Daudi Ballali's Death

Daudi Ballali's Death

Status
Not open for further replies.
Kuna kitu kinaitwa hindsight bias. Sasa hivi kila mtu atajifanya alijua hii kitu lakini ukweli ni kwamba hatukujua.

Shukrani sana Invisible kwa hizi news na MKJJ kwa ile tungo yako ambayo Invisible ameamua kuitungua.

Kitendo cha Balali cha kuamua kufa na habari zote za ufisadi pale BoT ni cha aibu na kinazidi kuthibitisha kwamba sisi waafrika tuna matatizo makubwa kuliko tunavyojijua. Ingekuwa kwa wenzetu wangeshaandika lundo la vitabu kuhusu hii saga ikiwemo memoirs zake Balali.

Inaelekea bado tunaendelea kuamini kwamba njia peke ya kuendelea kuwa na ushawishi ni kuhakikisha kwamba wananchi hawana taarifa muhimu kuhusu yale tunayoyatenda. Ni aibu sana.

Mkuu nakubaliana nawewe na ktk hili kifo chake kinatakiwa kiwe chachu pia kwa watanzania kutaka kujua ukweli kuhusu yale madudu tunayoyasikia BoT.

Tungemuomba Rais JK aweze kutoa riport ya wakaguzi wa EPA au aruhusu uchunguzi ufanyike kwa kutumia waheshimiwa wabunge.

Otherwise hili ni pigo kubwa la maendeleo ya nchi yetu. Hapa ukweli wote unaelekea kuzimika. Shukrani kwa watuzi wa nyimbo mbali mbali ambazo zilikuwa zinatupelekeka ktk hili.
 
Nafikiri kuwe nashinikizo ya Kudai mwili uletwe otherwise...
ila hukawii kuambiwa nduguze wameomba azikwe huko huko.ukasikia wale wale wamesafiri kwenda kumzika and u'l never see even a single photo at the funeral.
 
kaka BALALI HAJAFA, wanakupiga changa la macho ili msahau kumdai aletwe ili atoe ushahidi KIKWETE WATANZANIA SIO WAJINGA

Hisia zako huenda zina chembe chembe ya ukweli ndani yake,

Inashangaza kwamba serikali siku zote imekaa kimya ikijidai mara mgonjwa kaenda kwa matibabu, mara hijui balali alipo, mara ni mtu huru, mara tuna mtafuta, na katika kuibukia kumtafuta ndo tuna ambiwa kafa, na anazikwa huko huko???

I smell something fishy!! what a coincidence?
 
Hisia zako huenda zina chembe chembe ya ukweli ndani yake,

Inashangaza kwamba serikali siku zote imekaa kimya ikijidai mara mgonjwa kaenda kwa matibabu, mara hijui balali alipo, mara ni mtu huru, mara tuna mtafuta, na katika kuibukia kumtafuta ndo tuna ambiwa kafa, na anazikwa huko huko???

I smell something fishy!! what a coincidence?

MAFISADI wanashangilia, watanzania wanalia. Hapa kama kuna ka mchezo fulani kanafanyika. Hile tume inaelekea kumaliza muda wake, na main actor amefariki. SINEMA itakuwa imefika mwisho.
 
SINEMA itakuwa imefika mwisho.
Kakudanganya nani? Huu ni mwanzo wa sinema yenyewe! Ni suala la muda tu...

Halafu wengine wananidai ushahidi kuwa Ballali kafa, dah... Nadhani la kufanya ni kuisihi serikali mwili wa marehemu urejeshwe nchini ili watu waweze kufanya kama 'Tomaso'.
 
Kama ni kweli kafariki kimwili basi Wadanganyika wataendelea kuitafuta roho yake hadi pale ufisadi aliotufanyia utakaposafishwa. Naamini Familia yake, Ndugu na jamaa wataendelea kufaidi kwa kile alichotutenda hivyo dhambi hii haitafutika kwenye uso wa Dunia. Mafisadi wenzake naamini watasheherekea sana kwani wanaamini sehemu kubwa ya ushahidi itakuwa imepotea na kwenye msiba watampamba na kumsifu sana..., alikuwa mwenzetu...., tulimpenda sana...., bwana ametoa na bwana ametwaa.....!!!!!!!

Binafsi naona kama kuna kamchezo fulani kanaendlea hapa.. Mi siamini kama Kweli Balali amekufa hadi siku nitaona maiti yake ikiletwa Tanzania na Kuzikwa, Nasikia eti amezikwa Marekani Kwa nini?? Naona hapa kuna changa la macho
 
Poleni na kazi wana JF, Kazi mliyoifanya mpaka kutoa habari hii uvunguni mwa kitanda cha ikulu sio mchezo..... bIG UPU!!!!
TUNACHOWEZA KUSEMA NI KWAMBA SEREKALI IFANYE JUU CHINI IREJESHE MWILI WA HUYU KUNGWI WA MAFISADI hata tuuone tuu tuweze kuamini kama Tomaso.
Sasa na huyu msukuma wa vijisenti nadhani ndugu yangu mwanakijiji tusubiri tuu taarifa
 
...wamemuuuwa Balali...kosa Kubwa Alilotufanyia Watanzania Ni Kufa Kabla Hajaweka Ukweli Wazi!!!!!!!!!!
 
Tuandamane!
Nadhani mwenye jukumu la kuurudisha mwili wa BALALI nyumbani kwa mazishi ni familia yake maana serikali ilishamfukuza kazi na alikuwa raia huru(Salva Rwemamu,2008).

Ni mtuhumiwa mkuu na ni namba one, kwa kawaida bado yuko mikononi mwa serikali, inapaswa imrudishe laa sivyo watanzania wote tutaituhumu serikali kwa kumuua
 
Kakudanganya nani? Huu ni mwanzo wa sinema yenyewe! Ni suala la muda tu...

Halafu wengine wananidai ushahidi kuwa Ballali kafa, dah... Nadhani la kufanya ni kuisihi serikali mwili wa marehemu urejeshwe nchini ili watu waweze kufanya kama 'Tomaso'.


Mkuu mimi siko kwako kabisa katika kuudai mwili, mi nalia na Serikali kwanza tunataka mwili ufanyiwe uchunguzi ili tujue kama kafa kifo cha kawaida sbb hata kama ni mtuhimiwa kunahaki ya uchunguzi kufanyika na tujue nini chanzo chas kifa na hata kama kauwawa basi uchunguzi ufanyike na kesi ifunguliwe

Bado naendelea kusema BALABI HAJAFA
 
Itabidi tumuulize very seriously Salva Rweyemamu alikuwa anamaanisha nini kuwa hawamtafuti Balali! Hivi alikuwa anamsemea JK! Kweli kazi tunayo na hii senema! Mimi hata nikiona mwili wa Balali naweza kuamini yawezekana tunaonyeshwa Kinyago!! Kifo cha Balali ni hatari zaidi kwa Mafisadi kwa sababu itabidi sasa tuwapige mawe!! Kama sheria itashindwa kufanya kazi kwa kweli tutafika mahali tutawapiga mawe!!
 
Balali kama amekufa naamini wamemuua... Na kama amekufa picha imeisha kwani stelingi akifa picha nayo inaisha... Naamini usanii wa nchi yetu ndio mwisho wa uchunguzi...

Invisible: naona bado una imani kubwa sana kwamba picha ndio kwanza imeanza.. najua upo makini lakini nakuhakikishia usanii wa nchi hii ni kiboko wee tulia uone.. kwani miezi sita ya tume sii inafika tuu muda sii mrefu
 
Ni jioni iliyogubikwa na utulivu, ambao katika maeneo haya ya Kinondoni Makaburini, haujapata kutokea kwa siku nyingi. Kelele za wapiga debe za Posta wa haraka!!!! zilizoeleka kusikika, leo hii hazipo.

Kwa ufupi ni kwamba hata daladala za Posta-M/nyamala au kinyume chake leo hazipiti katika njia hii. Japokuwa sina uhakika kama kuna askari wa Traffic anayezielekeza njia mbadala.

Waombolezaji ni wengi sana wenye nyuso zenye vionjo na hisia tofauti kulingana na jinsi walivyoguswa na msiba huu ambao mahudhurio yake hayajashuhudiwa katika siku za hivi karibuni.

Licha ya wingi wa waombolezaji, ni sauti moja tu inayosikika katika eneo hili.
"Sasa tukio linalofuata ni kuweka mchanga kwenye kaburi la marehemu ambapo wataanza viongozi mashuhuri" Ilisikika sauti ya MC wa mazishi hayo ambayo inaonekana ni ya mtu mkubwa sana kama siyo Kigogo (simaanishi lugha ya kabila fulani).

Licha ya kuwa si mhudhuriaji mzuri wa misiba ambayo haitokei mtaani kwetu Kwa Mnyamani na maeneo ya jirani, lakini kwa msiba huu nimeshawishika kuahirisha safari yangu ya kwenda kwenye ufukwe wa Salender Bridge kuokota Simbi, ili niweze kushuhudia namna misiba ya Watu Maarufu kama huu inavyofanyika.

Najitahidi kupenya taratibu ili japo nipate fursa kushuhudia kinachofanyika pale kaburini lakini nashtuka kukutana na kundi la watu waliyovaa kaunda suti na miwani myeusi waliotanda kama mita Ishirini kutoka lilipo kaburi ambao badala ya kutazama kwenye tukio, wao wameelekea walipo watu.

Wakati, nashangaa na kutafakari nikahisi wote wananiangalia labda kutokana na mavazi niliyovaa, Nikajisemea mwenyewe, "Hata hapa panatosha" kisha nikatulia.

"Sasa ni zamu ya Ndugu jamaa na marafiki wa Marehemu" Ilisikika tena sauti ya yule MC, ambayo kwa sasa ilikuwa ikisika kwa karibu zaidi kutokana na umbali niliyokuwepo.

"Atakayeanza ni Chiefmtz, rafiki wa damu wa marehemu" MC aliendelea.
Watu wote waliokuwa karibu walikuwa wakiangalia huku na kule kwa shauku ya kumuona huyu rafiki wa damu wa marehemu, aliyepewa heshima ya kuweka mchanga.

Kwa utulivu wa kimsibamsiba, akatokea Bwana mmoja akipenya kati ya waombolezaji na kuelekea lilipo kaburi huku akisindikizwa na macho ya waombolezaji. Mmoja wa vijana wenye suti nyeupe, kati ya vijana waliokuwa waliokuwa wakitoa huduma pale, alikuwa ameshikilia Koleo lenye mchanga akimsubiri Chiefmtz achukue mchanga kidogo kama ilivyozoeleka, kwa ajili ya kutupia kaburini.

Kwa utulivu, huku akifuta machozi kwa kitambaa cha mkononi, Bw, yule alichukua lile koleo alilokuwa ameshika yule kijana na kumwaga ule mchanga wote kaburini.

Kama mtu asiyeamini alichokiona akasema kwa sauti kavu na ya kujiamini,

" Babaangu Balali! Hivi ni kweli umekufa aati!! Nimekumwagia beleshi zima la
mchanga ili uamke uturudishie hela zetu za EPA, mbona husikii"

Huku waombolezaji wakiwa wamepigwa butwaa na yaliyokuwa yakijiri, yule Bwana akachota mchanga mwingine, ukiwa mwingi zaidi wenye mabongemabonge na kuumwaga tena kwa nguvu zaidi na kutoa kishindo "Puuuuuuu!!!!!!!! huku akiendelea kusema

"Nakumwagia mchanga mwingine tena, yaani unajifanya umekufa kabla
hujaturudishia hela zetu za EPA"

Ikasikika sauti ya MC, "Mtoeni huyo, atakuwa amechanganyikiwa!!!!!"

Wale vijana wenye suti wakamuondoa kwa haraka ili kupisha wengine.

Kwa niliyoyaona, nikajikuta huku nikiondoka, naguna "He!!! KUMBE NI BALALI YULE ALIYESHIRIKIANA NA WENZAKE KUTUPORA HELA ZETU? Nikajilaumu sana kwa kuacha shughuli zangu. Hata hivyo nikaishia kusema

BWANA AMETWAA!!!!!
 
jama hii ni changa la macho, wanatuweka sawa kabla ya tume kutoa taarifa ya uchunguzi wake (kumbukeni ukamilifu wa uchunguzi uko ukingoni) KIKWETE UNAHARIBU NCHI.... BALALI HAJAFA
 
Itabidi tumuulize very seriously Salva Rweyemamu alikuwa anamaanisha nini kuwa hawamtafuti Balali! Hivi alikuwa anamsemea JK! Kweli kazi tunayo na hii senema! Mimi hata nikiona mwili wa Balali naweza kuamini yawezekana tunaonyeshwa Kinyago!! Kifo cha Balali ni hatari zaidi kwa Mafisadi kwa sababu itabidi sasa tuwapige mawe!! Kama sheria itashindwa kufanya kazi kwa kweli tutafika mahali tutawapiga mawe!!

Unajua uvumilivu siku zote una mwisho.. Hata paka ukimchezea tuu akiona anazidiwa atajihami kwa kukukwaruza ikibidi kukung'ata. Tanzania we are in that stage now. Rweyemamu anaujua ukweli. JK anajua kila kitu na hakuwahi kuongelea chochote maana yake nini.. Yupo Busy na Sulivan ambayo sioni faida yake kama mafisadi wakishaiba wanakimbia na kujifanya wamekufa.. Kwangu mimi ni mchezo wa kitoto.. Kwa nini raisi wa nchi asimami kama Rais kwa kusema na kukemea ufisadi? sio kwa kwa maneno yake ya kutuchekea bali kwa action.. Mambo ya EPA ndio picha imeungua hivyo Maumivu kwa watanzania
 
Mkuu mimi siko kwako kabisa katika kuudai mwili, mi nalia na Serikali kwanza tunataka mwili ufanyiwe uchunguzi ili tujue kama kafa kifo cha kawaida sbb hata kama ni mtuhimiwa kunahaki ya uchunguzi kufanyika na tujue nini chanzo chas kifa na hata kama kauwawa basi uchunguzi ufanyike na kesi ifunguliwe

Bado naendelea kusema BALABI HAJAFA
Sasa mkuu kama hudai mwili, uchunguzi utafanyika kwenye nini kama sio mwili?
 
I feel sorry for his relatives, I give congrats to all the EPA beneficiaries.Possibly, everything has now covered!

I have a feeling that this was almost expected. This is what Mwanyika and his fellows fisads wanted to ease there 'doctoring' of the so called EPA 'investigation'. Tangu lini fisadi akamchunguza fisadi?

The continual existence of Ballali was the biggest threat to 'sisiem' and the JK government. Ballali has most likely been 'assassinated' to cover the whole EPA scandal.

SMU
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom