DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Mkuu kwa jambo hili ipo wazi Makonda kakosea.
Anaweka vitisho kujaribu kuzuia kutekelezwa kwa sheria halali sio tamko binafsi la kiongozi flani.

Alichofanya Dk. Philip Mpango ni kwenda kuondoa wasiwasi kwa umma ili sheria ikitekelezwa basi mali ziuzike bila shida.

Hapo waziri kaenda kufanya kazi ya mawasiliano kwa umma. Angeweza kumuagiza afisa alie chini yake lakini huyo anaweza kuwa chini kiitifaki kumpinga mkubwa wake kiitifaki.
Nimeeleza hapojuukwamba sina tatizo na Waziri kutimiza wajibu wakekwa kufuata sheria.

Magufuli alimpongeza trafiki aliyemzodoa mke wa Balozi Dr. Waziri Mahiga, kwa minajili ya kwamba serikalihii haijali wewe mkubwa, mke wa mkubwa wala nani, hapa kazi tu. That was debatable given the proctacted circumstances,na yule mama alijaribu kujirudi na ku contain ile situation lakini ikawa too late.

Kwa hiyo, kama suala ni "hapa kazi tu" na Waziri anafanya kazi yake, nimeshasema hapo juu Makonda kakosea.

Ila mimi ni mtu wa kutaka uongozi wa old school decorum, Mzee Mwinyi anakwambia enzi zao wanasoma, mwanafunzi ukionekana unatembea barabarani huku unakula, mwalimu wako akakuona "unakula majiani", ukifika shule ni fimbo.

Kwa nini unakosa ustaarabu wa kukaa kitako ukiwa unakula?

Labda hii old schooldecorum iko out of touch na reality, lakini sisi tuliokua enzi za serikali ya Mwalimu Nyerere, tunakumbuka enzi ambayo serikali ya Tanzania viongozi walifanya kazi kwa nidhamu ya hali ya juu, angalau machonipetu.

Kama walikuwa na beef zao, tunakuja kuzisikia wakati washatangulia mbeleya haki,kutoka kwa insiders huko.

Enzi hizo huwezi kusikia Mkuu wa Mkoa anabishana na Waziri kwenye vyombo vya habari,regardless ya nani kakosea na nani kapatia, viongozi wa serikali moja kukozana kupitia vyombo vya habari ni utovu wa nidhamu.

Serikali inaendeshwa kwa imani.

Mizozo ya viongozi wa serikali moja kati yao, ina ondoa imani ya wananchi kwenye serikali kiujumla bila kujali nani kakosea na nani kapatia.

Jay-Z aliimba katika "Takeover"

"A wise man once told me, don't argue with a fool. Cause people from a distance, can't tell who is who".

Mpango angepiga mnada tu hayo makontena bila kuzozana, tuone hiyo laana ingeanzia wapi.
 
Hivyo vifaa haviendi kuuzwa Bali vinaenda kutumiwa na walimu tena wa serikali Kwa nini serikali isiangalie hili Kwa jicho LA pili?sheria hizi sio msahafu kuwa haziwezi kugeuzwa kidogo Kwa maslahi ya taifa naamini Iko njia ya kupita kumaliza hili bila vikwazo-makonda hoyeee
mi naamini kama sheria za kodi haziruhusu kutoa izo mali bila kodi pia sheria izo izo zimemruhusu raisi kutoa msamaha wa kodi kwa bidhaa yoyote ile so kwanini haoni sakata hili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Laana imrudie mwenyewe anaedanganya mara sio makontena yake mara diaspora wamempa[emoji849]
Diaspora ipi ya kumpa vitu vya bil 10 ..
Na Bado
 
Hii ni poul Makonda not RC against wizara ya fedha sio mamlaka mbili za uteuzi kulumbana ni mamlaka v/s mtu binafsi ambaye alishapewa utaratibu lkn hajafata

Sent using Jamii Forums mobile app
That's even worse.

Waziri angemdharau na kunadi tu vitu bila majibizano mengi, kwa sababu wananchi wakiona viongozi wanajibizana, bila kujali ni mtu na taasisi au taasisi na taasisis, na nani kapatia na nani kakosea, ule mzozanotu ni negative energy inayoondoa imani ya wananchi katika serikali.

Sasa hawa watu washatengeneza uadui, kesho wakitakiwa kukaa pamoja kwa manufaa ya umma, badala ya kuanza kazi, itabidi wanze usuluhishi kwanza.

Some schoolyard mentality, sio national leadership.

Natambua Makonda ana makosa, ila nafadhaika sana viongozikuzozana regardless ya nani kakosea.

Viongozi hawatakosa kukosea, ila wakishindwa kumaliza mizozo yao kwenye vikao wakajibizana kwenye vyombo vya habari, hilo linaonesha mapungufu makubwa sana katiak uongozi wetu.
 
kwani kutokana na sheria za kodi raisi si anauwezo wa kutoa msamaha wa kodi kwenye bidhaa yoyote anayoona inafas kupewa kodi kwanini yuko kimya asimsaidie raisi wa dareesalaam akaamuru tax exemption kama kweli mzigo ni wa msaada

Sent using Jamii Forums mobile app
Msamaha wa kodi hautolewi na Rais. Japo ana uwezo huo lakini akifanya hivyo atakuwa anapeleka ujumbe mbaya kwa wasaidizi wake na wananchi pia.

Bashite alifanya kosa kuamua kuingiza hayo makonteina bila ya kufanya mawasiliano kwanza ili kujia ni kitu gani kinaweza kupata msamaha wa kodi na kipi hakiwezekani.

Ni mbaya sana kwa kipngozi yeyote au mwananchi wa kawaidia kujiaminisha kuwa Rais ni rafiki yake kiasi kwamba anaweza kufanya chochote eti kwa vile tu kitu hicho kina manufaa kwa umma.

Kuna siku watu wwtakuja kujua kuwa Magufuli hana rafiki wa kudumu bali huangalia zaidi kama unaendana naye katika mipango yake au la.

Nahisi Bashite alienda mbali mno katika kumzoea Rais. Nilishangaa siku moja rafiki yangu aliponiambia kuwa amepigiwa simu na Baba mzazi wa Bashite akitaka ampe hela na kwamba yeye ana uwezo kwa kupitia mwanae kuhakikisha biashara za rafiki yangu zinaenda vizuri. Nilimwambia rafiki yangu kuwa ampuuze, jambo la muhimu ahakikishe anaendana na sheria. Ni aheri kutengeneza faida ndogo ndani ya sheria kuliko kutajirika nje ya sheria.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
#MwananchiNukuu Wengine hugawa watu katika mafungu. Mtu fulani akifanya kosa hata liwe kubwa, hasemwi lakini mwingine akifanya kosa japo dogo hukuzwa likawa kama Mlima Kilimanjaro" Hayati Baba wa Taifa, Julius Kambarage Nyerere #MwananchiLeo


Sasa huyu bashite kafanya bonge la kosa lakini baba yake anamlinda tu hapo ndo utajua jiwe alivyombaguzi.
Heshima yako boss!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwisho wa siku Philipo will be the loser. Subirini mtaona. Keep watching.. If you do not know how does double standards work, keep watching.
 
#MwananchiNukuu Wengine hugawa watu katika mafungu. Mtu fulani akifanya kosa hata liwe kubwa, hasemwi lakini mwingine akifanya kosa japo dogo hukuzwa likawa kama Mlima Kilimanjaro" Hayati Baba wa Taifa, Julius Kambarage Nyerere #MwananchiLeo


Sasa huyu bashite kafanya bonge la kosa lakini baba yake anamlinda tu hapo ndo utajua jiwe alivyombaguzi.
Inasemekana dab hawaivi na mzazi wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na Benny Mwaipaja, WFM - Dar es Salaam

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika eneo la kuhifadhia makontena-Bandari Kavu Dar es Salaam (DICD), na kukagua makontena 20 yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea na mnada wa makontena hayo ili kupata kodi ya Serikali inayokadiriwa kufikia shilingi bilioni 1.2.

Dkt. Mpango amesema kuwa kodi hiyo inadaiwa kwa mujibu wa sheria za nchi baada ya mwenye mali kushindwa kulipa kodi na kwamba amesikitishwa na vitisho vinavyotolewa na Mkuu huyo wa Mkoa na vilivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini akitumia vifungu vya Biblia kwamba yeyote atakaye nunua mzigo huo atalaaniwa.

"Sheria za nchi hazichagua sura wala cheo cha mtu, na mimi ndicho nilicho apa, kutekeleza sheria za nchi, sheria za kodi, ndiyo dhamana niliyo pewa kwahiyo Kamishna, simamia sheria za kodi bila kuyumba" alisisitiza Dkt. Mpango akitoa maelekezo kwa Kamisha wa Forodha Bw. Ben Usaje.

Alifafanua kuwa mzigo wa Samani ulioagizwa kutoka nje ya nchi hauna msamaha wa kodi na kwamba huyo aliye agiza (RC Paul Makonda) alipe kodi stahidi na asipo lipa kodi hiyo mchakato unaoendelea wa kuyapiga mnada makontena hayo uendelee.

"Napenda niwaombe viongozi wenzangu Serikalini, ni muhimu tukachuja maneno! Unasema mtu anayekuja kununua samani atapata laana, tena laana ya Mungu, kwanini tunamhusisha Mungu kwenye vitu vya namna hii" alieleza kwa masikitiko Dkt. Mpango

Dkt. Mpango alitoa wito kwa watanzania wanaotaka kununua bidhaa hizo ambazo nyingi ni vifaa vinavyoweza kutumika shuleni ama maofisini kama vile viti meza na makabati, kujitokeza bila hofu kununua mali hizo.

Aliwaomba walimu na wanafunzi wasiwe na wasiwasi na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua na kuwekeza kwenye elimu kwa kutenga zaidi ya shilingi bilioni 20 kila mwezi kulipa ada ya wanafunzi ili wasome bila kulipa ada na ina mpango madhubuti wa kuboresha miundombinu ya elimu nchi nzima ikiwemo ujenzi wa madarasa na ofisi za walimu.

"Tunawapenda na kuwathamini sana walimu wetu, asitokee mtu yeyote akaanza kuwaambia hadithi kama vile Serikali hii inawapuuza! Si kweli hata kidogo" Aliongeza Dkt. Mpango

Kwa upande wake, Kamishna wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Ben Usaje, alimweleza Dkt. Philip Mpango kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda, aliwasilisha maombi ya kutaka kupewa msamaha wa kodi wa makontena 36 yenye samani kutoka Diaspora nchini Marekani.

Alisema kuwa kati ya makontena hayo, yaliyoingia nchini ni makontena 20 ambayo yanadaiwa kodi ya shilingi bilioni 1.2 na kwamba utaratibu kwa kumtaka Paul Makonda alipe kodi hiyo ili aruhusiwe kuyachukua makontena hayo ulifanyika kwa mujibu wa sheria na kwamba mpaka sasa hajayachukua ndio maana yanapigwa mnada.

Naye aliwatahadharisha watu wanao tumia masuala ya siasa na uongozi Serikalini kutaka kukwepa kulipa kodi a kwamba suala la kodi za samani zinaonekana ziko juu kwa sababu Bunge lilitunga sheria hiyo ili kulinda soko la ndani la samani na kuweka sheria ya kutokuwepo kwa msamaha wowote wa kodi kwenye bidhaa kama hizo.
Karibuni tutajua nani ni kipenzi Baba
 
Hii series hii inaonyesha magu kashamchoka Bashite na ndio maana wateuliwa wa magu hawatishiki kwa sasa, na napata uhakika sasa kuwa ni kweli Bashite akili zake hazipo sawasawa maana mara ya kwanza aliyakana hayo makontena kuwa sio yake akaja tena akisema kuwa ni yake na anaomba msamaha wa kodi na sasa anawalaani wanaoyapiga mnada wakati ni yeye mwenyewe mwazo aliyakana kuwa sio yake

Alafu ukimkuta kule insta anavyopost mambo ya kilokole huwezi mshtukia kuwa ni shetani mkubwa huyu

Sent using Jamii Forums mobile app
Dab kapoteza credibility kwa mzazi wake...ndio maana husikii zile mbwembwe zake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom