Darasa: Maadhimisho ya leo ni ya Uhuru wa Tanzania ila kumbukumbu ndio ya Uhuru wa Tanganyika!

Haimake sense kwako kwasababu umekubali kupoteza historia yako.Jina ni utambulisho tu ila hapa hoja sio jina bali hilo jina linamtambulisha nani.kwasababu bila utambulisho maana yake hicho kitu hakipo.je ni kweli tanganyika haipo?
Tanganyika haipo kwasasa.
 
Tanganyika haipo kwasasa.
Sasa kama haipo kinachosherehekewa Leo ni kitu gani? CUF waliambiwa wanataka lumtejesha sultan Zanzibar,Leo sultan wa Oman ametuma mwakilishi wake shamba la Bibi. Kuna mwanajeashi mmoja amempiga mtangazaji wa TBC eti mwaka 1964 Sultan wa Zanzibar alikuwa Bargash.Nimeshangaa Sana.Bargash toka 1870s hadi 1964 bado ni sultan wa Zanzibar.
 

Aisee. Kimataifa, tarehe 26 Aprili ndiyo hutambulika rasmi Kama Tanzania’s National Day. Watanzania wanaofanya kazi kwenye taasisi za UN, AU, ACP, n.k. hupewa ruhusa ya mapumziko siku hiyo. Tarehe 9 Desemba haijulikani.
 
Aisee. Kimataifa, tarehe 26 Aprili ndiyo hutambulika rasmi Kama Tanzania’s National Day. Watanzania wanaofanya kazi kwenye taasisi za UN, AU, ACP, n.k. hupewa ruhusa ya mapumziko siku hiyo. Tarehe 9 Desemba haijulikani.
Sii kweli, Tanzania National Day, ni tarehe 9 Desemba, kila mwaka na inatambulika dunia nzima. Zaidi ya national day, kila nchi inazo sikukuu zake za kitaifa na zinaheshimika kimataifa hadi UN. UN haina mamlaka ya kusema inatambua, au haitambui siku fulani, bali ni kwa kumwandikia, NV, Katibu Mkuu, na kumweleza Tanzania imeamua Tarehe 8/4 ya kila mwaka, ni sikuu ya kitaifa kwa Tanzania, na hana mamlaka ya kusema hatambui. Mfano Uingereza, Birthday ya Queen ni public holiday, sio tuu England, bali UK, yote na dominions zake ikiwemo, Canada, Australia New Zealand, na kwa nchi zote za Jumuiya ya Madola, na kwenye balozi zao zote ni public holiday.
P
 
Mkuu kwa hiyo leo tunasherehekea uhuru wa Tanzania (Tanganyika isiyokuwepo) alafu very soon next January tutasherehekea uhuru wa Zanzibar??
Si ndiyo?

Je, wewe unaona sawa tu??
Hapo ndipo siwaelewagi kabisa hawa watawala koko.
 
Rubbish
 
Kwa kweli Pascal Mayalla mnatukera wengine kwa kuikataa asili yetu. What is wrong with Tanganyika ?!

Nawe leo mkane Mzee Mayalla kwa kuwa tu una jina la kizungu leo .

Mbona wa Zanzibari hawasahau asili yao ?! what is wrong with Tanganyikans !!
 
Si kweli. Wewe unatoa ufafanuzi usiohitajika. Siku ya taifa ni moja tu. Tarehe 26 Aprili ndiyo tarehe iliyokubaliwa na pande mbili za muungano wa JMT na kuwasilishwa rasmi huko nje na Foreign kama National Day of the URT.
 
Mkuu kwa hiyo leo tunasherehekea uhuru wa Tanzania (Tanganyika isiyokuwepo) alafu very soon next January tutasherehekea uhuru wa Zanzibar??
Si ndiyo?

Je, wewe unaona sawa tu??
Yaani huyu jamaa anajifanya ana uwezo wa kutengeneza hoja kumbe hovyo tu.
Huyu angepewa URC au UDC, asingekuwa tofauti na makonda na sabaya

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Ni siku ya uhuru wa TANU wala sio Tanganyika, Mtanganyika gani yuko huru na Tanganyika yenyewe iko wapi?
Uhuru wanao wao TANU wala sio Watanganyika.
 

What's wrong with you Pascal Mayalla ..?

1. Ni kweli Mtoto akizaliwa hupewa jina...

2. Lakini ni kweli pia, mtu akifa huzikwa na jina lake na tunapomkumbuka (wengine hufanya mpaka ibada za kukumbuka wafu) kwa jina lake lilelile alilokufa na kuzikwa nalo...!

3. Ni uwendawazimu na ujinga uliopinduka kubadili jina kwenye kaburi la aliyekufa na kuzikwa. Wasiojua watajuaje kuwa hili kaburi ni la Pascal Mayalla...?

Hiki ndicho wanachofanya watawala hawa chini ya CCM....

Haieleweki wanajaribu kuficha nini kwa umma. Kwa sbb iko very clear kuwa, tarehe 9/12 kila mwaka ni kumbukumbu ya Uhuru wa nchi inayoitwa TANGANYIKA na siyo TANZANIA maana hiyo haipo na haikuwepo mwaka 1961....!


Kwa kifupi hujaeleweka na sijui kama utaeleweka hata ukiendelea kujitetea...!!
 
Iliyopata Uhuru ni Tanganyika. Na Tanganyika ipo japo kwa uzuzu wetu tu tunaikana.

Tanganyika ndiyo iliyoungana na Zanzibar na kuunda JMT.

WaZanzibari wameikumbatia Zanzibar yao, sisi tunaikana Tanganyika yetu. Tunasema eti Uhuru wa Tanzania bara. Mbona WaZanzibari hawasemi Mapinduzi ya Tanzania Visiwani?
 
Tanganyika pia si nchi yenu. Ilianzishwa na Uingereza baada ya kumpora Mjerumani makoloni yake baada ya vita ya kwanza ya dunia (WW1) na kuyagawanya. Kihistoria nyie hamna nchi, mna makabila. Tanganyika mnayoililia ilikuwa ni chini ya mfalme George na baadaye malkia Elizabeth wa Uingereza. Tanganyika ni nchi bandia na Tanzania ni nchi bandia. Nchi ya kweli ni Zanzibar kwa sababu kihistoria ilikuwepo kama nchi siyo makabila tuu.

Kwa muhtasari

1) Tanganyika - nchi bandia iliyoundwa na Mfalme wa Uingereza chini ya League of Nations mandate
2) Tanzania - nchi bandia iliyoundwa na Nyerere baada ya kuiuwa Tanganyika na kuivamia Zanzibar
3) Zanzibar - nchi halisi ambayo ipo kihistoria na inajulikana kihistoria
 
Mkuu Mti wa Muwese, The Palm Tree , huu ndio uelewa wa baadhi ya Watanzania, wewe ukiwemo, halafu mkiambiwa ukweli mna uwezo finyu wa uelewa, mnakasirika.

You are absolutely right, kumbukumbu ni za uhuru wa nchi iliyokuwa Tanganyika, lakini maadhimisho ni maadhimisho ya uhuru wa Tanzania!.

Kuna mambo mawili.
1. Kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika.
2. Maadhimisho ya Uhuru wa Tanzania ambayo hapo zamani ilikuwa Tanganyika.

Sasa najaribu kukuelewesha kwa kutumia kiwango cha chekechea, usipoelewa sasa, utanisamehe bure.

Mfano,
  1. Kuna binti mmoja anaitwa Binti Mti wa Muwese, kila siku yake ya kuzaliwa anaisherehekea kama kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya Binti Mti wa Muwese.
  2. Kila akisherehekea siku hiyo, ni sherehe za kukumbuka ile siku yake ya kuzaliwa, na anayesherehekea siku hiyo ni Binti wa Muwese.
  3. Ikatokea mimi Pasco Mayalla, nimempenda Binti Mti wa Muwese, nikamuoa, akabadili jina sasa haitwi tena Binti Mti wa Muwese, sasa anaitwa Mrs. Pasco Mayalla na nyumbani anaitwa Mama Junior, maana kanizalia kidume kinaitwa Pasco Junior.
  4. Siku ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Binti Mti wa Muwese, ila sherehe ni ya Mama Junior.
  5. Kumbukumbu ni ya kile kilichofanyika wakati kikifanyika, ni kumbukumbu ya kuzaliwa kale kachanga kalikoitwa Binti Mti wa Muwese, lakini sherehe, yaa birthday party, sio party ya binti Mti, ni party ya Mama Junior (Mrs Pasco)
Hivyo nchi iliyopata uhuru ile tarehe 9 Desemba 1961 ni Tanganyika, hivyo kumbukumbu ndio ya uhuru wa Tanganyika, lakini maadhimisho, sherehe, ni ya Tanzania, kwasababu yule Tanganyika amebadili jina na kuwa Tanzania Bara, kwa kifupi Tanzania.

P.
 
Umechemsha!! Umejivua nguo!! watoto fumbeni macho mtu mzima kajitupua!! Mayala umejitupua!!
Unaposema maadhimisho ya leo ni ya uhuru wa Tanzania na siyo wa Tanganyika je unaijua DHANA ya UHURU? Unaposema uhuru maana yake ni uhuru toka kwa utawala wa mkoloni! Je mkoloni mwingereza alikùwa anaitawaĺa Tanzania au Tanganyika? Kumbukizi pekee la Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililozaa Tanzania! Tanzania haiwezi kusherehekea siku ya uhuru maana haijawahi kutawaliwa na mkoloni yeyote!! Unless Mayala una maana yako ya uhuru iliyo tofauti na ile inayojulikana katika nchi zote zilizowahi kutawaliwa!! Narudia tena Mayala umetupua!!!
 
mayala akili zimekuruka! unalazimisha kuyatenganisha maneno kumbukumbu na maadhimisho wakati haya maneno kwenye muktadha/context ya siku husika yanakwenda pamoja na yanatumika pamoja yaani Maadhimisho ya kumbukumbu/ maadhimisho kwenye kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika!! Kwa bahati mbaya hujui kama unajitupua!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…