TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Tabia ya viongozi kuchukulia wepesi mambo magumu kama haya ya utekaji,utesaji na uuaji si nzuri hata kidogo.Intelijensia mara zote ni wakinzani tu kwamba wataleta fujo.Lakini,hayo ya utekaji na uuaji intelijensia haina macho iyaone kabla?Nchi inaenda kuwa kiroja kabisa.
 
Kuna msemo: karma is real.

Kwa kuzingatia huo msemo, kesho na keshokutwa, linaweza kutokea jambo kama adhabu kwa haya yanayoendelea na hamtoweza kuamini.

Binafsi sitaki kuingia ndani sana kuhusu hilo, balli naacha Nature/muda ndio utaamua.

Swali: Yakitokea, mtataka tuungane kuomboleza?

Jibu: Msijidanyanye, watu watashangilia kwani avunacho mtu, ndicho apandacho.
Mluu nimestushwa sana na member mwenzetu kujijasirisha na akafungua uzi kuwatuhumu CHADEMA kuwa wanahusika na hivi vifo.

Huu ujasiri na intention ya kuspin imelindwa na online mods.

Tupo kwenye hatari kubwa sana sana. Na watu wanaleta dhihaka na mabezo.

Umenena kweli
 
Hii kitu inamchafua sana Mh. Rasi Mama Samia, asipofanya maamuzi mazito kukemea haya yanayoendelea hii nchi itamfia mikononi mwake.

Very sad new indeed.
Naona kashtuka katoa pole kwa familia, muhimu aache kuwa muoga yeye kama amri jeshi mkuu avunje kikosi kazi husika na ikiwezekana wajulikane na wafikishwe kwenye vyombo vya sheria ili haki itendeke.
 
Hizi ni ndoto. Amkeni mfanye jambo
Kwa taarifa yako, kilichompata Jiwe nilionya 2015 wakati wanamkejeli Lowassa kuwa Ikulu sio wodi ya wagonjwa.

Nakumbuka niliandika kwa mafumbo nikawaonya CCM na mgombea wao na miaka 6 baadae yalitokea.

Ni bahati mbaya, baada ya muda mchache, ule uzi sikuuona tena hapa Jukwaani, nahisi mods waliufuta.
 
Usijekujaribu kuandamana, Hawa watu wamejipanga, Dola ni zao, watawamaliza, ziko njia mbadala za kushughulika nao.
Hakuna nguvu ya dola iliyowahi ishinda nguvu ya umma.

Kumalizwa hatabila kuandamana watakumaliza tu kwani hao waliouawa na kumalizwa waliandamana?

Leo mzee wetu, hatujui kesho ni nani? Inaweza kuwa wewe au mimi. Bila kupiga kelele, tutakuwa kama kondoo mbele ya Fisi mkuu.

Tanzania ni yetu sote.
 
Anaandika Boniyai kutoka Account yake ya X
View attachment 3090046
View attachment 3090047

======


Ali Mohamed Kibao Ameuawa

Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu umekutwa hospitali ya Mkoa wa Kinondoni,Mwananyamala katika chumba cha kuhifadhia maiti mwili wake ukiwa UMEHARIBIWA VIBAYA SANA.

Mwili wa ALI MOHAMED KIBAO ulikutwa umetupwa jana alfajiri maeneo ya UNUNIO (jirani na viwanja vya NSSF) ukiwa na majereha makubwa sehemu za usoni kiasi ndugu zake walipata tabu kuutambua kirahisi.

ALI MOHAMED KIBAO alikamatwa na watu wanao dhaniwa kuwa ni askari wa Jeshi la Polisi eneo la TEGETA, mbele ya Jengo la KIBO COMPLEX baada ya gari mbili za Jeshi za Polisi za Landcruiser hardtop nyeupe kuzuia (block) basi la TASHIRIF lenye namba T 343 EES alilokuwa amepanda ALI MOHAMED KIBAO kutoka Dar es saalam kuelekea nyumbani kwao Mkoani Tanga.

Kwa bahati nzuri wakati wote wa tukio likitendeka ndani ya gari palikuwa na askari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani (Traffic) ambaye alikuwa kiti cha mbele kama abiria na alishuhudia tukio lote, anatambulika kama MACHIWA anayepatikana kwa namba 0652484802.

Namba ya simu aliyokuwa anatumia ALI MOHAMEDKIBAO ni +255 624 724 247 mpaka wakati anatekwa na kwenda kuuwawa,pia ndiyo namba ambayo mara kadhaa waliomteka walikuwa wakimpigia kuhakiki kama ni yeye.

Kwa mujibu wa wenyeji wa UNUNIO ambao ni walima mchicha, wanasema Jana asubuhi walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi baada ya Kuona mwili wa Mtu mzima, mweupe mwenye asili ya Kiarabu ambaye baadae Jana jioni ndugu waliutambua kuwa ni mwili ALI MOHAMED KIBAO ukiwa na majeraha.

Kabla ya umauti wake ALI MOHAMED KIBAO aliwahi kuwa afisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akastaafu na kujiunga na CCM,baadae akachaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Tanga wakati wa Rais Kikwete,na baadae alijiunga CHADEMA.

Baada ya mauaji haya ya Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA na Msaidizi wa Katibu Mkuu kuwawa idadi ya Viongozi wa CHADEMA wakiotekwa inaongezeka
1. Dioniz Kipanya 2. Kombo Bwana Twaha 3. Godwin Mlay 4. Deusdedith Soka 5. Frank Mbise.


Soma Pia:
Boniface Jacob
Ex-Mayor
0712 239 595
Another sad sad day kwa Watanzania. Haitoshi kwa IGP au Mkuu wa Usalama kuujiuzulu. Waziri wa Mambo ya Ndani ni lazima awe wa kwanza kujiuzulu. Vyombo vya usalama haviwezi kujichunguza.
 
Back
Top Bottom