DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

MAkonda alifanikiwa kuingilia sana wizara ya mambo ya ndani kupitia uenyekiti wa kamati ya ulinzi alivuka mipaka na kuingilia kazi za mwigulu!

Leo kaingia cha Kik! Kakutana na Mpango kakaziwa; ajue tu pale wizarani yupo mtoto mpendwa kuliko yeye (doto):
Msikie mpango akimpa za uso hapa!

Siku zimekaribia za gavana kuondoka habebeki!

Makonda fahamu kuwa Dr. mpango siyo mwigulu au ummy mwalimu ambao ulikuwa unawaingilia majukumu yao! Nasubili laana

Kwa kauli ya RC Makonda ilipaswa afukuzwe,ameifitinisha serikali.Tukizingatie sheria sote nchi itaenda vizuri.
 
Acha utoto wewe
Huyo mpango kaacha ofisi dodoma kaenda bandarini kushindilia container za Makonda tu?Basi hata kutumia ziara hiyo kuamuru na mizigo mingine yote inadiwe,lakini kwa kua anaongozwa kwa chuki mizigo mingine kwake si lolote hata ikikaa miaka 10
pole sana daudi bashite
 
Hilo limeshafanyika kazi ipo kwa mpango
Mpango anaamani kwa dhati kabisa ya moyo wake kuwa samani hizo kuukuu ni za Makonda,hivyo basi azilipie ushuru.
Mpango kwa chuki yake kaenda kuyashindilia yauzwe,badala ya kuyataifisha basi yapelekwe shule za serikali nchi nzima
Tueipende kuandika vitu tusivyokuwa na uhakika! Kila mtu anjua Mizigo ya nani!
 
Kunajambo limefichika ndani ya huo msaada wajuzi wanajua.
 
Acha utoto wewe
Huyo mpango kaacha ofisi dodoma kaenda bandarini kushindilia container za Makonda tu?Basi hata kutumia ziara hiyo kuamuru na mizigo mingine yote inadiwe,lakini kwa kua anaongozwa kwa chuki mizigo mingine kwake si lolote hata ikikaa miaka 10
Hata tusingejua kama si makonda kutangaza anapigiwa mnada, unafikiri kila mnada wa makontena wanakutangazia kama ya makonda?
Hata mahakamani tunajua kesi za watu maarufu tu zinaendaje lakin za chokambaya hatujui lolote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kontena 36 za samani zitolewe hivihivi kama msaada?tena na diaspora aliyeko marekani?jamani tuache masihara.hapo kontena za msaada ni moja au mbili tu nyingine zote zingepelekwa showrooms tu.wangechukuliwa baadhi wa walimu na waandishi wa habari wapigwe picha wakigaiwa baadhi ya viti na meza mchezo uishe.sasa wanalazimisha mzigo utoke bila kulipa kodi kinyume na sheria kwa kisingizio cha msaada kwenye mashule.wanataka kuichakachua serekali mchana kweupeee
 
Hizo samani ni za nani au zinalengwa kupelekwa wapi?Msaada au?(Kuuliza si ujinga)
 
Ulitaka aagize tu anavyotaka kisa ni vifaa vya kugawa mashuleni?
Kama ni vifaa vya kugawa kwenye mashule kwanini aandike majina yake?
Alafu watu wanaongea vitu wasivyovijua ukiagiza mzigo au ukituma mzigo kwenda nje ya nchi kuna namba agency wako atajaza kuwa huu ni mzigo Wa aina gani na CPC ipi mfano kama ni mradi Wa serikali mfano kampani ya bam inayojenga jengo pale airport hawezi kuleta mavyuma tu bila kujaza CPC TRA wanakadiria kodi kwa kufuata taratibu na sheria zilizowekwa na serikali kuna hsc code za bidhaa zote sasa makonda ameagiza kwa CPC gani kwenye mzigo wake ili TRA waupitishe kama ni msaada Wa shule na je vinamsamaha Wa kodi?kwa sheria hizi na kama umeshaingizwa kwenye systems ya tancis ningumu KWA ushauri wangu kwakuwa yeye ni MTU mkubwa aombe wahisani wamchangie alipe kodi kama utaratibu ulivyo KWA maana kila siku storage inaongezeka na siku nyingine kabla hajaagiza aonane na wahusika wampe maelekezo kabla
 
Hivi hata viti, meza na kabati tunaagiza toka nje wakati humu Nchni kuna samani nzuri na imara zinatengenezwa na vijana wetu mitaani, Hao diaspora wangekupa Fedha ungenunua hapa nchini kuliko kununua mabox toka ng'ambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwandishi yuko sawa Tanzania ni ngumu hata kuisaidia. Kwa wanaokaa TZ wengi hawawezi kuamini haya lakini sisi wa nje tunajua ndugu zetu. Tunaenda kwenye ma hospital na mashule kuombea vifaa mfano Ali ambaye ni Mtanzania mwenye asili ya Zanz ndiye aliyetuma hivyo vifaa cha ajabu akituma nchi nyingine hakuna hizi shida! Yuko seattle na watu wanajitolea kupakia kwenye makontena, watu wanachangia gharama za kutuma na storage halafu zikifika TZ eti tulipe kodi wakati vifaa ni vya watoto wanaokaa chini ndiyo wameomba. Sasa hiyo kodi ni ya nani kama haitasaidia watoto wanaokaa chini! Tulifikiri kodi ni kusaidia Watanzania.... Halafu watu hao hao wanasema sisi watu
Wa nje hatuna faida maana hatusaidii. Mna mkomoa nani Makonda yupo kwenye jumba la serikali, sisi tuko huku US anayepata shida ni yule mtoto. Sasa wazuri wakitucheka tutasema nini mlitaka watu wasaidiaje kutoa pesa tu ambazo zitaishia kwa wajanja..!

Mimi nilijuwa mkiwa nje mnakuwa na akili lakini kumbe hovyo tu, ukiwa unachangia lazima ujue unachangia kwenye Taasisi gani . Unamchangia Bashite then unakuja kusema vifaa vya watoto mashuleni. TRA kazia humo humo
 
Nimeeleza hapojuukwamba sina tatizo na Waziri kutimiza wajibu wakekwa kufuata sheria.

Magufuli alimpongeza trafiki aliyemzodoa mke wa Balozi Dr. Waziri Mahiga, kwa minajili ya kwamba serikalihii haijali wewe mkubwa, mke wa mkubwa wala nani, hapa kazi tu. That was debatable given the proctacted circumstances,na yule mama alijaribu kujirudi na ku contain ile situation lakini ikawa too late.

Kwa hiyo, kama suala ni "hapa kazi tu" na Waziri anafanya kazi yake, nimeshasema hapo juu Makonda kakosea.

Ila mimi ni mtu wa kutaka uongozi wa old school decorum, Mzee Mwinyi anakwambia enzi zao wanasoma, mwanafunzi ukionekana unatembea barabarani huku unakula, mwalimu wako akakuona "unakula majiani", ukifika shule ni fimbo.

Kwa nini unakosa ustaarabu wa kukaa kitako ukiwa unakula?

Labda hii old schooldecorum iko out of touch na reality, lakini sisi tuliokua enzi za serikali ya Mwalimu Nyerere, tunakumbuka enzi ambayo serikali ya Tanzania viongozi walifanya kazi kwa nidhamu ya hali ya juu, angalau machonipetu.

Kama walikuwa na beef zao, tunakuja kuzisikia wakati washatangulia mbeleya haki,kutoka kwa insiders huko.

Enzi hizo huwezi kusikia Mkuu wa Mkoa anabishana na Waziri kwenye vyombo vya habari,regardless ya nani kakosea na nani kapatia, viongozi wa serikali moja kukozana kupitia vyombo vya habari ni utovu wa nidhamu.

Serikali inaendeshwa kwa imani.

Mizozo ya viongozi wa serikali moja kati yao, ina ondoa imani ya wananchi kwenye serikali kiujumla bila kujali nani kakosea na nani kapatia.

Jay-Z aliimba katika "Takeover"

"A wise man once told me, don't argue with a fool. Cause people from a distance, can't tell who is who".

Mpango angepiga mnada tu hayo makontena bila kuzozana, tuone hiyo laana ingeanzia wapi.
Hicho kisa cha kula barabarani umenikumbusha mbali.

Nikiwa shule ya bweni kidato cha tano mwalimu wangu mmoja alitukuta njiani tunakula 'pears' alitusimamisha kwa hasira karibu atupe adhabu.

BTW, Nakubaliana na busara uliyo shauri kuhusu mgogoro wa Makonda na Waziri. Kama ulivyosema ilikuwa njia mbaya iliyotumiwa na waziri.

Nadhani ilichochewa na historia ya Makonda kuhusishwa na minong'ono ya kuwa anaogopwa na mawaziri na analindwa na mamlaka zilizo mteua na kwamba yeye huamua chochote bila hofu ya kutumbuliwa.
Sasa wahusika wakaona kuzima kelele haraka bora waziri awahi kumkosoa.

Tukio lilisha trend kwenye vyombo vya habari tayari. Hii ndio athari ya siasa zetu za kibongo zinaamua mambo mangi ndivyo sivyo kuogopa wanasiasa au kuwapatia umaarufu wanasiasa usio wa faida kwa taifa.
 
Haiwezekani mtu mmoja atumie mgongo wa madaraka kukwepa kulipa Kodi kisa ukuu wa Nkoaaa tuone sasa Jiwee atamtetea kwa hilii...
IMG_20180828_071220_484.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanasema kuna maajabu ya dunia yanayopatikana katika nchi mbali mbali, ila Tanzania yenyewe ni ajabu miongoni Mwa maajabu,

Watu wanajitolea kukusanya vifaa kuwasaidia watanzania walioko katika shule zisizo na vifaa Alafu inafika bandarini eti viuzwe,??

Kama wanajali sana hela basi vinunuliwe na wizara ya elimu,

Tanzania ilivyonikatisha Tamaa mimi kuhusu michango ya kujitolea kuokoa majanga nadhani hata wengine wamekata tamaa,

Kuna rafiki yangu mtoto wa mtu mkubwa wa zamani anakaa Norwich nilipomtembelea juma lilee akanambia kuna vifaa vya hospital tuvikusanye tutume visaidie hospital za Tanzania, nisiwe mnafiki nilimjibu Tokea serikali imeleta zuruzunga kwenye Hela ya Tetemeko niliyochangia USD 400 nikidhani zitamfikia yule mama ambaye alitumika kukusanya Hela Mara matembezi masaki Mara changia bukoba, kumbe picha yake inatumika tu, sitakuja kuchangia Janga lolote Tanzania, acha wenye za kuchezea wachange,

Sasa Leo huyo jamaa yangu baada ya kusikia makontena ya makonda ya msaada yamezuiliwa ili yauzwe kanipigia moja kwa moja kwamba ulisema kweli, nami sivikusanyi

Mnakatisha wanaojitolea tamaa,
Ni bora ukatumia hela yako kuinua familia yako kuliko kuchangia Majanga ambayo serikali haithamini mchango wako,

Britanica

Jiongeze badala ya kukurupuka kuandika thread. Makontena yalikuwa 36 kwa jina binafsi. Yote yaliombewa kufutiwa kodi. Iliposhindikana, akayalipia makontena 16 kwa fedha binafsi. Mpaka Leo hayajulikani yapo wapi. Yaliyobaki, 20, ndiyo tunapigiana kelele zisizo na msingi humu ndani. Achana na jambazi huyu. Kama mlichangia mliingizwa choo cha kike. Mlipaswa mjiulize kwanini michango yenu inasafirishwa kwa jina binafsi. Na kwanini kwanza aliyakataa hayajui?!?! Mlitumika kama mradi binafsi bila hata Wizara ya Elimu kujua au mamlaka za mkoa kutaarifiwa. Sasa kaeni kimya mkijutia uzumbukuku mlioufanya kwa kuzidiwa akili na Form Four Failure.
 
Tumesikia hivi karibuni sakata la makontena ya Mh Makonda.

Sakata lilianza mnamo Februari mwaka huu kwa kuyapokea makontena hayo mbele ya vyombo vya habari kule bandarini.

Lilipokuja swala la kodi mnamo mwezi wa nne au tano hivi, Makonda aliyakana MBELE YA VYOMBO VYA HABARI kuwa na yeye nado kwanza anayasikia!

Tukumbuke mapema, Mkuu wa nchi alimhimiza apige kazi kwenda mbele!

TRA wakakomaa na mnada, makontena bei ikawa juu ya viwango, hivyo hayakununulika.
Jumapili hii Makonda kaenda Kanisani( na siyo TRA) kuyaombea laana kwa atakayeyanunua!
~Mbele ya vyombo vya habari!

Hapa nikachoka!
Uongo ukawa dhahiri, makontena sasa ni yake na Makonda alitaka kukwepa kodi.

Na sasa anatumia ushirikina(sijui kanisa linalotoa laana kwa utendaji wa Serikali).

Haya ndo matokeo ya kuweka mtu kwenye madaraka makubwa huku kichwani ni patupu.
 
Huyu kiumbe alitakiwa awe makini sana ili kuprove wrong kuwa si kweli kuwa ana vyeti vya kufoji na hatumii jina lake

Lakini kila siku zinavyosonga anaonyesha ni kweli kichwani hamna kitu alafu alitakiwa awe mtulivu sana pia alitakiwa kusoma alama za nyakati mapema wakati anajua kabisa anaishi kwa kubebwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mi naamini kama sheria za kodi haziruhusu kutoa izo mali bila kodi pia sheria izo izo zimemruhusu raisi kutoa msamaha wa kodi kwa bidhaa yoyote ile so kwanini haoni sakata hili

Sent using Jamii Forums mobile app
Pengine wakubwa wamehisi hizo samani sio zote zinaenda kusaidia kwenye elimu.

Inaweza kuwa wafanyabiashara flani wanapitisha vitu kwa mgongo wa makonda.

Kwanini havikuletwa kwa jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam badala ya jina binafsi?
 
Back
Top Bottom