Dar watu wana roho mbaya sana, nimeamua nikalale stendi kesho nirudi zangu mkoani

Dar watu wana roho mbaya sana, nimeamua nikalale stendi kesho nirudi zangu mkoani

Ushimen

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2012
Posts
40,828
Reaction score
99,523
Huyu jamaa ni ndugu yangu wa karibu kabisa. Yaani ni mjukuu wa shemeji yake na binamu wa mamaangu wa kambo.

Ni siku ya tatu sasa tangu nifike hapa mjini, baada ya kuuza ng'ombe nikaona sio mbaya nikaosha kidogo macho na ning'arishe ngozi kwa maji ya mwambao.

Sasa nilifikia kwa huyu ndugu yangu wa karibu kabisa. Kwakweli walinikaribisha uzuri na sote tulifurahi na kukumbushana habari za majirani wa kule kijijini, siku hiyo walinitandikia jikoni na nikalala bila tatizo hadi ikawa asubuhi.

Nilipo amka nikakuta sebleni wameweka chai mezani na kamkate kamoja, mie nikakakata vipande viwili nikaloweka kwenye chai nika kakula kakaisha. Kwanza chai yenyewe niliona niweke kwenye bakuli la kunawia na ikaishia humo, maana tuvikombe niliona twa watoto.

Kisha nikaondoka nikaenda kwenye genge la jirani nikanunua viazi ili nikazie maana nilikua sijashiba.

Mchana nilipo rudi, nikakuta ugali umepikwa kidogo kama kilo mbili tu, mie nikaula ukaisha na ile mboga nikamaliza yote hadi mchuzi nikaunywa.

Sasa nilipo rudi jioni nikawekewa kikao na mke wa ndugu yangu kwamba nina tabia mbaya, nami nikamuuliza "tabia gani"? Akajibu kwamba sifai kukaa kwake, basi nikasema kwamba hakuna tatizo. Nikaenda kulala na kwakua ndugu yangu alichelewa kurudi, yule mama akaniambia kesho ananiaga na niondoke.

Mie huyooo nikaingia jikoni, nikawapanga kuku wao pale nami nikaweka tandiko nikalala. Kesho yake palipokucha nikawahi kuamka asubuhi nikijua leo ninaagwa, basi nikakamata jogoo (kama desturi yetu kule kijijini tunapo muaga mgeni) nikamchinja na nikamuweka kwenye beseni nikisubiri wenyeji wangu waamke wanipikie kuku ili nile niondoke.

Lahaula! Kilicho tokea baada ya wenyeji wangu kuamka ni siri yangu wakuu. Ila kumbe watu wa Daslam mnaroho mbaya sana wallah, na hamtokaa mnione tena ndio mtajuta..🤨😑
 
Huyu jamaa ni ndugu yangu wa karibu kabisa. Yaani ni mjukuu wa shemejiyake na binam wa mamaangu wa kambo.....
Ni siku ya tatu sasa tangu nifike hapa mjini, baada ya kuuza ng'ombe nikaona sio mbaya nikaosha kidogo macho na ning'arishe ngozi kwa maji ya mwambao....
Sasa nilifikia kwa huyu ndugu yangu wa karibu kabisa. Kwakweli walinikaribisha uzuri na sote tulifurahi na kukumbushana habari za majirani wa kule kijijini, sikuhiyo walinitandikia jikoni na nikalala bila tatizo hadi ikawa asubuhi. Nilipo amka nikakuta sebleni wameweka chai mezani na kamkate kamoja, mie nikakakata vipande viwili nikaloweka kwenye chai nika kakula kakaisha. Kwanza chai yenyewe niliona niweke kwenye bakuli la kunawia na ikaishia humo, maana tuvikombe niliona twa watoto..... kisha nikaondoka nikaenda kwenye genge la jirani nikanunua viazi ili nikazie maana nilikua sijashiba.
Mchana nilipo rudi, nikakuta ugali umepikwa kidogo kama kilo mbili tu, mie nikaula ukaisha na ile mboga nikamaliza yeto hadi mchuzi nikaunywa.
Sasa nilipo rudi jioni nikawekewa kikao na mke wa ndugu yangu kwamba nina tabia mbaya, nami nikamuuliza "tabia gani"?? Akajibu kwamba sifai kukaa kwake, basi nikasema kwamba hakuna tatizo. Nikaenda kulala na kwakua ndugu yangu alichelewa kurudi, yule mama akaniambia kesho ananiaga na niondoke.
Mie huyooo nikaingia jikoni, nikawapanga kuku wao pale nami nikaweka tandiko nikalala. Kesho yake palipokucha nikawahi kuamka asubuhi nikijua leo ninaagwa, basi nikakamata jogoo (kama desturi yetu kule kijijini tunapo muaga mgeni) nikamchinja na nikamuweka kwenye beseni nikisubiri wenyeji wangu waamke wanipikie kuku ili nile niondoke....
Lahaula.... kilicho tokea baada ya wenyeji wangu kuamka ni siri yangu wakuu....
Ila kumbe watu wa Daslam mnaroho mbaya sana wallah, na hamtokaa mnione tena ndio mtajuta..[emoji2955][emoji58]
Hapo mwisho imebidi nicheke, sasa wajute kwa lipi!?
 
basi nikakamata jogoo (kama desturi yetu kule kijijini tunapo muaga mgeni) nikamchinja na nikamuweka kwenye beseni nikisubiri wenyeji wangu waamke wanipikie kuku ili nile niondoke.


Wewe ulichokoza kiranga, ulistahili
Kufurushwa 🤣🤣
 
Huyu jamaa ni ndugu yangu wa karibu kabisa. Yaani ni mjukuu wa shemeji yake na binamu wa mamaangu wa kambo.

Ni siku ya tatu sasa tangu nifike hapa mjini, baada ya kuuza ng'ombe nikaona sio mbaya nikaosha kidogo macho na ning'arishe ngozi kwa maji ya mwambao.

Sasa nilifikia kwa huyu ndugu yangu wa karibu kabisa. Kwakweli walinikaribisha uzuri na sote tulifurahi na kukumbushana habari za majirani wa kule kijijini, siku hiyo walinitandikia jikoni na nikalala bila tatizo hadi ikawa asubuhi.

Nilipo amka nikakuta sebleni wameweka chai mezani na kamkate kamoja, mie nikakakata vipande viwili nikaloweka kwenye chai nika kakula kakaisha. Kwanza chai yenyewe niliona niweke kwenye bakuli la kunawia na ikaishia humo, maana tuvikombe niliona twa watoto.

Kisha nikaondoka nikaenda kwenye genge la jirani nikanunua viazi ili nikazie maana nilikua sijashiba.

Mchana nilipo rudi, nikakuta ugali umepikwa kidogo kama kilo mbili tu, mie nikaula ukaisha na ile mboga nikamaliza yote hadi mchuzi nikaunywa.

Sasa nilipo rudi jioni nikawekewa kikao na mke wa ndugu yangu kwamba nina tabia mbaya, nami nikamuuliza "tabia gani"? Akajibu kwamba sifai kukaa kwake, basi nikasema kwamba hakuna tatizo. Nikaenda kulala na kwakua ndugu yangu alichelewa kurudi, yule mama akaniambia kesho ananiaga na niondoke.

Mie huyooo nikaingia jikoni, nikawapanga kuku wao pale nami nikaweka tandiko nikalala. Kesho yake palipokucha nikawahi kuamka asubuhi nikijua leo ninaagwa, basi nikakamata jogoo (kama desturi yetu kule kijijini tunapo muaga mgeni) nikamchinja na nikamuweka kwenye beseni nikisubiri wenyeji wangu waamke wanipikie kuku ili nile niondoke.

Lahaula! Kilicho tokea baada ya wenyeji wangu kuamka ni siri yangu wakuu. Ila kumbe watu wa Daslam mnaroho mbaya sana wallah, na hamtokaa mnione tena ndio mtajuta..🤨😑
😃😃😃😃 Wewe una vituko sana. Umeuza ng'ombe halafu unaenda kulala kwa ndugu!!! Tena jikoni!!!!
 
😃😃😃😃 Wewe una vituko sana. Umeuza ng'ombe halafu unaenda kulala kwa ndugu!!! Tena jikoni!!!!
Mkuu, kwani hela ni zangu ama zao??
Mie nimeuza ng'ombe, lakini nauli ya kurudia kijijini walitakiwa wanipe wao...😪
 
Kosa lako kusubiri upikiwe huyo kuku, kama ulimkamata, ukamchinja bila idhini ya wenyeji wako kwanini ulishindwa kumpika pia na kumla kisha uondoke zako bila kuaga??!!🤣🤣
Nilikua nasubiri waamke alafu mke wa ndugu yangu amchemshe anipe kwanza supu, ndipo ampike nimle kabla hawajanipa nauli niondoke..😪
 
Back
Top Bottom