DAR: Vijana watano wamepotea katika mazingira ya kutatanisha

DAR: Vijana watano wamepotea katika mazingira ya kutatanisha

Mmoja ama mwenzao na hao madogo kwa taarifa ni kwamba aliposikia hao madogo wamekamatwa alitoroka na hajulikani alipo hadi sasa. Huyo wanafanya nae biashara ya simu za wizi hapo Kariakoo.

Hii taarifa niliisikia hapo kariakoo juzi kwa mafundi nilienda kutengeneza simu yangu wakiwa wanaongea lakini sijui ukweli wake.

Isije kua madogo wamekamatwa na vikosi vya maangamizi hapa Bongo.

Mtoa mada akili huna. Wewe ndio ulipaswa opotee qenge mkubwa.
Nadhani mtoa mada yeye katoa tu taarifa kama ilivyo kwenye gazeti
 
Mi milikuwaga nawaza uji wali.sisomi mpaka ninywe uji wali na miogo ya kukaanga.nashushia na gubiti na pipi karanga nazifata Nera.
Kuhusu hii story kuna nyingine nimeisoma jana kuna dada alitoka out na mwenzake
Wakapiga kilaji kisha yele mwenzake akaondoka na danga
Kilichotokea mwenzake hakuoatikana mpaka walipokuta maiti yake muhimbili ikiwa imeondolewa figo
HILI JAMBO LINATISHA WAKUU MUWE NA TAHADHALI
HIZI OUT KUWENI MAKINI NAZO KAMA NDO TUMEANZA KUIBIWA FIGO KWA KUTEKA WATU
TUWE MAKINI
Ndugu wamekanusha, hajapasuliwa kokote tumboni
 
Rafiki wa dada yangu mume wake alipotea mwaka jana kama mwezi wa tisa hivi, na yeye pia alikua na wenzake sijui wawili au watatu sikumbuki vizuri ila walikua wanasafiri kuelekea tanga na gari private, Mara ya mwisho mawasiliano yao ilikua wakiwa tegeta baada ya hapo ndio kimyaaa, hadi leo wametafutwa kweli lakini hamna majibu, yule sister keshalia hadi amenyamaza amemuachia Mungu tu.. za kijiweni sasa kule mtaani wanasema eti yule kaka na wenzie ni Wezi wakubwa wa magari kwaiyo wale wamewekwa sehemu undeground sijui wapi hadi chain yote ishikwe..
 
Ukisikia mtu mweusi anamtenga ndugu yake ndio haya sasa. Ujumbe wa Kariakoo na Tanzania kwa ujumla ila mtu kaandika Kikristo.
 
Mmoja ama mwenzao na hao madogo kwa taarifa ni kwamba aliposikia hao madogo wamekamatwa alitoroka na hajulikani alipo hadi sasa. Huyo wanafanya nae biashara ya simu za wizi hapo Kariakoo.

Hii taarifa niliisikia hapo kariakoo juzi kwa mafundi nilienda kutengeneza simu yangu wakiwa wanaongea lakini sijui ukweli wake.

Isije kua madogo wamekamatwa na vikosi vya maangamizi hapa Bongo.

Mtoa mada akili huna. Wewe ndio ulipaswa opotee qenge mkubwa.
kama ishu zao ni kupika IMEI za simu za wizi basi huo ndio mwisho wao! Polisi huwa ina mtindo wa kuweka records za wahalifu ila kesi ikiwa reccuring huwa wanaamua kuwa eliminate tu kwa namna wanaoijua wao. Ila ni baada ya kuwapa maonyo sana kuwa acheni hio michezo😅
 
Sina elimu.


Basi nisamehe maana ningekudharau Sana Kama unashindwa kutofautisha mambo madogo Kama hayo.

Wapo wanapotea Kwa mambo ya kishirikina,
Wengine Kwa sababu za Mapenzi
Wengine Mali na wauza viungo
Wengine mambo ya Kisiasa.

Hata polisi kabla ya kumtafuta Mtu lazima wajue hadhi yake kijamii ili wabaini sababu ya mtu huyo kupotea ni kisiasa, kijamii au kiuchumi.

Mtu hajihusishi na Siasa atapoteaje Kwa sababu za Kisiasa, hakuna logic hapo.
 
Kama Majambazi ndiyo IMEISHA hiyo ,Polisi wanawapa VYUMA tu.
Hawa nina wasiwasi ni wale wachonga IMEI au wauzaji wa simu za ishu! Ukifuatilia kwa kina utagundua wale waliokamatwa mara kwa mara katika huenda katika maelezo walipoint kuwa dealers wanaowauzia hizo simu ni hawa vijana waliopotezwa. Na kimsingi polisi lazma walishatoa maonyo sana!
 
Tafsiri isiyo rasmi

Hofu imewakumba wazazi na jamaa za vijana watano ambao wameripotiwa kutoweka kwa zaidi ya wiki tatu sasa. Vijana hao watano wanaotajwa kuwa ni wafanyabiashara wa Kariakoo, walitoweka tangu Desemba 26 walipotoka kwenye sherehe za ufukweni Kigamboni.

Baadhi ya ndugu walisema walipata mawasiliano ya mwisho kutoka kwa vijana hao kuwa wamekamatwa na polisi lakini hadi sasa ni kitendawili waliko. "Tumetembelea vituo mbalimbali vya polisi, hospitali na hata vyumba vya kuhifadhia maiti lakini hatujapata fununu bado," alisema Bw Longili Martin, baba wa mmoja wa vijana hao waliotoweka. “Ninapozungumza na wewe, nimekuwa tu kwenye vituo vya Polisi vya Msimbazi na Central kuona kama kuna maendeleo. Kwa bahati mbaya, hakuna. Polisi wanasema tu kwamba wanachunguza,” alisema.
Bw Martin, mkazi wa Gongolamboto alieleza kuwa mara ya mwisho aliwasiliana na mtoto wake Edwin Kunambi mnamo Desemba 23, alipomwalika mtoto huyo kwenye sherehe za Krismasi. Kulingana naye, Edwin alimwambia kwamba hatajiunga na familia hiyo kwa sababu atakuwa na shughuli nyingi na akaahidi kujumuika nao Siku ya Mwaka Mpya. Alipotafutwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es Salaam, Jumamane Muliro, alisema anafahamu kupotea kwa vijana hao na kwa sasa polisi wanaendelea na uchunguzi wa suala hilo. Alikanusha madai kuwa wamewakamata wanaume hao ambao sasa wanawatafuta.

Baadhi ya wanafamilia wametoa taarifa polisi na tunasema si kila mtu aliyepotea anakamatwa na polisi. Sio kila mtu aliyepotea amekufa, mara kadhaa watoto hupotea na hupatikana mahali pengine…. Kwa hiyo mtu anapopotea watu wawe na subira,” alisema. Kwa mujibu wake, alipokuwa RPC wa Shinyanga na Mwanza, karibu kila siku watu walikuwa wakienda migodini, wanakaa huko kwa muda wa miezi sita na kurudi baada ya kushindwa kupata walichotarajia. "Polisi wanapowakamata watu, kwa kawaida tunatangaza ili wanafamilia wafahamu waliko," alisema.
Bi Sylvia Quentin, jamaa wa mmoja wa vijana waliopotea aitwaye Tawfiq Mohamed, alisisitiza kuwa wametembelea kila kituo cha polisi, hospitali na chumba cha kuhifadhia maiti zaidi ya mara mbili, lakini yote yameambulia patupu. "Hatuwezi kuendelea hivi, leo tunapanga kuandamana kwa Waziri wa Mambo ya Ndani na kuona jinsi gani anaweza kutusaidia," alisema. Bi Tabu Saidi aliiambia The Citizen kuwa mtoto wake Rajab Mdoe alikwenda nyumbani kwake Kinyerezi Desemba 26, akaomba gari ili aende ufukweni wa Kingamboni na marafiki zake kwa tafrija.
“Nakumbuka ilikuwa majira ya saa 2 mchana, alikuja na kuchukua gari. Ilipofika saa sita usiku, niliamua kumpigia simu lakini simu yake iliita bila kupokelewa. Haikunisumbua, kwa sababu nilijua atarudi lakini nilitilia shaka baada ya kutorudi hadi asubuhi,” alisema. Kulingana naye, alijaribu kupiga simu yake asubuhi na kwa bahati mbaya, haikupatikana. Aliongeza kuwa mnamo Desemba 27, marafiki wawili wa mwanawe walikwenda nyumbani kwake, kuarifu kwamba mwanawe alikuwa amekamatwa na polisi walipokuwa wakienda ufukweni.
"Nimeripoti suala hilo katika vituo vya polisi, nimepitia hospitali zote na vyumba vya kuhifadhia maiti lakini hakuna fununu," alisema, akiongeza kuwa hana la kufanya.
Mods nqomba muunganishe Iwe faida kwa Swahili audience
 
Kuna kaka wa marehemu alikuwa anasimulia Clouds fm PB.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]mkuu umechanganya madesa yule sio kaka yao...yule ni mtangazaj wa clouds anaitwa mbarouk khan. Na yeye alikua anashare tu kisa chake cha kufanana na hvo,jinsi kakake ilivomtokea.
 
Kuna siku nipo catalunya Barcelona,, Spain.
Nilikuwa nahitaji kuelekezwa Jambo fulani.
Niliuliza kila mspanish kwa lugha ya English,,na sikupewa majibu.

Kila mtu niliyokutana nae nilipoongea English alionyesha kunikwepa., .
sababu ya English.
Nilihangaika sana siku hiyo,,

Mwisho nilikutana na jamaa mmoja,, nilipoongea English,,
Aliniangalia kwa dharau halafu akanijibu kwa English.
"" this is not an English country.""
Speak Spanish or catalunya.

Nilijiona zuzu kweli kweli..
Njoo sasa bongo hapa kwa wasiojielewa ukijua kingereza na kuokteza mambo wanakuamini

Mfano mange kimambi na fatuma karume kwa kile kingerza chao wanaonekana watu wa maana na vijana wa ovyo wanawaamini asilimia 100 yaani sijui kwa nn
 
Hawa nina wasiwasi ni wale wachonga IMEI au wauzaji wa simu za ishu! Ukifuatilia kwa kina utagundua wale waliokamatwa mara kwa mara katika huenda katika maelezo walipoint kuwa dealers wanaowauzia hizo simu ni hawa vijana waliopotezwa. Na kimsingi polisi lazma walishatoa maonyo sana!
Interesting..
 
Rafiki wa dada yangu mume wake alipotea mwaka jana kama mwezi wa tisa hivi, na yeye pia alikua na wenzake sijui wawili au watatu sikumbuki vizuri ila walikua wanasafiri kuelekea tanga na gari private, Mara ya mwisho mawasiliano yao ilikua wakiwa tegeta baada ya hapo ndio kimyaaa, hadi leo wametafutwa kweli lakini hamna majibu, yule sister keshalia hadi amenyamaza amemuachia Mungu tu.. za kijiweni sasa kule mtaani wanasema eti yule kaka na wenzie ni Wezi wakubwa wa magari kwaiyo wale wamewekwa sehemu undeground sijui wapi hadi chain yote ishikwe..
Na gari je haikupatikana? Unajua Tanzania tunasema ni kisiwa cha amani ila kuna mambo yanaendelea kimya kimya and no body cares labda mpaka ya kukute ndo unaanza lia lia
 
Haya mambo kwenye ukanda wa Afrika mashariki yanatamaradi sana, kule Kenya napo kuna vijana kadhaa wamepotea na baadae kuonekana eneo lingine pembezoni mwa mto.
 
Back
Top Bottom