Dar: Mfanyabiashara Mohamed Dewji(Mo Dewji) atekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay

Dar: Mfanyabiashara Mohamed Dewji(Mo Dewji) atekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay

Dah tunaletewa movie nyingine
.sijui itakuwa na part 2?
.sijui itachezwa kwa ustadi au itafanana na zile nyingine?
.sijui inataka kumpa kiki nani ?

Wakati utasema...stay tuned....!!!!
Wewe ndio umeona mbali..

Hivi Manji atekwe kwa lipi alilofanya la kutisha?
 
Kuna hizi habari kwamba Mfanyabiashara Mohamed Dewji ametekwa leo asubuhi maeneo ya Collosium Gym , Oysterbay alipokuwa ameenda kufanya mazoezi..

Mwenye habari kamili atujuze.

======

UPDATES:

Mfanyabiashara maarufu nchini, ambaye pia ni mwekezaji wa Klabu ya Simba, Mohammed Dewji (Mo Dewji), anadaiwa kutekwa na watu wasiojulikana waliokuwa na silaha za moto, saa 11 alfajiri wakati akiingia kufanya mazoezi katika gym ya Colosseum, Oysterbay jijini Dar leo Oktoba 11. Kamanda wa Polisi Kinondoni, Jumanne Muliro athibitisha.

RPC Lazaro Mambosasa amesema Polisi Dar inafuatilia madai ya kutekwa kwa mfanyabiashara huyo maarufu nchini

UPDATE 1:

Dereva wa Uber amesema aliona watu 4 wakishuka kwenye gari dogo, wakiwa wamejifunika usoni, wakapiga risasi moja juu na kumchukua Mohammed Dewji

UPDATE 2:

RPC Lazaro Mambosasa amesema waliomteka mfanyabiashara Mohamed Dewji (Mo) ni wazungu wawili. Aidha, amesema msako mkubwa unafanywa kwa raia wa kigeni wote waliopo nchini kufuatia kutekwa kwa Mo Dewji

UPDATE 3:

RPC Lazaro Mambosasa amesema watu watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano kuhusu kutekwa kwa mfanyabiashara Mo Dewji

haya kumekucha.. ngoja tuone.. watakavyojihusisha na tukio hili la MO maana tunavojua hili tukio halina tofauti na la ANTIPAS T LISSU. Sasa tuone ufatiliaji utakavyofanyika na hatimae tupate majibu kwa muda mfupi kuliko tunavotarajia.. japo kwa tukio la LISSU mpaka leo hiii hata hiyo NISSANI JEUPE halijapatikana hata ile taarifa ya camera kunyofolewa haijatolewa maelezo.
 
Hapana inategemea na mtu...fuatilia maisha anayoishi Warren buffet au aliyokuwa akiishi Steve job utaona..ni wewe tu jinsi unavyojiweka na jamii..

Hao wote unadhani hawana security?!umeshasikia wareen buffet anaenda kwny public gym?!...Watu kama hao issue ya security inakuwa sio juu yao makampuni yao yenyewe ndio yanadeal na security yake na wanatumia peaa nyingi sn kwny issue ya security bila hivyo ungekuwa unasikia matukio mengi sn ya mabilionea kutekwa
 
Screenshot_2018-10-11-10-14-07.png
 
taarifa zinasema watekaji walifunika nyuzo zao, mambosasa na kikundi chake tayari wameshajua ni wazungu. wamejuaje?
Huwa taarifa yake ya mwanzo inapingana na atayoitoa baadae, ngoja tuone na tukio hili kauli atakayoitoa tena
 
Hapana inategemea na mtu...fuatilia maisha anayoishi Warren buffet au aliyokuwa akiishi Steve job utaona..ni wewe tu jinsi unavyojiweka na jamii..
Kumbuka Jamii yenyewe ndo hii hii yenye majambazi Na vibaka.. Kuishi vizuri Na Jamii yako hakumzuii MTU kukudhuru mkuu. Mo alitakiwa akumbuke yeye ni asset.
 
Back
Top Bottom