Daudi Ballali's Death

Daudi Ballali's Death

Status
Not open for further replies.
ee mola inusuru nyumba yetu Tanzania maana ufa umezidi na tunakaribia sasa kujenga ukuta.
R.I.P Ballali
Najua atakuwa ameacha wosia kuhusu ufisadi wa EPA, huo ni muhimu kwetu tulio hai.
 
Niccolò di Bernardo dei Machiavelli (May 3, 1469 – June 21, 1527) ? RIP if its true...hii mafia hatari.
 
Kibunango.
Are you serious kwamba Mungu amlaze mahali pema au ni mazoea tu?
 
Mkuu, kuna zaidi usiyoyajua kuhusu hili. Mpe heshima yake marehemu na kama ni kuwambia watanzania NAKUHAKIKISHIA kawambia... Ni suala la muda tu!

YES, nakwambia,,, alisema. Kwa maandishi? Sijui!


Kumuua Balali sio mwisho wake, sanasana naona wanazidiharibu tuu, maana yatakuja semwa tuu na ushahidi utatolewa, je hapo wataua wangapi???? kumuua ni kuzidi kuprovoke watanzania tuu... kwa kumuua BALALI MMEKANYAGA PABAYA
 
Tayari yameshatimia wengi walishatabiri watamtoa kafara tumeshuhudia ushahidi wamesha upoteza tena MAFISADI....ndugu zangu tuungane kuwakana hawa mafisadi wana roho mbaya tayari wamesha mrestisha in peace....Mungu ailaze mahali pema roho yake.....AMINA
R.I.P BALALI na wote
 
Jamamni kuna thread imeshaanzishwa na Invisible juu ya hili na nyie mnaanzisha nyingine hii inafanya kusiwe na mtirirko mzuri wa mawazo. Ungeileta tua kama post kati ile thread na mchango wako ungeonekana na ungekuwa na Tija
 
Eti Balali amekufa? Invisible angalia tena hizo source mkuu wangu, jina lako zito sana mkuu! Angalia nia na madhumuni ya waliokupa hizo dataz mkuu!

Maana majuzi kuna mahali alionekana akibadilisha vitambulisho vya zamani vyenye jina la Balali na kuwa jina jipya la ............!, Mkuu wangu najua kuwa wewe ni kichwa, ila kwenye hili umetapeliwa na mafisadi, unajua kuwa wana sura nyingi sana!

Jina jipya ndio The Late Dr Daudi Balali????
Any way RIP The Late .......
 
Kwani haiwezekani ikawa amefariki baada ya "kuugua kwa muda mrefu", badala ya kuwa ameuawa na mafisadi au ma-anti-mafisadi??

Siku hizi Wabongo wengi na hata viongozi na watu mashuhuri ni kawaida kufariki kwa 'ugonjwa wa kuugua kwa muda mrefu'...
 
On the other hand... kuna kiongozi wa Tanzania anayekufa kwa kuwa siku yake imefika?
 
Nimekuwa mzito mno leo kuweza kuchangia hoja hii ya kufariki dunia kwa mtu ambaye tulimhitaji kwa hamu atusaidie sisi watanzania tujue nani hasa mhusika wa wizi wa mabilioni ya wavuja jasho, hii ni kutokana na taarifa kama hizi zilitolewa kumhusu Andrew Chenge sipendi kumwita Mh. Chenge kwasababu hana heshima yoyote kwetu. Lakini kila linapotoke jambo yatupasa kutoa mchango wetu. Mchango wangu kuhusu "kifo" cha Daudi Ballali kimenishitua sana na kama ni kweli kimetokea sisi Watanzania tungependa kuiasa serikali kuurejesha mwili wake ili tupate uhakika kuliko kuifanya serikali kama inataka kufanya usanii. Hata kama wataonyesha mwili uko katika jeneza sitashawishika kuamini hivyo maana tuhuma zinazomkabili ni kubwa na ili kuwa huru kwa namna fulani usanii kama huo unaweza kufanyika kama vile picha sinema katika runinga.

Binadamu hatuna ubavu mbele ya mavuno ya Mungu sote tutavunwa tu siku ikifika. Ballali alikuwa ni mtu muhimu kwetu wanyonge ambaye angeweza kutoa picha halisi ya nini maana ya viapo ambavyo mawaziri huapa na kusema ......."....na kwa vyovyote sitaweza kutoa siri za baraza la mawaziri, Ee mwenyezi Mungu nisaidie" Siri hizi naye Ballali aliapa hivyo na amekufa akiwa amefumba mdomo kwa kiapo chake ndani akiwa na siri nzito.
Ipo siku kuna waziri mmoja atageuka Yuda Skariote atatoa siri zote hadharani.
 
Duh!! Hii ni mchanga wa macho tu...jamaa ana mambo mazito ambayo wakimuachia upenyo aseme...hakuna atakayepona na Tanzania nzima tutaishi kwa kuogopana, kutoaminiana tena ..so hii imekaa ki usalama wa taifa zaidi.. kama kweli amekufa basi watakua wame msumu tu...kama sio basi hii nimoja ya mbinu ya ku save taifa.. oK tusubiri tuone
 
Naungana Na Wewe Nyangumi Siwezi Kumchagulia Mungu Mahali Pa Kumweka Yeye Balali Ndiye Alikuwa Na Uwezo Wa Ku Ditamini Wapi Pa Kuwekwa Eee Mola Mweke Alipo Mobutu Na Hitler,i Dont Have Sympas With Satanic Argents Who Has Been Sent By Devil To Spoil Our Economy.
 
Lakini nimesoma kwenye Tanzania Daima la leo linadai habari ni zakuthibitika Balali hatunae tena ila taarifa za kifo zimewekwa siri na atazikwa Ijumaa na serikali itatoa taarifa rasmi leo.Hawa jamaa wanadai wamepata DATA saa 4 usiku wa jana kwa watu wa karibu na Balali na kafia nyumbani kwake Washington toka Ijumaa...
 
But Also As Invisible Has Said Is The Matter Of Time The Issue Will Be Out,iam Waiting That Day When I Will Read The Whole Story,
 
Kwa hiyo ndugu wa Gavana huyo wa zamani wandai wamesha toa taarifa serikalini kwa hiyo kwa more news ni leo serikali itatoa tamko rasmi..
....naona MWANA KIJIJI alikuwa na full details toka Balali afe Ijumaa ndo maana alikuwa anatupa news.
 
Kama kweli Balalli amefariki sasa kufichaficha kifo chake kuna faida gani? Si watangaze tu, unless wamemkolimba wenyewe?
 
Death only conquers the dead and leaves the living in woes!
For Balali to die at this moment it leaves so many questions unanswered, than if he'd disappered.
Mungu Ibariki Tanzania.....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom