Dar: Mfanyabiashara Mohamed Dewji(Mo Dewji) atekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay

Dar: Mfanyabiashara Mohamed Dewji(Mo Dewji) atekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay

Kutekwa kwa Mo Dewji kutakuwa na athari nyingi sana.
Muathirika wa kwanza ni jeshi letu la polisi.

Kama tulivyoona habari za Mo zimetikisa dunia nzima, na macho ya dunia yana sikiliza kujua jeshi letu la polisi litatumia weledi gani kumpata Mo na watekaji wake.
Kwa vile watekaji inasemekana ni wazungu, hapa si tena kazi ya virungu na kutoa " kipigo cha mbwa koko" , maana watekaji ni maproffessionals, na polisi inabidi waonyeshe u proffessionalism wa hali ya juu kutatua tatizo hili.

The world is watching.
Wakilimaliza hili kwa weledi wa kutukuka tutahoji tena kwa nguvu sana, vipi kuhusu Azory na Saanane? Vipi kuhusu "wasiojulikana" waliomjeruhi vibaya TAML?
 
Hakuna lolote la maana wanalolizungumza zaidi ya kuongeza maswali tu, huyo Waziri bora akae kimya tu maana ndio wale wale tu wasiojua nini cha kuongea na kuanza kuropoka tu
Mkuu wanaojua cha kuongea wako idara gani hiyo?
 
Hata mimi mpaka sasa najiuluza swali hilo na sipati majibu.
Ninyi watu wa ajabu sana...! Makonda kazunguza kidogo mumtie kaa la moto mdomoni...huku mkitaka akae kimya vyombo vya usalama vifanye kazi yake na ili ushahidi usivurugike...hakuja kucha sawa sawa mnamtaka Mh. Lugola aseme..ili mpate cha kuzungumza kwa kebehi...what is wrong with you, 'people'!?
 
Nitajie nchi moja tu, yoyote ile ambayo tajiri wake mkubwa kuliko wote aliwahi kutekwa na saa 24 kupita bila vyombo vya dola kuwa na clue!

Kwamba, eti "haijalishi huyo mtu ni maarufu au kama mimi" hiyo ni kujaribu ku-justify uozo uliopo kwenye mfumo wetu wa ulinzi na usalama! Endelea kujidanganya kwamba akina eti sie tupo sawa tu na akina Reginald Mengi na kwamba, utekwaji wa yeyote miongoni mwetu hiyo ni ishara mbaya! Ni kweli, ni ishara mbaya lakini anapotekwa mtu kama Mo Dewji, hiyo sio tu ni ishara mbata bali ni ishara mbaya zaidi na zaidi!

Sie wengine miaka kadhaa iliyopita tulishuhudia Mzee Reginald Mengi akipewa ulinzi wa polisi nyumbani kwake Oysterbay baada ya kutishiwa kuuawa! Kama unaamini wewe na Mzee Mengi ni sawa, basi nenda kwenye kituo cha karibu ukaripoti kwamba unatishiwa kifo na kisha wathibitishe kwamba kweli unatishiwa kifo halafu uone kama unapewa askari polisi wa kuja kukulinda hapo unapoishi!!!

Mtu kama mimi, nitaenda viwanja gani kama sio Tandale, Mwananyamala, Manzese, Temeke n.k! Huko haitashangaza nikitekwa kwa sababu mfumo wetu wa ulinzi haujafika kisawasawa hadi Uswahilini!!! Lakini inapotokea mtu anatekwa maeneo kama ya Colleseum na kupita 24 hours bila vyombo vya dola kuwa na clue, hapo akina sie hatutaacha kujiuliza ikiwa maeneo kama yale na mtu kama yule anaweza kutekwa na watekaji kutokomea kusikojulikana! Maeneo ambayo angalau yana mifumo mizuri ya mitaa ambayo ingewezesha kuwa na street cams; vipi akina sie tunaoishi Kwa Mtogole! Huku kwetu watu si wanaweza kuingia hadi na vifaru na wasionekane!!

Ikiwa maeneo kama yake hayana hata Patrol inayoweza ku-respond kwa haraka anapotekwa mtu kama Mo Dewji, vipi huku kwetu?Ikiwa Richest Person anaweza kutekwa na polisi wasiwe na clue hata baada ya saa 24 kupita huku tukifahamu wamewekeza nguvu zao zote katika kufanya msako! Vipi ninapotekwa mtu kama mimi ambae polisi haitaweza kutoa japo askari mmoja kutafuta nipo wapi!!!

Kwa wale wanaoamini katika siku ya huku, mimi na Mo Dewji ni sawa lakini ni sawa mbele ya mwenye kiti cha enzi lakini hatuna usawa wowote mbele ya viti vya akina Magu!!

No wonder tunapotekwa akina sie wala hakuna anayejishughulisha! Endelea kuhangaika ku-justify ujinga!

Mkuu, Ishu hapo ni MASLAHI. Utatafutwa kwa bidii kiasi gani kuendana na wanaokutafuta wana maslahi kiasi gani na wewe.

Unaweza kuwa Tajiri mkubwa au mtu Maarufu lakini uhusiano wako na wanaokuzunguka ni mbovu au wivu ama wanakuchukia tuu kwa sababu wanazojua wao. Hapo ukipotea watu watasema bora tuu apotee, wataendelea tuu na shughuli zao kama vile hakuna kilichotokea. Pamoja na mapesa uliyonayo, no one will give a sht about yr disappearance!
 
Na wala hawawezi kwenda huko manake wanaweza kufanya assumption kwamba police wangeweza ku-react mapema na hivyo kuweka vizuizi kwenye barabarani hususani ya Kilwa Roand na ile iendayo Kisarawe! Pale si karibu na bahari! Unaenda kufanya tukio huku speed boat ikiwa standby! Mkishapata mtu wenu, moja kwa moja mlipoegesha boti itakayowatoa kwenye eneo la tukio kwa haraka! Huko mbele za safari, unamtoa kwenye boti ambayo inaweza ku-catch attention unamwingiza kwenye mashua ya uvuvi yenye wavuvi fake!

Hapo mtaenda na "mzigo" wenu hadi Mombasa bila kokoro! Kinyume chake, mnaweza kutia nanga maji marefu huku wavuvi fake wakijifanya wapo bize na nyavu huku wenye mchezo wao wakifanya chochote na mateka wao hadi watakapohitimisha walichokusudia kufanya!


Kumtoroshea Baharini kwa speed boat kwenda nchi nyingine wanaoweza kufanya kitu kama hiki ni Internationally organized criminal groups au majasusi tu na si nje ya hapo. Akili yangu inakataa majambazi wa kawaida wa nchini kwetu kuemploy mbinu kama hizi! And of course lazima jamaa wametumia akili nyingi katika kusuka na kutekeleza uhalifu kama huu.
 
Hakuna lolote la maana wanalolizungumza zaidi ya kuongeza maswali tu, huyo Waziri bora akae kimya tu maana ndio wale wale tu wasiojua nini cha kuongea na kuanza kuropoka tu
Huyo waziri asijesema Mo ameenda kutafita maisha!
 
Watekaji sio maboya wale " ... fununu nilizozsikia ni kwamba walitupa simu ya mo ". kama walikuwa na akili ya kufanya hivyo " basi tu assume kuwa walikuwa na kifaa cha kumfanyia scanning ili waweze kuona kama amefungwa GPRS ... (yote hayo yange jiri endapo itakuwa mo alifungwa hicho kifaa )
 
Huyu ni mnyama wa mwitu hana ubinadamu hata kidogo
Screenshot_2018-10-12-08-10-45~2.jpg
 
Najiuliza swali hili baada ya kuona vyombo vikubwa vya habari duniani vikiwemo BBC, CNN, Al jazira, Xiua na Reuters vikiripoti na kulifuatilia kwa karibu tukio hili la utekaji lililotokea nchini mwetu!
Wanashangaa nchi yenye amani na utulivu yanatokea hayo
 
Na wala hawawezi kwenda huko manake wanaweza kufanya assumption kwamba police wangeweza ku-react mapema na hivyo kuweka vizuizi kwenye barabarani hususani ya Kilwa Roand na ile iendayo Kisarawe! Pale si karibu na bahari! Unaenda kufanya tukio huku speed boat ikiwa standby! Mkishapata mtu wenu, moja kwa moja mlipoegesha boti itakayowatoa kwenye eneo la tukio kwa haraka! Huko mbele za safari, unamtoa kwenye boti ambayo inaweza ku-catch attention unamwingiza kwenye mashua ya uvuvi yenye wavuvi fake!

Hapo mtaenda na "mzigo" wenu hadi Mombasa bila kokoro! Kinyume chake, mnaweza kutia nanga maji marefu huku wavuvi fake wakijifanya wapo bize na nyavu huku wenye mchezo wao wakifanya chochote na mateka wao hadi watakapohitimisha walichokusudia kufanya!

Chavda aliwahi kukimbia na speed boat hapa enzi za Mwinyi au Mkapa na akatokomea, Pia kuna kisa cha boat moja ikijulikana kama seaexpress au butterfly (hapa sikumbuki vizuri jina) jamaa walikuwa wanadaiwa kodi nyingi sana lakini siku moja waliipandisha boti yao pale posta kwa ajili ya matengenezo na walipoenda for sea trial jamaa wakatokomea na walipojaribu kufuatwa hawakuonekana taarifa zikatoka kwa polisi wa Kenya/Mombasa kuwa jamaa walishakatiza maeneo ya Somalia muda mrefu sana. Hili la MO najaribu hata mimi kulifikiria katika angle hiyo kama kweli wale ni watekaji wenye shida naye kweli lazima watakuwa wametumia njia hiyo ndio maana strategically lazima atekwe maeneo ya oysterbay ambapo fukwe ziko karibu na wao ni rahisi kupark speed boat yao yenye horse power za kutosha, ukiwa na boat yenye horse power za kutosha kutoboa hapo ukanda wa Somalia, Yemen ni kugusa tu.
 
Duh ila wahusika nao watabe sana

Waliokamatwa miguu inakoma huko walipo
 
Back
Top Bottom