Dar: Kijana mbaroni kwa kumuua mama yake mzazi

Dar: Kijana mbaroni kwa kumuua mama yake mzazi

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linamshikilia Julius Mzava (26) Mkazi wa eneo la usalama Chang’ombe Wilaya ya Temeke kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Magdalena Peter (56) kwa kumchoma kisu sehemu ya mwili wake.

Tukio hili limetokea tarehe 08/10/2021 saa 1:05 usiku eneo la Sandali Chang’ombe wakati marehemu(Magdalena Peter) alipoiingia chumbani kwa mtoto wake Julius Masawe(mtuhumiwa) kwa nia ya kumpa chakula na hapo ndipo aliposhambuliwa kwa kisu eneo la mwili wake akapata majeraha makubwa yaliyopelekea kupoteza kwa maisha yake licha ya jitihada za kumpeleka hospitali kufanyika.

Mtuhumiwa Julius Masawe (mtoto wa marehemu) amekamatwa, anahojiwa kwa kina na atafikishwa mahakamani kama sehemu ya hatua muhimu za kisheria.

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limewakamata na linawashikilia watu watano(5) kwa tuhuma za kujihusisha na wizi wa vifaa vya magari na kupokea vifaa/vipuri vya magari vya wizi.

Watuhumiwa hao walikamatwa na vifaa mbalimbali vya magari zikiwemo taa za magari aina ya Toyota IST na milango ya magari ya aina mbalimbali.

Aidha, vitu mbalimbali vilivyokuwa vimeibiwa na wahalifu kwenye matukio mbalimbali ya uvunjaji vimekamatwa katika kituo cha Polisi Goba yakiwemo majenereta zaidi ya 25,vifaa mbalimbali vya ujenzi na mitungi ya gesi 10.

MULIRO J. MULIRO
KAMANDA WA POLISI
KANDA MAALUM DAR ES SALAAM
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linamshikilia Julius Mzava (26) Mkazi wa eneo la usalama Chang’ombe Wilaya ya Temeke kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Magdalena Peter (56) kwa kumchoma kisu sehemu ya mwili wake.


KAMANDA WA POLISI
KANDA MAALUM DAR ES SALAAM
Yaani Official Police Statement ndio wameshindwa kujua jina la Mtuhumiwa? Huku ni Julius Mzava huku para nyingine anatajwa Julius Masawe! Duh
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linamshikilia Julius Mzava (26) Mkazi wa eneo la usalama Chang’ombe Wilaya ya Temeke kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Magdalena Peter (56) kwa kumchoma kisu sehemu ya mwili wake.
Julius Mzava (Mpare)
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linamshikilia Julius Mzava (26) Mkazi wa eneo la usalama Chang’ombe Wilaya ya Temeke kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Magdalena Peter (56) kwa kumchoma kisu sehemu ya mwili wake.



MULIRO J. MULIRO
KAMANDA WA POLISI
KANDA MAALUM DAR ES SALAAM
Mbona mnatuchanganyia habari ni Julius Mzava ama Julius Massawe? para ya kwanza na yapili kama haziendani hivi, which is which
 
usiku eneo la Sandali Chang’ombe wakati marehemu(Magdalena Peter) alipoiingia chumbani kwa mtoto wake Julius Masawe(mtuhumiwa)
Julius Masawe??

Yupi ni yupi? Au kwa kuwa Wachaga na Wapare ni Watani basi mkaamua kuwatumia hivyo hivyo?
 
Yaani Official Police Statement ndio wameshindwa kujua jina la Mtuhumiwa? Huku ni Julius Mzava huku para nyingine anatajwa Julius Masawe! Duh
Labda wale wa Mama wa kutype ndiyo wamekosea, maana wanakuwaga ni watu wazima kidogo,hasa wengi utawakuta kwenye office za Serekali,na wengi wao ndiyo vitengo vyao,hapo unakuta Mmama watu kawekewa mabarua karibu hamsini ya kutype,hapo ni mwendo wa kubuuluza tu!!
 
Back
Top Bottom