Dar: Msanii Nay wa Mitego amepata ajali ya bodaboda

Dar: Msanii Nay wa Mitego amepata ajali ya bodaboda

Wewe umetoa taarifa kwamba alipanda bodaboda baada ya kukwama kwenye foleni akiwa na gari yake. Halafu hapo chini bado tena unajiuliza maswali Wewe mwenyewe, tukueleweje?

Halafu ajali sio bodaboda tu, hata ukipanda ndege inaweza kukukuta.
 
Msanii Nay wa Mitego amepata ajali ya bodaboda wakati anawahi kwenye Interview ya kipindi cha Friday Night Live cha East Africa TV, kwa sasa msanii huyo yupo katika Hospitali ya Kairuki Mikocheni akipatiwa matibabu na hali yake bado haiko vizuri.

Taarifa iliyotolewa na EAST AFRICA RADIO inaeleza kuwa Nay alipanda bodaboda ili kuwahi kipindi baada kukwama kwenye foleni akiwa na gari yake. Tutaendelea kutoa taarifa zaidi za maendeleo ya afya yake.


.......................................................
Hivi ni kweli hadi sasa Nay anatumia bodaboda tena usiku kma usafiri? si tuliambiwa na alionesha ana magari mengi sasa imekuwaje?
Sasa hiyo gari ameacha kwenye foleni ikiisha itabaki hapo hapo au kamuachia mtu mwingine arudi nayo home tu ?
 
Huenda ni Kiki mana hawa wasanii ni wasanii kweli kweli , alafu Yale magari yake yako wapi? Au tuamini kauli ya shamsha Ford kwamba jamaa hata pa kulala hana
 
Binafsi naona kwa ajali ya bodaboda ambapo mwili wa binadamu ndiyo body lake na hana michubuko usoni wala bandeji kichwani inawezekana akawahi kupona.

Minus p.o.p kokote so pretty well kupona kupo.
 
Aisee Kuna dogo mmoja nampata alikuwa Yuko Safi tu mwili nyumba Ila boda boda imefanya awe mlemavu

Kavunjika mikono na mguu Yuko homu tu
 
Msanii Emmanuel Eribariki Munis (Nay wa Mitego), amepata ajali ya bodaboda wakati anawahi kwenye Interview.

Kwa sasa msanii huyo yupo katika Hospitali ya Kairuki Mikocheni akipatiwa matibabu na hali yake bado haiko vizuri.

Inaelezwa alipanda bodaboda ili kuwahi kipindi baada kukwama kwenye foleni akiwa na gari yake.

Hali yake haijatengamaa.
View attachment 1800835
Kwa jinsi wasanii wanavyorogana si ajabu ajali hii ikahusishwa na uchawi
 
Kuendesha Bodaboda hata uwe mstaarabu vipi kuna vitu utafanya kama bodaboda wengine.

Najua kama umewahi kuendesha pikipiki yoyote unakumbuka ujinga ambao umewahi kufanya. Pikipiki zina raha yake ambayo huvuruga ubongo unaanza kujiamini hata sehemu zisizofaa.

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom