Dar: Maandamano ya ACT Wazalendo kuelekea Ikulu kushinikiza waliotajwa wizi kwenye ripoti ya CAG kuchukuliwa hatua

Dar: Maandamano ya ACT Wazalendo kuelekea Ikulu kushinikiza waliotajwa wizi kwenye ripoti ya CAG kuchukuliwa hatua

ACT kinapambana sana kuwa chama kikuu cha upinzani. Wakiendelea hivi chini ya miaka mitatu ijayo watakuwa wameshaipiku CHADEMA hasa hii ya sasa.

Maandamano yana nia nzuri sana sema mwamko wa Watanzania ndiyo zero....

View attachment 2591675
Maandamano makubwa yameanza eneo la Fire Kariakoo yakiwa yameandaliwa na ACT-Wazalendo kushinikiza wezi wote walionaswa na Ripoti ya CAG waondolke maofisini kwenda magerezani.

Maandamano yanaongozwa na viongozi waandamizi wa chama hicho Cha upinzani na yataishia lango Kuu la Ikulu ya Magogoni ili yapokelewe na Rais Samia Suluhu Hassan.

Binafsi Niko mbele na bango langu. Hali ya hewa si rafiki sana hata kuandika ni taabu lakini umma unazidi kujitokeza kuwataja wezi wakamatwe. Karibuni.
Hakuna maandamano hapo. Ni ujinga ujinga tu ushaona wapi Raisi apokee maandamano ya upinzani tena ikulu.

Samia anatakiwa kufukuza wizi hahitaji kushinikizwa
 
ACT kinapambana sana kuwa chama kikuu cha upinzani. Wakiendelea hivi chini ya miaka mitatu ijayo watakuwa wameshaipiku CHADEMA hasa hii ya sasa.

Maandamano yana nia nzuri sana sema mwamko wa Watanzania ndiyo zero....

View attachment 2591675
Labda wataipiku Chadema ya mwandiga na ujiji huko.
 
Kupitia thread hii ndipo utajifunza udhaifu wa wanasiasa wa upinzani Tanzania.
ACT wataanza kushambuliwa na wafuasi na shabiki wa vyama vingine vya upinzani kuhusu haya maandamano kuliko watakavyo shambuliwa na wafuasi wa chama tawala (CCM).

Hiyo yote ni kuwakatisha tamaa wasifanikiwe kupata umaarufu kuliko wao. Kwao bora CCM iendelee kukaa madarakani na kuvurunda vitu kuliko wenzao wawe juu yao kisiasa.

Kwa mshangao kesi kama hii hadi watu maarufu na wajuaji wakubwa wa JF utawakuta wanashangilia kukwamishana wapinzani.

Ufuasi wa vyama kwa misingi ya ukabila, udini na ukanda husababisha tatizo hili.
 
Maandamano makubwa yameanza eneo la Fire Kariakoo yakiwa yameandaliwa na ACT-Wazalendo kushinikiza wezi wote walionaswa na Ripoti ya CAG waondolke maofisini kwenda magerezani.

Maandamano yanaongozwa na viongozi waandamizi wa chama hicho Cha upinzani na yataishia lango Kuu la Ikulu ya Magogoni ili yapokelewe na Rais Samia Suluhu Hassan.

Binafsi Niko mbele na bango langu. Hali ya hewa si rafiki sana hata kuandika ni taabu lakini umma unazidi kujitokeza kuwataja wezi wakamatwe. Karibuni.
Niko nyuma yako na pajama ya kijivu hapa. 🤣 🤣 🤣 Tusonge mbele mpaka ilipo pochi ya mama
 
Back
Top Bottom