Dar: Maji ya Bahari yafanyiwe Desalination tuyanywe

Dar: Maji ya Bahari yafanyiwe Desalination tuyanywe

Kujenga reli Dar-Mwanza ni ghali zaidi kuliko kutoa maji ziwa Victoria to Dar.

Maji ya ziwa Victoria yako Tabora tayari na hayakati hovyo kama hayo ya mtoni.
 
Desalination ni kweli inahitaji uwekezaji mkubwa wa awali kwa kuwa serikali inatakiwa itoe huduma kwa wananchi wake inatakiwa itafute pesa kama inavyofanya kwa miradi mingine mikubwa na iwekeze kwenye huduma hiyo na isitegemee kupata faida kubwa au kukusanya mapato kwa muda mfupi ili wananchi waweze kupata huduma ya maji kwa uhakikika na hivyo kuchochea shughuli zingine za uwekezaji na huku ndiko ikusanye kodi
Nashindwa kuelewa mtu anaogopa gharama..serikali imekua ikijenga vioo sehem mbalimbali, na huduma hii ilitakiwa kuwa bure ila inafanya biashara na inakusanya mapato permanently, maji dawasco wanawauzia wananchi dumu la litre 1000 ni kama 1700 au elfu 2000. Hapa inakusanya mabilioni ya pesa. Kwanini uogope uwekezaji wa gharama ambao unajua utarudisha mtaji? Labda mniambie nchi hii haina viongozi wenye maono ya mbali. Sehem nyingi raslimali zipo. Makaa ya mawe yanaweza zalisha umeme continuously bila kuongelea maji na ni rafiki wa mazingira. But kila leo migao migao ya umeme . Sisi miafrica na miviongozi yetu Akili fwa fwa fwaa kabsaa.!!
 
Kwa umeme upi? Huu wa Makamba ambao unakatika bila taarifa!
Pale Usokami, Mkoani Iringa kuna mradi wa Umeme wa Upepco (Wind energy) wa 2.4 MW. Je, haiwezekani baharini ukajengwa mradi wa umme wa upepo wakuendesha mitambo ya maji tu?
 
Nikweli hii high-tech ipo Saudi Arabia na baadhi ya mataifa ya kiarabu lkn kwetu ni ndoto mkuu, inasemekana ni moja kati ya technology ghali sana duniani... hatuwezi lipa kwa bili zetu hizi, haswa ukichukulia zaidi ya 60++% ya wakaazi wa DSM ni "WAKORA" wa maji....
Viwanda na hoteli zinadumu garama. Lita za maji 37,000 gharama ya kuzalisha ni dola 2 hadi 5.
 
Kwa kweli mku kama unayo hiyo technologia, tusaidie basi uende kwa mku wa mkoa anafikika kirahisi, alafu akupe mtu wake muongozane kwenda DAWASCO shida iishe . Wape hiyo idea then tutafurahi ukirudisha majibu humu JF tukupongeze.

Ukienda wewe kama wewe DAWASCO hawawezi kusikiliza hata huwezi kumuona mkrugenzi wao.
Hamna haja ya kwenda. Waziri wa maji Jumaa Aweso akitaka andiko tunampa anaenda kulifanyia kazi. Mgao wa maji bye bye Dar. Hoteli na Viwanda vyote vifingiwe maji ya bahari.. Hawa wananchi waachiwe maji ya Ruvu. UN-Water wana hela zimekaa hazina kazi. Rais Samia akakope aokoe wananchi wake. Tutalipa taratibu.
 
Ruv
Ingekua ni rahisi wangegharamika kutandika mabomba toka Ruvu hadi DSM kwa gharama kubwa?
Ruvu Mabomba yapo. Hakuna mradi wa mabomba ya maji kutoka Ruvu ambao umekwama. Wizara ya maji haipewi hela ya kutosha. Ndo Wizara pekee inategemea huruma ya Mungu ili mambo yaende
 
Kukunyima maji ni njia moja yapo ya kukutawala. Wakileta maji kesho utasahau kama una siku tatu hujalala na maji. .

Kuna mijitu unakuta hata umeme ukirudi anamshukuru Allah, Bure kabisa. Kwanza kutaja jina la Allah Bure dhambi😡😡
 
Kujenga reli Dar-Mwanza ni ghali zaidi kuliko kutoa maji ziwa Victoria to Dar.

Maji ya ziwa Victoria yako Tabora tayari na hayakati hovyo kama hayo ya mtoni.
Serikali inaweza. Sema hawana utashi. Hela ya Tozo ya miezi mitatu inanunua Mitambo ya kutengeneza maji ya bahari
 
Nashindwa kuelewa mtu anaogopa gharama..serikali imekua ikijenga vioo sehem mbalimbali, na huduma hii ilitakiwa kuwa bure ila inafanya biashara na inakusanya mapato permanently, maji dawasco wanawauzia wananchi dumu la litre 1000 ni kama 1700 au elfu 2000. Hapa inakusanya mabilioni ya pesa. Kwanini uogope uwekezaji wa gharama ambao unajua utarudisha mtaji? Labda mniambie nchi hii haina viongozi wenye maono ya mbali. Sehem nyingi raslimali zipo. Makaa ya mawe yanaweza zalisha umeme continuously bila kuongelea maji na ni rafiki wa mazingira. But kila leo migao migao ya umeme . Sisi miafrica na miviongozi yetu Akili fwa fwa fwaa kabsaa.!!
Nahisi viongozi wanagombania kupata vyeo ili wapate ulaji si kusaidia wananchi. Mradi wa maji si gharama kabisa. Sema hawaoni umuhimu wa maji sababu wao wanajaziwa maji kwenye matenki yao na Serikali
 
Mkuu bado hatujafikia huko tuna vyanzo vingi vya maji tamu/baridi
Dar hakuna vyanzo vya maji. Mbona maji ya Victoria yanatumika unaambiwa yanakaribia Dodoma? Kuna tofauti gani na bahari? Kikibwa tupate rais anaye thubutu. Huko Mkuranga na Nangurukuru wqtatumia maji ya bomba sio visima. Tena ndani ya miezi sita. Nchi yetu haina Vita, hela iliyo jeshini, irudishwe hazina ifanye kazi za maendeleo. Natamani CAG akague jeshi watu mshangae hela inavyotumika
 
Kuna mgeni alikuwepo leo radio one sijui ni Boss kutoka Wizara ya maji,naye anasema kutumia maji ya bahari ni ghali lakini hasemi ni ghali ukilinganisha na nini? Na ni ghali kiasi gani? Tunaambiwa tu ghali.
Hata daraja la kwenda Busisi walikuwa wanasema ghari. Dar haina miundombinu ya maji halafu mtu fulani na kichwa chake anajenga daraja la Coco Beach 🤣
 
desalination inafaa zaidi sehemu siyo na chanzo/ vyanzo vya maji ya baridi. Ila kwa Tanzania tunavyanzo vingi tu vya kutosha vya maji baridi.
Kuna maji mengi tu ya mvua upotea ovyo. Hayo maji ya mvua yanayopotea ovyo yanatakiwa yavunwe kwa matumizi ya baadaye. Wizara inapaswa kujenga hayo mabwawa (Earth dams) ambayo yatakuwa ni cheap kuliko desalination process kwenye miji ya pwani (Dar, Tanga, Pwani, Lindi na Mtwara).
Kwa mtizamo wangu naona kuna tatizo mahali kwani kuna sehemu japo kuna wingi wa maji baridi (kanda ya ziwa), wakazi wake walio wengi wanashida ya maji safi na salama.
 
Desalination ni process aghali sana duniani.
Mkuu mimi nimeitumia hizo RO tukiita fresh water maker,au desalination plants,kwa zaidi ya miaka 15 huko offshore bahari ya Pacific.Tukitengeneza kati ya tani 150 hadi 200 kwa siku.
Kwanza hiyo initial cost ni aghali mno.
Operating cost na maintenance cost ni kubwa mno,kubadirisha filters weekly.
Hayo maji ni pure water hayana ingredients, hivyo kuyatumia yalivyo yana upungufu wa madini unless huongeze hizo ingredients.
Inatumia umeme mwingi mno kwa sababu ya pumps zake kusukuma maji chumvi kupitisha fresh water kwenye vipenyo vidogo mno vya membrane ni big issue.
Kitu kilicho ghali ni hizo membranes,zinataka usimamizi na matumizi sahii sana.Bei za membrane spare part ni zaidi ya nusu bei ya mtambo mpya.
Kibaya ni coastal waters si salama kwa kupata maji safi sababu ya pollution tokea viwandani na vinyesi vya binadamu , ina maana itabidi kusukuma maji kuyahifadhi kwanza kwenye setting tanks inaongeza initial cost na maintenance cost.
Lakini kama tukichimba visima hivi vyetu tukapata maji yenye chumvi kidogo inaweza kutumia RO kuzalisha maji safi kwa gharama pungufu zaidi kuliko maji ya bahari.
 
Back
Top Bottom