO COMPLEX baada ya gari mbili za Jeshi za Polisi za Landcruiser hardtop nyeupe kuzuia (block) basi la TASHIRIF lenye namba T 343 EES alilokuwa amepanda ALI MOHAMED KIBAO kutoka Dar es saalam kuelekea nyumbani kwao Mkoani Tanga.

Kwa bahati nzuri wakati wote wa tukio likitendeka ndani ya gari palikuwa na askari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani (Traffic) ambaye alikuwa kiti cha mbele kama abiria na alishuhudia tukio lote, anatambulika kama MACHIWA anayepatikana kwa namba 0652484802.

Namba ya simu aliyokuwa anatumia ALI MOHAMEDKIBAO ni +255 624 724 247 mpaka wakati anatekwa na kwenda kuuwawa,pia ndiyo namba ambayo mara kadhaa waliomteka walikuwa wakimpigia kuhakiki kama ni yeye.

Kwa mujibu wa wenyeji wa UNUNIO ambao ni walima mchicha, wanasema Jana asubuhi walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi baada ya Kuona mwili wa Mtu mzima, mweupe mwenye asili ya Kiarabu ambaye baadae Jana jioni ndugu waliutambua kuwa ni mwili ALI MOHAMED KIBAO ukiwa na majeraha.

Kabla ya umauti wake ALI MOHAMED KIBAO aliwahi kuwa afisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akastaafu na kujiunga na CCM,baadae akachaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Tanga wakati wa Rais Kikwete,na baadae alijiunga CHADEMA.

Baada ya mauaji haya ya Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA na Msaidizi wa Katibu Mkuu kuwawa idadi ya Viongozi wa CHADEMA wakiotekwa inaongezeka
1. Dioniz Kipanya 2. Kombo Bwana Twaha 3. Godwin Mlay 4. Deusdedith Soka 5. Frank Mbise.


Soma Pia:
Boniface Jacob
Ex-Mayor
0712 239 595
🥲🥲
 
Kuna rafiki yangu mmoja ana cheo kichama.
Nimesoma nae na hata ghetto tulikaa nae Sana
Aliwai nambia ✍️ Dr am 4 real PhD wewe ni jembe na ni very potential unakubalika na una ushawishi kwa watu wanao kuzunguka na jamii kwa ujumla wake.
Nikamjibu: Sipendi Mambo ya siasa KABISA Kuna undumila kuwili mwingi mno.

Humu Jf Kuna brainy nyingi sanaaa Ila zipo mbali na SIASA sababu ya factors nyingi nyingi Kama hizi.

Apumzike kwa amani tuviachie vyombo vya ulinzi na usalama zitende kazi yake.
 
Baada ya Kuutambua kwa sasa wanasubiri uchunguzi wa Madaktari.

Screenshot_2024-09-08-12-07-27-1.png
 
Uchunguzi utafanyika kwa mujibu wa mtuhumiwa, tumeambiwa wameingia kwenye basi wakiwa na bunduki, wakajitambulisha kama sheria inavyotaka, wakasema wanamtaka mzee Mohamed, wakampiga pingu,wakaondoka naye, kisha kumuua na kumtupa ununio!! It looks exactly like a dog, walk like a dog and bark like a dog! Yes its a Dog!!
 
Wakimalizana na Chadema watarudi ccm na wakimalizana na ccm watarudi na wataongeza kasi ya kuwamaliza wananchi wakosoaji.

Eva ni zao la Magufuli na atapita njia zile zile za mwendazake.

Uzuri wanajua Midanganyika inalalama tu na haiwezi kuchukua hatua. Ni kupiga tu domo mitandaoni.
 
Back
Top Bottom