Dar: Watu 7 wapofuka Macho kwa kujitibu Ugonjwa wa 'Red Eyes' kienyeji

Dar: Watu 7 wapofuka Macho kwa kujitibu Ugonjwa wa 'Red Eyes' kienyeji

Ule ugonjwa ata usipoutibu unapona wenyewe ni kunawa uso tu na soap
si ndo hapo sasa, mm nashangaa Mpaka vingozi wa afya wanatia attention kubwaa ya kuogoflaaa, Mwili wenye afya hauwez kukaa na red eye disease zaidi ya week mbili,

Tafuna carrot, matango, maji kwa wingi ebupa vitu ya sukari nyingi basi, sasa watu wanaweka limao kwenye macho😲!!? Unaongeza acidity level kwenye jicho kwann usipofukee
 
Hawa wahuni tu.
Hawa walishadidia kupiga "nyungu" na miti isiyoeleweka wakati wa Corona.
Watupe takwimu watu wangapi walikufa kwa kupiga nyungu mkorogo!
 
Hawa wahuni tu.
Hawa walishadidia kupiga "nyungu" na miti isiyoeleweka wakati wa Corona.
Watupe takwimu watu wangapi walikufa kwa kupiga nyungu mkorogo!
Hujawahi kwenda hospital ukaambiwe mfukize mtoto? Nyungu ni kufukiza na ni tiba.
 
Hadi maduka ya uchochoroni zipo dawa za matone ya macho, au watu wanaona mzuka wakiambiwa tia mafuta ya taa au mkojo wa punda wanajua hiyo ni komesha ya ugonjwa, kumbe wanaishia kukomesha macho yao wenyewe....
 
Mtu anaweka kila atakachoambiwa, limao anaweka, kesho akiambiwa ni mkojo anatia, keshokutwa akiambiwa ni chumvu ya mawe anaweka, yaani hata hajionei huruma na ukizingatia ni part sensitive sana na haina spare.
Dawa ya uhakika ni moja tu! Kunawa uso kwa sabuni kila baada ya masaa kadhaa ili kuhakikisha huambukizi wengine na mwili unajitibu wenyewe baada ya siku 7 hadi 10.
 
Hadi maduka ya uchochoroni zipo dawa za matone ya macho, au watu wanaona mzuka wakiambiwa tia mafuta ya taa au mkojo wa punda wanajua hiyo ni komesha ya ugonjwa, kumbe wanaishia kukomesha macho yao wenyewe....
Usitumie hizo dawa bila ushauri wa dakitari, kila dawa inalenga tatizo tofauti na nyingine.
 
Kwa hiyo wanaouza pharmacy hawajui matumizi yake? hizo ni antibiotics tu hata maelezo yake yapo kwenye lebo
Acha ubishi, uamuzi ni wako kwani kila kichupa kinakutahadharisha kupata ushauri wa dakitari.
 
Sasa kwanini hawajaweka wazi hizo namna za kienyeji zilizotumika kujitibu zilizopelekea upofu ili watu wachukue tahadhari wakati mwingine?

B... ungenikuta kipofu huku. Mdakuzi
 
Sasa kwanini hawajaweka wazi hizo namna za kienyeji zilizotumika kujitibu zilizopelekea upofu ili watu wachukue tahadhari wakati mwingine?

B... ungenikuta kipofu huku. Mdakuzi
Mkuu Tanzania kuna tatizo la mass ignorance na hili siyo tukio la mwisho wala la kwanza. Magufuli alijenga mpaka ''maabara'' ya kijifukiza kwenye hospital kubwa kuliko zote nchini, yenye mabingwa wa kitabibu na watu wakamuangalia tu. Tatizo letu ni zaidi ya kujua dawa za kienyeji walizotumia.
 
Ila wabongo nao ni tatizo inakuwaje mtu akwambie kitu fulani kinatibu ugonjwa fulani basi nawe bila kutafakari unatumia tu! Haya tunawapa pole.
 
Zipo na zinasaidia ukiweza kuapply mapema kabla ya tatizo halijakaa sana , na kuna namna yake ya kufanya kwa mtu aliyepata maambukizi ya red eyes, kwa mfano inashauriwa kama umegundua dalili la kuathiriwa na red eyes kwenye moja ya jicho lako basi ni vema kuanza kuweka (ma) tone kwenye lile ambalo bado halijaanza kuathiriwa ili kuepusha maambukizi, ila si unajua watanzania na akili zetu watu wanaokoteza maneno ya vijiweni ndio maana umesikia wengine wamenawa maji ya chumvi na limao, wengine wamepaka asali, utashindwa kupofuka kweli?haya ni sawa na yale ya Covid 19, kila mtu aligeuka daktari akaja na mbinu yake, ili mradi taflani.
Matone ya nini?
 
Mkuu Tanzania kuna tatizo la mass ignorance na hili siyo tukio la mwisho wala la kwanza. Magufuli alijenga mpaka ''maabara'' ya kijifukiza kwenye hospital kubwa kuliko zote nchini, yenye mabingwa wa kitabibu na watu wakamuangalia tu. Tatizo letu ni zaidi ya kujua dawa za kienyeji walizotumia.
Mkuu usinikumbushe hayo mambo, awamu ya 5 ukiitafakari ni kwamba hii nchi wote tuligeuka vichaa.
Mengi yalifanyika hadi huwa nahofia tutawajibu nini watoto wetu, tulikuwa wapi wakati yote hayo yanatokea?
 
Back
Top Bottom