BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Deodatus Thadei Luhela, Mhasibu wa Kampuni ya ‘Your Home Choice’’ amekamatwa kwa kutoa taarifa za uongo akidai Majambazi walimjeruhi na kumpora fedha za Mwajiri wake.
Mtuhumiwa alifungua kesi ya unyang'anyi kituo cha Polisi Chang’ombe, baada kubanwa kwa maswali ya Askari, aliwapeleka Chanika Kitunguu na kuonesha fedha hizo.
Jeshi la Polisi limewatahadharisha Wananchi juu ya tabia ya kutoa taarifa za uongo kuwa ni kosa na ikibainika watachukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja kufikishwa Mahakamani.
=====================
“Tukio limetokea November 14,2022 eneo la Chang’ombe Temeke ambapo Mtuhumiwa huyo alidai tarehe hiyo majira ya saa 3:30 asubuhi alikamatwa na Majambazi wawili waliokuwa na gari nyeusi baada ya kumtishia kwa silaha baadae akaingizwa kwenye gari ambapo walimjeruhi mkono wa kushoto na shavuni, na kumpora fedha alizokuwa nazo na baadae kumtupa maeneo ya Gongo la Mboto njia panda ya Pugu na Mbezi alijikongoja hadi kituo cha Polisi kidogo cha Gongo la Mboto ambako alipewa PF. 3 kwaajili ya matibabu.
“Baada ya tukio hilo majira ya saa 8 :00 mchana Mtuhumiwa huyo alifungua kesi kituo cha Polisi Chang’ombe ya unyang’anyi na kuporwa tsh 60,000,000, Makachero wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam walimuhoji kwa kina na kubaini kuwa taarifa hizo zilikuwa ni za uongo na ilipofika tarehe 15/11/2022 majira ya saa 8 :00 mchana Mtuhumiwa aliwaongoza Askri hadi Chanika Kitunguu alipokuwa amezificha pesa hizo”
“Jeshi la Polisi linawatahadharisha Wananchi juu ya tabia ya kutoa taarifa za uongo kwa Maafisa wa Serikali kuwa ni kosa na ikibainika watachukuliwa hatua stahiki kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja kufikishwa Mahakamani”
POLISI KANDA MAALUM DAR
Mtuhumiwa alifungua kesi ya unyang'anyi kituo cha Polisi Chang’ombe, baada kubanwa kwa maswali ya Askari, aliwapeleka Chanika Kitunguu na kuonesha fedha hizo.
Jeshi la Polisi limewatahadharisha Wananchi juu ya tabia ya kutoa taarifa za uongo kuwa ni kosa na ikibainika watachukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja kufikishwa Mahakamani.
=====================
“Tukio limetokea November 14,2022 eneo la Chang’ombe Temeke ambapo Mtuhumiwa huyo alidai tarehe hiyo majira ya saa 3:30 asubuhi alikamatwa na Majambazi wawili waliokuwa na gari nyeusi baada ya kumtishia kwa silaha baadae akaingizwa kwenye gari ambapo walimjeruhi mkono wa kushoto na shavuni, na kumpora fedha alizokuwa nazo na baadae kumtupa maeneo ya Gongo la Mboto njia panda ya Pugu na Mbezi alijikongoja hadi kituo cha Polisi kidogo cha Gongo la Mboto ambako alipewa PF. 3 kwaajili ya matibabu.
“Baada ya tukio hilo majira ya saa 8 :00 mchana Mtuhumiwa huyo alifungua kesi kituo cha Polisi Chang’ombe ya unyang’anyi na kuporwa tsh 60,000,000, Makachero wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam walimuhoji kwa kina na kubaini kuwa taarifa hizo zilikuwa ni za uongo na ilipofika tarehe 15/11/2022 majira ya saa 8 :00 mchana Mtuhumiwa aliwaongoza Askri hadi Chanika Kitunguu alipokuwa amezificha pesa hizo”
“Jeshi la Polisi linawatahadharisha Wananchi juu ya tabia ya kutoa taarifa za uongo kwa Maafisa wa Serikali kuwa ni kosa na ikibainika watachukuliwa hatua stahiki kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja kufikishwa Mahakamani”
POLISI KANDA MAALUM DAR