Dar: Wananchi Mikocheni wagomea Kituo cha Mafuta kujengwa kwenye makazi yao

Dar: Wananchi Mikocheni wagomea Kituo cha Mafuta kujengwa kwenye makazi yao

-Kabla ya kufanya mabadiliko ya matumizi ya ardhi, kunatakiwa kutolewa notisi ya siku kadhaa, kwa yeyote mwenye Pingamizi apeleke kwa Mkurugenzi wa halmashauri,
- Na pia Panatakiwa pafanyike mkutano na Wananchi watoe mawazo yao
 
Nikisoma baadhi ya michango ya wadau napata uzuni kubwa kwa taifa langu Tanzania! Hii mitandao imesaidia sana kubaini uwezo wa fikra za watanzania wa sasa, juzi kulikuwepo mada kuhusu marufuku ya matumizi ya bangi comments nyingi zilionesha ni upuuzi kuzuia matumizi ya kilevi hicho, nikaenda jamiicheck kwenye ufafanuzi wa athari za bangi sikuona comment hata moja au ya kukubaliana na marufuku au kuikataa!

Hii yaja mada ya kituo cha mafuta kujengwa kwenye barabara ya huduma za dharura kwenye makazi ya watu (access road) bado kuna wanaoona marufuku ya ujenzi huo ni upuuzi, kwamba hawajui umuhimu wa access roads, kwamba hawajui athari za kituo cha mafuta katikati ya makaazi ya watu (japo aliyechomoa battery kule msamvu miaka fulani) alama ya athari zake ipo mpaka leo lakini hapa kuna watu hawawazi kwamba hata kituoni hapo battery yaweza chomolewa pia. Lakini hawajui kama huwa kuna mipango miji yenye master plan inayoonesha kila ardhi na matumizi yake, na kwamba mkuu wa wilaya anaposema atachunguza vibali alivyokutwa navyo bwana mwekezaji kama vilipatikana kiharari yupo sahihi!

Hutimisho, hatuwezi kuendeleza uhalifu eti kisa uhalifu huo unatendeka kwa wengine wawe waburuza ndala au vigogo.
 
Licha ya kuwa ni idea nzuri ila sioni point zao,
At the end hicho kituo kitajengwa tu,
Huwezi sema kisa ni Access road hivyo haistahili uwepo wa kituo cha mafuta, + kuhusu eneo kwani hiyo sheli itakuwa inakaa na magari all the time?

Mimi binafsi sioni kama wana point,
Kama hujui abc za mipango miji lazima uongee pumba kama hii ujinga ni mzigo
 
Nikisoma baadhi ya michango ya wadau napata uzuni kubwa kwa taifa langu Tanzania! Hii mitandao imesaidia sana kubaini uwezo wa fikra za watanzania wa sasa, juzi kulikuwepo mada kuhusu marufuku ya matumizi ya bangi comments nyingi zilionesha ni upuuzi kuzuia matumizi ya kilevi hicho, nikaenda jamiicheck kwenye ufafanuzi wa athari za bangi sikuona comment hata moja au ya kukubaliana na marufuku au kuikataa!

Hii yaja mada ya kituo cha mafuta kujengwa kwenye barabara ya huduma za dharura kwenye makazi ya watu (access road) bado kuna wanaoona marufuku ya ujenzi huo ni upuuzi, kwamba hawajui umuhimu wa access roads, kwamba hawajui athari za kituo cha mafuta katikati ya makaazi ya watu (japo aliyechomoa battery kule msamvu miaka fulani) alama ya athari zake ipo mpaka leo lakini hapa kuna watu hawawazi kwamba hata kituoni hapo battery yaweza chomolewa pia. Lakini hawajui kama huwa kuna mipango miji yenye master plan inayoonesha kila ardhi na matumizi yake, na kwamba mkuu wa wilaya anaposema atachunguza vibali alivyokutwa navyo bwana mwekezaji kama vilipatikana kiharari yupo sahihi!

Hutimisho, hatuwezi kuendeleza uhalifu eti kisa uhalifu huo unatendeka kwa wengine wawe waburuza ndala au vigogo.
Hata mkuu wa wilaya hajui taratibu za mipango miji
Tanzania ni nchi iliyopo gizani
 
"Mkazi mwingine wa eneo hilo, Profesa Anna Tibaijuka amesema kituo hicho cha mafuta kinajengwa kwenye makazi ya watu kinyume cha sheria"
 
Kuna gas station moja ya Puma ipo Survey pale, huwa naitazama nashindwa kuelewa ilikuaje ikajengwa pale...

Kuna gas station nyingine ipo barabara ya Msewe (jina lake silijui), ila ipo katikati ya makazi ya watu, sijui walipataje vibali wale...
 
Wananchi wakazi wa Mtaa wa Ally Hassan Mwinyi, Kata ya Mikocheni wilayani Kinondoni Dar es Salaam wamelalamikia kujengwa kwa Kituo cha kuuza mafuta cha Barrel Petrol Station karibu na makazi yao.

Kituo hicho kinajengwa katika Barabara ya Senga, Mtaa wa Ally Hassan Mwinyi Kata ya Mikocheni.

Mmoja wa wananchi wa Mtaa huo, ambaye hakutaka kutaja jina lake alisema sheria ya mabadiliko ya matumizi ya ardhi haikufuatwa kabla ya ujenzi huo.

Mwananchi huyo ambaye amejitambulisha kuwa yeye ni mtaafu serikalini, alisema kabla ya kuanza kwa ujenzi huo, sheria inamtaka mtu anayetaka kubadilisha matumizi ya ardhi kushirikisha wananchi ikiwa ni pamoja na kuweka matangazo eneo la wazi kwa muda wa siku 21 ili kama kuna pingamizi litolewe.
View attachment 2814581
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule (mwenye suti) kushoto akisikiliza malalamiko ya wananchi wa Mikocheni kuhusu madai ya ujenzi wa kituo cha mafuta katika makazi ya watu.

“Haya mabadiliko ya matumizi ya ardhi katika eneo hili haikutushirikisha, matangazo hayakuwekwa. Tumekuja kushtuka ujenzi umeanza.”amesema mwananchi huyo.

Mkazi mwingine wa eneo hilo, Profesa Anna Tibaijuka amesema kituo hicho cha mafuta kinajengwa kwenye makazi ya watu kinyume cha sheria.

“Kwanza barabara hii si barabara kuu, hii ni access road (barabara ndogo ya mtaani), huyu anajenga kituo cha mafuta, yatakuja magari maroli makubwa hapa hakuna hata nafasi, barabara hii ni finyu sana, na si eneo zuri kwa usalama na afya za wananchi ” alisema Profesa Tibaijuka.

Profesa Tibaijuka ambaye amepata kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, alisema kuwa suala hilo tayari wamelifikisha kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambaye analishughulikia.

“Tunamshukuru mkuu wetu wa wilaya ameanza kulishughulikia kwa kufika eneo kinapojengwa kituo hiki cha mafuta, tunaamini suala hili litapata ufumbuzi.”aliongeza Profesa Tibaijuka.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule amekiri kupokea malalamiko hayo na wananchi wa Mikocheni.

“Kweli nilipokea malalamiko ya wananchi hao, jana nilikwenda kujionea mazingira ya kituo hicho kinachojengwa, nilichokigundua kampuni inayojenga kituo hicho inavyo vibali vyote vya ujenzi kikiwamo cha Baraza la Mazingira (NEMC).
View attachment 2814583
“Ni kweli nilipokea malalamiko ya kituo cha mafuta kujengwa katika makazi ya watu, jana nilikwenda (Novemba 14,2023) kujionea mwenyewe.

“Nilichokigundua ni kwamba hiyo kampuni inavyo vibali vyote vya ujenzi kikiwamo cha NEMC (Baraza la Mazingira), hatua inayofuata sasa ni kuangalia kama zile hatua za utoaji wa vibali hivyo ulifuatwa au kuna kilichokosewa. Baadaye nitakwenda kuwaeleeza wananchi tulikofikia”alisema Mkuu huyo wa Wilaya ya Kinondoni.

Mmoja wa makandarasi wanaosimamia ujenzi wa Kituo hicho (jina tunalo), alipopigiwa simu kuzungumzia suala hilo, aliahidi kupiga simu baadaye. “Nitakupigia, subiri”ulisomeka ujumbe wa simu kutoka kwa mkandarasi huyo.

Chanzo: MATUKIODAIMA
Wananchi wamefungua macho sasa. Sisi mtaani kwetu tumezubaa hadi kituo kimefunguliwa kiwanja cha makazi ya watu maana hatukutangaziwa mabadiliko ya matumizi.
 
Kwamba unavyoona kwa akili yako mkuu wa wilaya yuko sahii
Yuko sahihi ndio kwa sababu amejipa muda wa kuchunguza vibali alivyo navyo mwekezaji ili kubaini kama ni harari ndipo arudi kwa wakaazi wa eneo kuwapa majibu ya hatua zitakazofuata.
Huoni kama kafuata utaratibu sahihi?
 
Vituo vyote viko karibu na makazi akiona vipi arudi UN Habitat aje mpango kazi vituo vikae hewani sasa....anataka viwe karibu na makazi ya wadudu ? Kote kote kuna makazi na vituo vipo niambie kituo kilicho mbali na makazi watu ? Atuondelee umaarufu na kick zake
 
Nikisoma baadhi ya michango ya wadau napata uzuni kubwa kwa taifa langu Tanzania! Hii mitandao imesaidia sana kubaini uwezo wa fikra za watanzania wa sasa, juzi kulikuwepo mada kuhusu marufuku ya matumizi ya bangi comments nyingi zilionesha ni upuuzi kuzuia matumizi ya kilevi hicho, nikaenda jamiicheck kwenye ufafanuzi wa athari za bangi sikuona comment hata moja au ya kukubaliana na marufuku au kuikataa!

Hii yaja mada ya kituo cha mafuta kujengwa kwenye barabara ya huduma za dharura kwenye makazi ya watu (access road) bado kuna wanaoona marufuku ya ujenzi huo ni upuuzi, kwamba hawajui umuhimu wa access roads, kwamba hawajui athari za kituo cha mafuta katikati ya makaazi ya watu (japo aliyechomoa battery kule msamvu miaka fulani) alama ya athari zake ipo mpaka leo lakini hapa kuna watu hawawazi kwamba hata kituoni hapo battery yaweza chomolewa pia. Lakini hawajui kama huwa kuna mipango miji yenye master plan inayoonesha kila ardhi na matumizi yake, na kwamba mkuu wa wilaya anaposema atachunguza vibali alivyokutwa navyo bwana mwekezaji kama vilipatikana kiharari yupo sahihi!

Hutimisho, hatuwezi kuendeleza uhalifu eti kisa uhalifu huo unatendeka kwa wengine wawe waburuza ndala au vigogo.
Bangi na Sigara ipi ina madhara makubwa??
 
Back
Top Bottom