Dar es Salaam: Gharama za kujifungua ni Tshs 75,000. Uchaguzi huu unakupa nafasi ya kukataa uharamia huu

Dar es Salaam: Gharama za kujifungua ni Tshs 75,000. Uchaguzi huu unakupa nafasi ya kukataa uharamia huu

Wajawazito wanaojifungulia kwenye Hospitali ya Rufaa ya Temeke , wale wanaojifungua kwa njia ya kawaida inawalazimu kulipia pesa taslimu ya kitanzania shilingi elfu 75 kama gharama ya kuzaa , Wale wanaojifungua kwa njia ya upasuaji wanapaswa kulipa zaidi ya Tsh laki 2 na yaweza hata kufika laki 2 unusu kutegemeana na complications .

Gharama hizi hazijumuishi gharama ya vifaa ambavyo mjamzito anapaswa kuingia navyo chumba cha uzazi ikiwemo pamba na gloves.

Kwahiyo basi uchaguzi huu unakupa nafasi ya kuchagua kuendelea kulipia gharama ya kuzaa au la , wale waliotuaminisha kwamba tuendelee kufyatua watoto kwa vile elimu ni bure ni vema wangeanzia kuondoa hii kodi ya kuzaa ili mambo yawe mepesi zaidi na kuwezesha wananchi kufyatua watoto kwa amani zaidi .
Kama umeona ghali si uende kwa bibi uzalie nyumbani? Ulitaka nani akulipie kwenye starehe zako? Hakuna cha bure hapa ulimwenguni, wewe kila siku umo humu ulitaka nani akulipie hizo MB? Wacha kelele!
 
Kadema bwana! kujifungua ni jambo la furaha...yaani miezi 9 yote najiandaa kupata mtoto nashindwaje kuweka hela kidogo kidogo hadi nifikishe hizo pesa? Ila pia hiyo ni gharama kwa wale wanaotaka kujifungua kwa huduma za "private" ...ndio kuna sehemu private kwenye hospitali za umma kwa wasiopenda bugudha!
 
Mkuu upo sahihi kabisa mke wangu alienda kujifungulia Amana hosptal kwa njia ya operation nilishangaa kuambiwa natakiwa kulipia 200,000 kama gharama ya kujifungua na 49,000 ya dawa.

Nilielekezwa dirisha la kulipia na nililipia kihalali kabisa na risiti nikapewa.

Ni wamama wote walifuata utaratibu huu na nilishuhudia mama mmoja akizuiwa kuondoka wodini baada ya ndugu zake kushindwa kulipa gharama hii.
Vya bure viliisha enzi ya Mwalimu JK Nyerere kwa sababu ya ujinga wa wengi, wao kila kitu wanataka bure wakati kodi hawataki kulipa. Hata nchi kubwa zilizoendelea kama UK huwezi kutibiwa kama wewe huna uraia wa hiyo nchi na wewe sio mlipa kodi/raia wa nchi hiyo. USA wameshindwa itakuwa Tanzania? Hatutaki watalii wagonjwa kufilisi manufaa ya walipa kodi wa Tanzania.
 
Huu ni uongo kabisa. Mwanafamila wangu amejifungulia kaloleni hospitali. Hatukulipa hata senti moja. Ilkua mwezi wa sita, na huduma ilikuwa Safi Sana, usafi wodini, huduma ya mama na mtoto imeimarishwa Sana Tanzania. Hakuna hizo garama kwenye hospitali ya serkali

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app

Ata Kama ni bure lakini sioni kosa lolote la kulipia huduma ya mama kujifungua kwa usalama zaidi kumbuka hao ndo wanaongoza kuchangiana hadi birthday za kila mtu na harusi za kila siku. Vitu vingine ni unafiki kulalamika bana akiona hiyo gharama ni kubwa basi ajifungulie nyumbani. Huduma za afya ni gharama dunia nzima. Watu tunapenda sana vya bure. Simchangui yoyote maana ata kadi ya mpiga kura sina. Kila la Heri kwa yeyote atakayeshinda
 
Hospitali ya Temeke ni hospitali ya rufaa. Gharama za matibabu pamoja na bei za dawa na huduma nyinginezo zimewekwa kwa bango na siyo kwa kificho. Kwa maneno mengine hauhitaji uwe na risiti kuthibitisha hizo gharama.
 
MKuu unalipa Kodi kweli wewe?
unajua kuw akuna mpaka ufadhili kw aajkili ya mama na mtoto, kutibiwa bure na kujifungua bure?
unajua kuna grants na loans jina la mama na mtoto?
Mkuu post zako sijaziona muda mrefu sana, karibu sana, happy to see you around.
 
Mbona serikali kujifungua hulipi kitu hata kwa operation Sana una lipia hela ya kitanda kwa siku elfu tano
 
Kadema bwana! kujifungua ni jambo la furaha...yaani miezi 9 yote najiandaa kupata mtoto nashindwaje kuweka hela kidogo kidogo hadi nifikishe hizo pesa? Ila pia hiyo ni gharama kwa wale wanaotaka kujifungua kwa huduma za "private" ...ndio kuna sehemu private kwenye hospitali za umma kwa wasiopenda bugudha!
Kwamba kuna sehemu za private kwenye hospital za uma?
Unaelewa unachoongea kweli? Umeambiwa mpk jina la hospital bado unakaza mishipa ya shingo.
Mimi naongezea Vijibweni hospital ya Kigamboni nayo wanatoza kawaida ni 40 na operation kuanzia laki moja.
Ukitaka ushahidi nenda.
 
Kwamba kuna sehemu za private kwenye hospital za uma?
Unaelewa unachoongea kweli? Umeambiwa mpk jina la hospital bado unakaza mishipa ya shingo.
Mimi naongezea Vijibweni hospital ya Kigamboni nayo wanatoza kawaida ni 40 na operation kuanzia laki moja.
Ukitaka ushahidi nenda.
Bro unabishana na wanafunzi? Watakutoa kibiomgo bure hao hata bando wanaomba kwa mama zao watajua wapi gharama za hospital.
 
Mkuu acha uvivu wa kufanya utafiti unaweza kwenda kwenye hospital nilizokutajia kama upo Dar.
Ama tafuta mawasiliano ya uongozi wa hospital hasa kuanzia referral hospital then ulizia utapata jibu.

Kuna haja gani ya mimi kudanganya?
Sipo karibu tu sehemu risiti zilipo ningeweka humu sijui ungesemaje mkuu.
Utakapofika tutumie risiti tuone, mimi ninavyojua hakuna malipo ndio maana nataka utupe uthibitisho hapa ili tuanzie hapo.
 
Kama umeona ghali si uende kwa bibi uzalie nyumbani? Ulitaka nani akulipie kwenye starehe zako? Hakuna cha bure hapa ulimwenguni, wewe kila siku umo humu ulitaka nani akulipie hizo MB? Wacha kelele!
Mkuu tunataka JPM atulipie , anahamasisha dada,mama,wadogo zetu wafyatue ,kwani kufyatua kwawingi nayonimaendeleo.
 
Mbona serikali kujifungua hulipi kitu hata kwa operation Sana una lipia hela ya kitanda kwa siku elfu tano
HOSPITAL YA KITETE MKOA WA TABORA UNALIPIA, ELFU 50 KAMA MZAZI AKIJIFUNGUA MTOTO WAKIUME, ELFU 40 KAMA MTOTO WAKIKE. SIJUI KAMA TOZO ZIPO KIHALALI LAKINI NILAZIMA KULIPIA
 
HOSPITAL YA KITETE MKOA WA TABORA UNALIPIA, ELFU 50 KAMA MZAZI AKIJIFUNGUA MTOTO WAKIUME, ELFU 40 KAMA MTOTO WAKIKE. SIJUI KAMA TOZO ZIPO KIHALALI LAKINI NILAZIMA KULIPIA
Labda hospital zinatofautiana aisee maana hyo hospital niliyoenda ni ya Rufaa, na ulikuwa hulipii kitu
 
Labda hospital zinatofautiana aisee maana hyo hospital niliyoenda ni ya Rufaa, na ulikuwa hulipii kitu
Hospital ya kitete niyarufaa pia, nasijui kwa nini wametofautisha gharama kwa mtoto wakike na kiume. Lakini lazima mzazi alipie baada yakujifungua .Na Mimi nashangaa kusikia hospital zingine hawalipii nilijua ndio utaratibu wa nchi nzima. Mpaka thread yake niliwahi ileta humu kuulizia kama nihalali.
 
Back
Top Bottom