Dar: Mashehe washauri wanaomkashfu mitandaoni ‘Nabii Mkuu’, Dkt. Geor Davie wa Gurumo ya Upako, kumfata Arusha kwa nauli yao

Dar: Mashehe washauri wanaomkashfu mitandaoni ‘Nabii Mkuu’, Dkt. Geor Davie wa Gurumo ya Upako, kumfata Arusha kwa nauli yao

Huyu nabii katumwa na aliyekutana naye physical, hao mashehe ni uthibitisho wa nabii kutokewa na aliyemtuma so kazi inasonga mbele

Alijuaje ni Yesu? Ni vizuri kutofautisha sauti ya Mungu na ya Shetani
 
Mamia ya masheikh wamelaani watu wote wanamkashfu Nabii Mkuu Mheshimiwa Dr. Geor Davie wa Ngurumo ya Upako. Mashehe hao wanasema Nabii mkuu ni nabii wa kweli, nabii anaewapenda watu wote na anaewajali watu wote...
Ndugu naomba unisaidie! Nimecheka kweli.
 
Hayo mawazo yako tu..bongo hakuna waislamu wa kweli wengi ni wanafiki..waislamu wa kweli na wanaofuata mafundisho ya kiislamu ni magaidi wale isis..bokoharam..alshababu..alkaida n.k

#MaendeleoHayanaChama
Kwani ukitaka kuwa muisilamu wa kweli unakuwaje?
 
Mamia ya masheikh wamelaani watu wote wanamkashfu Nabii Mkuu Mheshimiwa Dr. Geor Davie wa Ngurumo ya Upako. Mashehe hao wanasema Nabii mkuu ni nabii wa kweli, nabii anaewapenda watu wote na anaewajali watu wote.

Mashehe hao wameitaja JamiiForums kuwa watu wanamtungia uzushi Nabii kwa kumuandika mambo ya uongo wakati Nabii mkuu hana tatizo lolote.

Mashehe hao wanasema wanamsubiri kwa hamu na wanamkaribisha kwa mikono miwili Nabii mkuu kwa mkoa wa Dar es Salaam aje kutoa huduma ya uponyaji na ukombozi.

Wasikilize hapa.

Ukiona hivi ujue watu wameshalishwa ubwabwa wameshiba ndi!
 
Hii nchi imejaa wapumbavu , wazinzi na wezi Mtu akijaribu kupambana na hayo Makundi
ya wazinzi , Wezi, na wazinzi

Lazima ashughulikiwe ao mashehk ubwabwa na Kina Mwamposa wezi + wachungaji wazinzi Ni hatari tupu
 
Hao ni waislam wale wahuni wahuni wa kwenye vijiwe vya kahawa wanaojua kusema Bismillah na inshaallah, kwanza katika maongezi ya kiislam ni haram kupiga makofi siyo mwenendo wa waislam kupiga makofi katika vikao vyao.

Na kwenye uislam nabii muhamad ndo alikua nabii wa mwisho dunian hatakuja nabii mwingne yoyote isipokua nabii issa pekee ndo atarud kwaajili ya kukamilisha dalili za kiama
Nakubaliana nawe kuwa hawa ni njaa inawasumbua. Ila Yesu Kristo ndio mwisho wa unabii wote hakuna baada yake!
 
Hawa wangekuwa Irani wangekuwa washakatwa vichwa,

Pesa mwanaharamu kweli, leo kafir anaitwa nabii mkuu,

Kafir anawakusanya wazee wetu na kanzu zao kutetea mambo yake binafsi,
Kwanini mungu wenu wa hiyo dini asiwakate yeye hicho kichwa?
 
Wanaitwa mashekhe ubwabwa aka majibwa, au umbwa yaani shekhe akashadadie kafir kaafiruuna mla wake za watu, ama kweli ukistaajabu ya jibwa utaona ya makhanithi, huo ni mwendelezo wa kulewa sadaka za waumin yani anawalipa mashekhe ubwabwa wakabwatuke hadharani ili ionekane anasafishwa? kweli Dunia imevaa gunia na hela mwana haram
 
Ila pesa mwanaharamu jaman leo mashehe wanamkarbisha kafir kwao? Hapo kweli dhahabu ikiwa shamban kwako hilo shamba ni mali ya serikali ila bangi ikikutwa shamban kwako hilo shamba mali yako
 
Nakubaliana nawe kuwa hawa ni njaa inawasumbua. Ila Yesu Kristo ndio mwisho wa unabii wote hakuna baada yake!


Tumsikilize Bwana yesu mwenyewe anasema nini :

“Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamuwezi kuyastahimili hivi sasa. Lakini yeye atakapokuja, huyo roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayo yasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.” (Yohana 16:12-13).

Katika andiko hili Bwana Yesu Kristo anaeleza kwamba uwezo wa kipaji cha watu wa wakati wake ulikuwa mdogo hawangeweza kustahimili mafundisho yote ya sheria. Kwahiyo alitabiri kwamba mwingine atakuja baadaye ambaye ametajwa kama roho wa kweli.

Yeye ataleta mafundisho kamili ya sheria kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Huyu ni Mtume Muhammad s.a.w. ambaye ameitwa katika Qur'an Roho itokayo kwa Mwenyezi Mungu.

Vilevile ni yeye ambaye ameleta sheria kamili yaani Qur'an Tukufu kutoka kwa Mwenyezi Mungu baada ya Bwana Yesu Kristo.

Kwahiyo hakuna shaka kwamba Roho wa kweli aliyetajwa katika aya hii ni Mtume Muhammad s.a.w
 
Kilq mtu anapambania kombe sasa hivi,uchawa utangszwe kama ajira rasmi sasa
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
“Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamuwezi kuyastahimili hivi sasa. Lakini yeye atakapokuja, huyo roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayo yasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.” (Yohana 16:12-13).
Huyo Roho wa Kweli anayezungumziwa ha Yesu hapa tunajua ni Roho Mtakatifu na sio SWW. Na alikwisha kuja siku ile mitume waliposhukiwa na Roho Mtakatifu ndio siku ya Pentekoste kama iliyoandikwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume 2:1-47.
 
Kwa iyo kwa sasa hv hakuna tofauti ya Dini sio..?! Kwa Masheikh hakuna kafri au Haram.. Kweli hiz ni dalili dhahir za kiama....😂🤣
 
Huyo Roho wa Kweli anayezungumziwa ha Yesu hapa tunajua ni Roho Mtakatifu na sio SWW. Na alikwisha kuja siku ile mitume waliposhukiwa na Roho Mtakatifu ndio siku ya Pentekoste kama iliyoandikwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume 2:1-47.

Natulichungue hili neno lililofasiriwa Msaidizi katika Bibilia ya Kiswahili, na ambalo limeitwa "Comforter" yaani Mliwazi katika Biblia ya Kiingereza ya zamani ya King James, na likaitwa "Counsellor", yaani Mshauri katika Biblia ya Kiingereza ya Revised Standard Version, na likaitwa "Helper" yaani Msaidizi katika Biblia za Kiingereza mpya mpya kama New World Translation na Good News Bible, na "Mu'azzi", yaani Mliwazi katika Biblia ya Kiarabu ya Darul Kitabul Muqaddas ya Cairo

Maneno aliyoyasema Yesu tunayapata kwa tafsiri tu, kwani Yesu hakusema kwa Kigiriki wala Kilatini, bali alisema kwa lugha ya kawaida ya Palastina wakati ule ilikuwa ni Kiaramiya na lugha yao ya dini ni Kiebrania.

Zote mbili hizo zina asili moja na Kiarabu.

Injili ya Yohana ndio hiyo iliyotaja hiyo bishara ya Yesu kuwa atakuja huyo aitwae Msaidizi.

Katika utangulizi wa nakla ya Biblia ya Revised Standard Version imeelezwa kuwa hata hiyo matini ya Kigiriki ilioko "imeharibiwa na makosa yaliyojumlika kwa kukosoea kosea kwa walionukulu muda wa karne kumi na nne."

Wataalamu wa Biblia wakubwa kama Rudolf Bultmann (Mprotestanti) na Father John Lawrence Mackenzie (Mkatoliki) wanakubali kuwa sehemu nyengine za Injili si kweli kihistoria, na ya kwamba maneno fulani ya Yesu kwa hakika yamebuniwa na Kanisa la kale.

Ni makosa kusema kuwa huyo Periklitos (Msifiwa) aliyefasiriwa kwa kukosea Msaidizi, ni Roho Mtakatifu, ambaye Wakristo wanasema ni nafsi ya Mungu. Ushahidi wa makosa hayo umo humo humo katika Injili ya Yohana.

Kama huyo Msaidizi ni Roho Mtakatifu kwanini Yesu alisema "yawafaa ninyi mimi niondoke; kwa maana mimi nisipoondoka, huyo (Periklitos) hatakuja kwenu.???

Roho Mtakatifu twaambiwa ni Mungu wa milele. Je, kwani Mungu hatokuwepo maadamu Yesu yupo?

Je, yeye Yesu na Manabii wote waliomtangulia na watakatifu wengine hawakuteremkiwa na Roho Mtakatifu?


Injili ya Mathayo, nayo inatueleza kuwa Yesu alibashiri kutokea kwa Muhammad, ambaye ni katika uzao wa Ismaili, anayefananishwa na jiwe liliokataliwa na wajenzi.

Pia Yesu alibashiri kuinuka kwa Umma wa Kiislamu utakaopewa Ufalme wa Mungu, nayo yote hayo yakatimia:

Yesu akwaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni; Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu?

Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake. Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vunjika; naye ye yote ambaye litamwangukia, litamsaga tikitiki.
Mathayo 21.42-44
 
Huyo Roho wa Kweli anayezungumziwa ha Yesu hapa tunajua ni Roho Mtakatifu na sio SWW. Na alikwisha kuja siku ile mitume waliposhukiwa na Roho Mtakatifu ndio siku ya Pentekoste kama iliyoandikwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume 2:1-47.

Yohana 16:7-8. “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke; kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu;”

Hii haiwezi kumaanisha Roho Mtakatifu; kwa vile Roho Mtakatifu inasemekana kwamba alikuwepo hata kabla ya Yesu hajazaliwa kama ilivyo katika Luka 1:41 “Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu”.

Hapa, Roho Mtakatifu vile vile alikuwepo wakati wa Yesu:

sasa vipi hii imaanishe kwamba ni sharti aondoke Yesu ndipo Roho Mtakatifu aweze kuja?
 
Back
Top Bottom