Marathon day
JF-Expert Member
- Jan 31, 2020
- 643
- 1,016
Soon tutasema R.l.PNilivyosoma "alikurupuka na kuanza kukimbia....." nikawaza ohoooo ndugu katafuteni mwili mochwari. Bahati yake kama yupo hai.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Soon tutasema R.l.PNilivyosoma "alikurupuka na kuanza kukimbia....." nikawaza ohoooo ndugu katafuteni mwili mochwari. Bahati yake kama yupo hai.
Kibaka anakuwa na silaha ya moto?Hawakumfunga pingu kwa sababu ni kibaka tu na sio gaidi 😀
HONGERENI JESHI LETU, MTU WA AINA HII WA NINI SASA.....!Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na operasheni kali ya kuzuia vitendo vya kihalifu ikiwa ni pamoja na kuwasaka wahalifu waliotenda makosa ya kijinai ya siku za nyuma katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.
Katika hatua hiyo Polisi wamemkamata GADI DAUDI@ tito Jeshi la mtu mmoja (28) Mkazi wa Ubungo Riverside kwa tuhuma za kumuua JULIUS FREDRICK (22) Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kumpora simu yake ya mkononi .Tukio hilo lilitokea tarehe 16/07/2022 majira ya saa kumi usiku huko eneo la karibu na hosteli za Magufuli Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam baada ya kumvizia, kumshambulia na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili, kupora vitu vyake ikiwemo simu na kumsababishia kifo.
Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam lilifanya upelelezi na ufuatiliaji wa kina na tarehe 27/07/2022 lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo maeneo ya Sinza, Kinondoni, baada ya kumuhoji kwa kina alikiri kumuua mwanafunzi huyo na kumpora vitu vyake na alikiri pia kufanya matukio kama hayo ya unyanganyi kwenye maeneo tofauti ya jiji la Dar es Salaam, Uchunguzi wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa mtuhumiwa huyo ni mhalifu sugu ambaye amekuwa akifanya matukio ya kiuhalifu maeneo ya Mlimani city, Mwenge na Kawe, na aliwahi kushtakiwa kwa kesi ya UNYANG’ANYI WA KUTUMIA SILAHA kesi No. 256/2020 na kufungwa miaka 30 kuanzia tarehe 6 Julai 2020, na aliachiwa huru Aprili 2022 kwa sababu za kisheria baada ya kukata rufaa.
Tarehe 1.8.2022 majira ya saa kumi na nusu jioni Mtuhumiwa alikubali kuwapekeleka askari kuwaonesha alipoficha silaha anazotumia katika uhalifu na simu ya marehemu aliyoipora katika vichaka vilivyopo eneo la katikati ya Mlimani city na Hostel za Magufuli.
Baada ya kufika eneo hilo alikurupuka na kuanza kukimbia kuelekea kwenye vichaka vya ndani zaidi. Askari walifyatua risasi tatu hewani kumtahadharisha kusimama lakini alikaidi na hivyo kulazimika kumzuia kwa risasi iliyomjeruhi kwenye paja la mguu wa kushoto, kuanguka chini na kukamatwa kutoka katika jaribio la kutoroka chini ya ulinzi huku akikabiliana na tuhuma nzito za mauaji . Alipelekwa hospitali kwa matibabu. Eneo hilo Polisi imepata panga moja, sime, bisibisi na simu mbili za mkononi.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam liendelea na msako mkali kuwakamata wahalifu wote wanaojihusisha na vitendo vya kihalifu na malengo ni kuhakikisha watu wanafanya shughuli zao katika mazingira yaliyo salama , bila hofu na kwa kuzingatia sheria za nchi.
Muliro J. MULIRO – ACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
Hatujafika level hizo kiongozi.Patamu
Yes mkuu ila kuna tatizo kubwa na police wetu, huyu ni suspect wa ujambazi na uuaji why aongozane na police bila ya kufungwa pingu hasa za miguuni?,hapo kwangu nimeona trigger happy police, ndio maana hili jeshi lifumuliwe na tuanze upya, tukio hili police wangekua no suspect wa mauaji ,ninahitaji IPID ndani ya jeshi hiliHujui.l wewe mara ingine mtuhumiwa kusema twende nikawaonyeshe wengine tunaoshirikiana nao walipojificha
Kumbe Muongo anataka kutoroka
Hata muuaji bila kipondo hawezi kukubali kuwa ni yy.Anakkiri kwakuwa anapewa kipondo kizito ila huenda sio yy
Hatujafika level hizo.Huwa wanapewa mawakili wa serikali kuwatetea. It happens so many times and it is an established rule of law to provide them with legal assistance in case one can not afford one of his own!
We ulitaka afanikiwe kutoroka au ulitaka afanikiwe kuachiwa tena mahakamani kwa technicality?Afande Mulilo, ina maana mlimpeleka bila kumtia pingu? Eleza ukweli kwamba hamkutaka kusumbuana mahakamani maana anaweza kutoka kwa technicalities
Unampelekaje vichakani confessed killer bila pingu za mikono na miguu?Hujui.l wewe mara ingine mtuhumiwa kusema twende nikawaonyeshe wengine tunaoshirikiana nao walipojificha
Kumbe Muongo anataka kutoroka
Ila za Hao majambazi wanaochinja wanachuo ndio ziko straight??Statement za polisi hazijawahi kuwa straight
IPO HAJA BODABODA ZIPANGIWE MUDA WA KAZI, SAA 12 ASB MPAKA SAA 3 USIKU, BAADA YA MUDA HUO INAYOONEKA IPEWE KIBANO NA ITOE MAELEZO SAHIHI YA KUELEWEKA,Kuna boda zinazagaa sana usiku maeneo mengi buguruni, taifa, mjini kati esp samora, mitaa ya ifm, upanga, sea view, morocco, salender nk wanatembea wawili (mshkaki) na silaha hasa panga, visu. wakikuta mtu holela wanamchangamkia fasta by the time raia wakijitokeza kutoa msaada jamaa washatambaa na kuacha majeraha kadhaa. nmeshuhudia zaidi ya mara 3 situation kama hizo.
Kuna boda zinazagaa sana usiku maeneo mengi buguruni, taifa, mjini kati esp samora, mitaa ya ifm, upanga, sea view, morocco, salender nk wanatembea wawili (mshkaki) na silaha hasa panga, visu. wakikuta mtu holela wanamchangamkia fasta by the time raia wakijitokeza kutoa msaada jamaa washatambaa na kuacha majeraha kadhaa. nmeshuhudia zaidi ya mara 3 situation kama hizo.
Kwa nini unaamini polisi wamesema ukweli ?Yes mkuu ila kuna tatizo kubwa na police wetu, huyu ni suspect wa ujambazi na uuaji why aongozane na police bila ya kufungwa pingu hasa za miguuni?,hapo kwangu nimeona trigger happy police, ndio maana hili jeshi lifumuliwe na tuanze upya, tukio hili police wangekua no suspect wa mauaji ,ninahitaji IPID ndani ya jeshi hili
Mtu kaua halafu polisi wanamchekea.Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na operasheni kali ya kuzuia vitendo vya kihalifu ikiwa ni pamoja na kuwasaka wahalifu waliotenda makosa ya kijinai ya siku za nyuma katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.
Katika hatua hiyo Polisi wamemkamata GADI DAUDI@ tito Jeshi la mtu mmoja (28) Mkazi wa Ubungo Riverside kwa tuhuma za kumuua JULIUS FREDRICK (22) Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kumpora simu yake ya mkononi .Tukio hilo lilitokea tarehe 16/07/2022 majira ya saa kumi usiku huko eneo la karibu na hosteli za Magufuli Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam baada ya kumvizia, kumshambulia na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili, kupora vitu vyake ikiwemo simu na kumsababishia kifo.
Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam lilifanya upelelezi na ufuatiliaji wa kina na tarehe 27/07/2022 lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo maeneo ya Sinza, Kinondoni, baada ya kumuhoji kwa kina alikiri kumuua mwanafunzi huyo na kumpora vitu vyake na alikiri pia kufanya matukio kama hayo ya unyanganyi kwenye maeneo tofauti ya jiji la Dar es Salaam, Uchunguzi wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa mtuhumiwa huyo ni mhalifu sugu ambaye amekuwa akifanya matukio ya kiuhalifu maeneo ya Mlimani city, Mwenge na Kawe, na aliwahi kushtakiwa kwa kesi ya UNYANG’ANYI WA KUTUMIA SILAHA kesi No. 256/2020 na kufungwa miaka 30 kuanzia tarehe 6 Julai 2020, na aliachiwa huru Aprili 2022 kwa sababu za kisheria baada ya kukata rufaa.
Tarehe 1.8.2022 majira ya saa kumi na nusu jioni Mtuhumiwa alikubali kuwapekeleka askari kuwaonesha alipoficha silaha anazotumia katika uhalifu na simu ya marehemu aliyoipora katika vichaka vilivyopo eneo la katikati ya Mlimani city na Hostel za Magufuli.
Baada ya kufika eneo hilo alikurupuka na kuanza kukimbia kuelekea kwenye vichaka vya ndani zaidi. Askari walifyatua risasi tatu hewani kumtahadharisha kusimama lakini alikaidi na hivyo kulazimika kumzuia kwa risasi iliyomjeruhi kwenye paja la mguu wa kushoto, kuanguka chini na kukamatwa kutoka katika jaribio la kutoroka chini ya ulinzi huku akikabiliana na tuhuma nzito za mauaji . Alipelekwa hospitali kwa matibabu. Eneo hilo Polisi imepata panga moja, sime, bisibisi na simu mbili za mkononi.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam liendelea na msako mkali kuwakamata wahalifu wote wanaojihusisha na vitendo vya kihalifu na malengo ni kuhakikisha watu wanafanya shughuli zao katika mazingira yaliyo salama , bila hofu na kwa kuzingatia sheria za nchi.
Muliro J. MULIRO – ACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAM.
Hili swali kama ungemtupia kama uko naye lazima angepatwa na kigugumizi na kutokwa na kijasho flani hivi cha hofu...Afande Mulilo, ina maana mlimpeleka bila kumtia pingu? Eleza ukweli kwamba hamkutaka kusumbuana mahakamani maana anaweza kutoka kwa technicalities
level ipi? sijakuelewa? kwani hujui kuwa serikali inawawekea advocates watu, hasa kesi kama za mauaji watuhumiwa ambao hawana mawakili? siyo civil cases, NO!Hatujafika level hizo.
Mkuu kwangu police hapa wameongopa,hakuna ukweli hapa kabisa ,huwezi kwenda site na suspect (murder)bila back up ya kutosha au bila pingu za miguuni, it's craze wenzetu mpaka wanatumia tag kwa suspectKwa nini unaamini polisi wamesema ukweli ?