DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Britanicca hivi unalia ama unacheka...ebu fafanua.!!
Nani kakwambia hiyo ya Makonda ni michango ya diaspora? Mtu kaingiza consignment ya samani kifisadi chini ya uratibu wa wafanyabiashra mafisadi nyie mnasingizia diaspora chini ya mwavuli wa elimu? Rais Magufuli shikilia hapohapo tuone mwisho wa hii kitu!
 
Mshua kaongea principle, ila mimi nasikitika sana hawajaweza kuongea na kuyamaliza kabla.

Bashite amesababisha aibu kubwa sana kwa serikali.
 
Inaonyesha kiswahili kina blabla nyingi, embu cheki apo "For the English Audience" ilivyofupi na kueleweka!
 
Mkuu wa jiji alikurupuka bila kumshirikisha Mwenye nchi yake...anaonekana kuizoea ikulu hivyo anajiamulia tuu.
 
Sheria si mnatunga wenyewe na kuzipitisha kwa kusema ndioooo!!Sasa hapo unashangaa nini?!

Alafu jiulize ni kwanini mwanzoni aliakana alafu baadae akayakubali?

We jua tu hilo ni dili limebumbuluka.
Hao watu ni wapumbavu sana ..
Wanatunga sheria za kukomoa zikiwabana wanatoa povu jinga sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukisikia utawala uliofitinika ndo huu, visasi na chuki nje nje. Yaani walimtumia mama wa watu kuuza sura kumbe wanaitafuta pesa waile, zile pesa kama kuna watu kulaanika lazima watalaanika tu
 
Dk Mpango angeonesha njia kwa kununua angalau kontena moja kuthibitisha kwamba yeye haogopi vitisho vya kulaaniwa yeye na uzao wake.
Mwisho wa siku hizo fanicha zitaozea hapo bandarini wakose wote!
Yaani anunue tu hata kama hana mpango wa kuzitumia!!, yaani afanye mambo ya kisiasa kwa nia ya kumkomoa dogo RC wa Dar!!.

Katimiza wajibu wake kama waziri, wenye kuhitaji kilichomo kwenye makontena ndio watakaonunua.
 
Mimi ni mfuasi wa magufuli na CCM lakini simuungi mkono Makonda hata kidogo. Mheshimiwa rais kama ulivyowajibisha Nape, Mwigulu na wengine wengi wajibisha makonda pia.
 
Mtoa hoja jiangalie....mbaka wanataka yapigwe mnada sio wajinga wamesha fanya uchunguzi wamegundua janjajanja hiyo kumbuka ndani yake kuna siasa,bila shaka wala kumung'unya maneno hayo makonten yalipwe ushu tena ushuru stahihiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, hii nchi kila mtu wa nje akikusanya vifaa na kuviweka kwenye kontena vije, bandarini visitozwe KODI, itakuwa ni upumbavu sana. ELIMU YA KUBANGAIZA alikana, ghafla akayatambua, leo anaambiwa KODI anaanza kulialia kanisani! The bushman (kolomije) anapambana kutafuta sifa binafsi kwa njia illegal. Hatuwezi kuwa na Taifa la namna hii, sheria ya KODI isimamiwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuwa na nia njema kama usemavyo,kwa nini aandike jina lake binafsi kama vifaa ni vya msaada katika taasisi husika,viuzwe tu next time aagize kupitia jina la taasisi husika
 
Yaani umemaliza kabisa mkuu! Elimu ikiwa kwa kiwango kidogo kuliko hitaji husika haya ndo matatizo yake; nimejifunza kuwa siku zote elimu ya kutosha inakufanya ujue kuwa kuna mengi mno ya kujua na hivyo kukufanya uwe mnyenyekevu na makini katika kuweka akiba, ikiwemo ya maneno.

Kwa bahati mvaya sana DAB, akuzingatia mashauri ya Sulemani katika Mithali 4:13 na kama kubadilisha jina kumeshindwa kumhekimisha hakuna kanisa litakalomsaidia kufikia malengo yake kwa mbinu dhalimu.

Kilichokaki ni kurudi na kubembeleza mamlaka ya uteuzi; labda kuna maajabu yatakayowezekana.

Pole nyingi kwa DAB lakini uzuri ni kwamba anaendelea kujifunza, japo kwa njia ngumu kuwa mara nyingine mbeleko inaweza kuwa ngumu sana kupatikana!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu huyu mkuu wetu wa mkoa si tu hana hekima, bali anataka kufungua uchochoro wa ukwepaji kodi.
Wakuu wa mikoa wote wakiagiza "vifaa kwa ajili ya mikoa yao", unaweza kupima ukwepaji kodi utakaofuata.

Naenda mbali zaidi, Makonda katumiwa tu, hizo samani kwenye makontena nahisi zina wenyewe.
 
Mara pap!! BREAKING NEEWZ!!!!,badiliko la baraza la mawaziri,mpango nje!!!!
Ofsini kwetu mabango ya baraza la mawaziri tulishayachana maana kila tukinunua hili,kesho linakuja jipya!!!

Wekeni soft copy wazee
 
Back
Top Bottom