Siyo mpox hiyo ?
View attachment 3202974
Mpox husambazwaje?
Mpox inaweza kusambazwa kuanzia wakati dalili zinaanza hadi vipele vipone kabisa na tabaka jipya la ngozi
lifanyizwe. Kirusi hicho kinaweza kusambazwa kutoka mtu hadi mtu kupitia mgusano wa karibu, mara nyingi
wa ngozi kwa ngozi, ikiwemo:
• Mgusano wa moja kwa moja na vipele vya mpox, makovu, au umajimaji fulani wa mwili kama vile mate,
au kamasi
• Mahusiano ya karibu kama vile ngono, kubusu au kukumbatiana
• Kugusa vitu (vikombe, sahani), nguo (mavazi, malazi, au taulo), na sehemu ambazo zimetumiwa na mtu aliye
na mpox lakini ambazo hazijasafishwa bado.
• Watu wajawazito walio na mpox wanaweza kusambaza kirusi hicho kwa fetasi wakati wa ujauzito au kwa
vitoto vichanga wakati wa ujauzito au baada ya kuzaliwa
Mpox HAISAMBAZWI kupitia mgusano wa kijuujuu kama vile unapokuwa
na watu ukifanya kazi ofisini, kwenda sokoni, au unapokuwa kwenye basi.
Unaweza kujilindaje?
• Epuka mgusano wa karibu, wa ngozi kwa ngozi na watu walio na vipele vinavyoonekana kama mpox.
• Usimbusu, kumkumbatia au kufanya ngono na mtu aliye na mpox.
• Epuka kugusa vitu na vifaa ambavyo mtu aliye na mpox ametumia, kama vile vyombo, malazi, au mavazi.
• Nawa mikono mara kwa mara kwa sabuni na maji au utumie kitakasa mikono kilicho na alkoholi.
Nikigusana na mpox, nifanye nini?
• Angalia dalili kwa siku 21 kuanzia mara ya mwisho ulipogusana
na mpox. Unaweza kuendelea kufanya shughuli zako za kawaida
za kila siku maadamu huna dalili au ishara za mpox.
• Ikiwa una vipele vipya au ambavyo huvielewi au dalili nyingine
za mpox,mwone daktari na upimwe mpox.
• Iwapo utaambukizwa mpox, kaa mbali na watu wengine kadiri
iwezekanavyo, funika vidonda vyako, na uvae barakoa unapokuwa
karibu na watu wengine hadi vipele vyako vitoweke kabisa,
Ni nani anayeweza kuugua vibaya?
Mpox inaweza kuwa hatari sana kwa watu fulani, kama vile:
• Watu ambao mfumo wao wa kingamaradhi ni dhaifu sana au walio na VVU (HIV) ambayo haijadhibitiwa
• Watoto wenye umri chini ya mwaka 1
• Watu walio na historia ya ugonjwa wa ukurutu (kizema)
• Watu ambao ni wajawazito
Iwapo wataugua mpox, huenda wakahitaji utunzaji wa ziada ili kuwasaidia kupata
Source : cdc.gov