Dar: Anayedaiwa kumuua mwanafunzi wa UDSM akamatwa, akiri kufanya tukio hilo

Dar: Anayedaiwa kumuua mwanafunzi wa UDSM akamatwa, akiri kufanya tukio hilo

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na operasheni kali ya kuzuia vitendo vya kihalifu ikiwa ni pamoja na kuwasaka wahalifu waliotenda makosa ya kijinai ya siku za nyuma katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.​


Katika hatua hiyo Polisi wamemkamata GADI DAUDI@ tito Jeshi la mtu mmoja (28) Mkazi wa Ubungo Riverside kwa tuhuma za kumuua JULIUS FREDRICK (22) Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kumpora simu yake ya mkononi .Tukio hilo lilitokea tarehe 16/07/2022 majira ya saa kumi usiku huko eneo la karibu na hosteli za Magufuli Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam baada ya kumvizia, kumshambulia na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili, kupora vitu vyake ikiwemo simu na kumsababishia kifo.

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam lilifanya upelelezi na ufuatiliaji wa kina na tarehe 27/07/2022 lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo maeneo ya Sinza, Kinondoni, baada ya kumuhoji kwa kina alikiri kumuua mwanafunzi huyo na kumpora vitu vyake na alikiri pia kufanya matukio kama hayo ya unyanganyi kwenye maeneo tofauti ya jiji la Dar es Salaam, Uchunguzi wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa mtuhumiwa huyo ni mhalifu sugu ambaye amekuwa akifanya matukio ya kiuhalifu maeneo ya Mlimani city, Mwenge na Kawe, na aliwahi kushtakiwa kwa kesi ya UNYANG’ANYI WA KUTUMIA SILAHA kesi No. 256/2020 na kufungwa miaka 30 kuanzia tarehe 6 Julai 2020, na aliachiwa huru Aprili 2022 kwa sababu za kisheria baada ya kukata rufaa.

Tarehe 1.8.2022 majira ya saa kumi na nusu jioni Mtuhumiwa alikubali kuwapekeleka askari kuwaonesha alipoficha silaha anazotumia katika uhalifu na simu ya marehemu aliyoipora katika vichaka vilivyopo eneo la katikati ya Mlimani city na Hostel za Magufuli.

Baada ya kufika eneo hilo alikurupuka na kuanza kukimbia kuelekea kwenye vichaka vya ndani zaidi. Askari walifyatua risasi tatu hewani kumtahadharisha kusimama lakini alikaidi na hivyo kulazimika kumzuia kwa risasi iliyomjeruhi kwenye paja la mguu wa kushoto, kuanguka chini na kukamatwa kutoka katika jaribio la kutoroka chini ya ulinzi huku akikabiliana na tuhuma nzito za mauaji . Alipelekwa hospitali kwa matibabu. Eneo hilo Polisi imepata panga moja, sime, bisibisi na simu mbili za mkononi.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam liendelea na msako mkali kuwakamata wahalifu wote wanaojihusisha na vitendo vya kihalifu na malengo ni kuhakikisha watu wanafanya shughuli zao katika mazingira yaliyo salama , bila hofu na kwa kuzingatia sheria za nchi.

Muliro J. MULIRO – ACP​

KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
HONGERENI JESHI LETU, MTU WA AINA HII WA NINI SASA.....!
 
Sasa kufungwa miaka 30 na kuachiwa kwa rufaa kwani ushahidi ulikuwa na shaka.

Sometimes polisi wakiamua wanaweza.
 
Hujui.l wewe mara ingine mtuhumiwa kusema twende nikawaonyeshe wengine tunaoshirikiana nao walipojificha
Kumbe Muongo anataka kutoroka
Yes mkuu ila kuna tatizo kubwa na police wetu, huyu ni suspect wa ujambazi na uuaji why aongozane na police bila ya kufungwa pingu hasa za miguuni?,hapo kwangu nimeona trigger happy police, ndio maana hili jeshi lifumuliwe na tuanze upya, tukio hili police wangekua no suspect wa mauaji ,ninahitaji IPID ndani ya jeshi hili
 
Huwa wanapewa mawakili wa serikali kuwatetea. It happens so many times and it is an established rule of law to provide them with legal assistance in case one can not afford one of his own!
Hatujafika level hizo.
 
Afande Mulilo, ina maana mlimpeleka bila kumtia pingu? Eleza ukweli kwamba hamkutaka kusumbuana mahakamani maana anaweza kutoka kwa technicalities
We ulitaka afanikiwe kutoroka au ulitaka afanikiwe kuachiwa tena mahakamani kwa technicality?
 
Kuna boda zinazagaa sana usiku maeneo mengi buguruni, taifa, mjini kati esp samora, mitaa ya ifm, upanga, sea view, morocco, salender nk wanatembea wawili (mshkaki) na silaha hasa panga, visu. wakikuta mtu holela wanamchangamkia fasta by the time raia wakijitokeza kutoa msaada jamaa washatambaa na kuacha majeraha kadhaa. nmeshuhudia zaidi ya mara 3 situation kama hizo.
IPO HAJA BODABODA ZIPANGIWE MUDA WA KAZI, SAA 12 ASB MPAKA SAA 3 USIKU, BAADA YA MUDA HUO INAYOONEKA IPEWE KIBANO NA ITOE MAELEZO SAHIHI YA KUELEWEKA,
BODABODA ZA BIASHARA WAENDESHAJI WOTE WAWE NA KAVAZI MAALUM KENYE NAMBA MGONGONI, NA KIBALI KINGINE MAALUM CHA UTAMBULISHO JUU YA MWENDESHA BODABODA NA MDHAMINI WAKE MMOJA MWAJIRIWA SEREKALINI.
 
Voda fasta ..huku walifanya tukio mchana bahati mbaya au nzuri pt iko nyuma na barabara ina mitaro pande zote mirefu .. boda boda cc 150 inavutwa haitembei mbele ya cruza ...walipewa ngao moja kila mtu analia kwa staili yake huko mtaroni
Kuna boda zinazagaa sana usiku maeneo mengi buguruni, taifa, mjini kati esp samora, mitaa ya ifm, upanga, sea view, morocco, salender nk wanatembea wawili (mshkaki) na silaha hasa panga, visu. wakikuta mtu holela wanamchangamkia fasta by the time raia wakijitokeza kutoa msaada jamaa washatambaa na kuacha majeraha kadhaa. nmeshuhudia zaidi ya mara 3 situation kama hizo.
 
Yes mkuu ila kuna tatizo kubwa na police wetu, huyu ni suspect wa ujambazi na uuaji why aongozane na police bila ya kufungwa pingu hasa za miguuni?,hapo kwangu nimeona trigger happy police, ndio maana hili jeshi lifumuliwe na tuanze upya, tukio hili police wangekua no suspect wa mauaji ,ninahitaji IPID ndani ya jeshi hili
Kwa nini unaamini polisi wamesema ukweli ?
 

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na operasheni kali ya kuzuia vitendo vya kihalifu ikiwa ni pamoja na kuwasaka wahalifu waliotenda makosa ya kijinai ya siku za nyuma katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.​


Katika hatua hiyo Polisi wamemkamata GADI DAUDI@ tito Jeshi la mtu mmoja (28) Mkazi wa Ubungo Riverside kwa tuhuma za kumuua JULIUS FREDRICK (22) Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kumpora simu yake ya mkononi .Tukio hilo lilitokea tarehe 16/07/2022 majira ya saa kumi usiku huko eneo la karibu na hosteli za Magufuli Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam baada ya kumvizia, kumshambulia na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili, kupora vitu vyake ikiwemo simu na kumsababishia kifo.

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam lilifanya upelelezi na ufuatiliaji wa kina na tarehe 27/07/2022 lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo maeneo ya Sinza, Kinondoni, baada ya kumuhoji kwa kina alikiri kumuua mwanafunzi huyo na kumpora vitu vyake na alikiri pia kufanya matukio kama hayo ya unyanganyi kwenye maeneo tofauti ya jiji la Dar es Salaam, Uchunguzi wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa mtuhumiwa huyo ni mhalifu sugu ambaye amekuwa akifanya matukio ya kiuhalifu maeneo ya Mlimani city, Mwenge na Kawe, na aliwahi kushtakiwa kwa kesi ya UNYANG’ANYI WA KUTUMIA SILAHA kesi No. 256/2020 na kufungwa miaka 30 kuanzia tarehe 6 Julai 2020, na aliachiwa huru Aprili 2022 kwa sababu za kisheria baada ya kukata rufaa.

Tarehe 1.8.2022 majira ya saa kumi na nusu jioni Mtuhumiwa alikubali kuwapekeleka askari kuwaonesha alipoficha silaha anazotumia katika uhalifu na simu ya marehemu aliyoipora katika vichaka vilivyopo eneo la katikati ya Mlimani city na Hostel za Magufuli.

Baada ya kufika eneo hilo alikurupuka na kuanza kukimbia kuelekea kwenye vichaka vya ndani zaidi. Askari walifyatua risasi tatu hewani kumtahadharisha kusimama lakini alikaidi na hivyo kulazimika kumzuia kwa risasi iliyomjeruhi kwenye paja la mguu wa kushoto, kuanguka chini na kukamatwa kutoka katika jaribio la kutoroka chini ya ulinzi huku akikabiliana na tuhuma nzito za mauaji . Alipelekwa hospitali kwa matibabu. Eneo hilo Polisi imepata panga moja, sime, bisibisi na simu mbili za mkononi.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam liendelea na msako mkali kuwakamata wahalifu wote wanaojihusisha na vitendo vya kihalifu na malengo ni kuhakikisha watu wanafanya shughuli zao katika mazingira yaliyo salama , bila hofu na kwa kuzingatia sheria za nchi.

Muliro J. MULIRO – ACP​

KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
Mtu kaua halafu polisi wanamchekea.

HUO NI UPUMBAVU WA KIWANGO CHA JUU
 
Afande Mulilo, ina maana mlimpeleka bila kumtia pingu? Eleza ukweli kwamba hamkutaka kusumbuana mahakamani maana anaweza kutoka kwa technicalities
Hili swali kama ungemtupia kama uko naye lazima angepatwa na kigugumizi na kutokwa na kijasho flani hivi cha hofu...
 
Hatujafika level hizo.
level ipi? sijakuelewa? kwani hujui kuwa serikali inawawekea advocates watu, hasa kesi kama za mauaji watuhumiwa ambao hawana mawakili? siyo civil cases, NO!
 
Back
Top Bottom