David Kafulila: Ajabu ni ipi Tanzania yenye ziada ya umeme kununua umeme?

David Kafulila: Ajabu ni ipi Tanzania yenye ziada ya umeme kununua umeme?

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila hivi ndivyo alivyoandika baada ya baadhi ya Watanzania kushangaa kauli ya Rais Samia Suluhu kuhusu Tanzània kununua Umeme nje ya nchi, Ethiopia.

Mkurugenzi Kafulila anasema pamoja na kwamba nchi kubwa na tajiri duniani kama Marekani ( USA ), Ujerumani, Norway, Sweden au Australia wanaumeme mwingi kiasi Cha kuuza nje ya nchi zao bado na wao kwa Upande mwingine wa nchi zao wananunua umeme kutoka nje ya nchi zao.

Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Kafulila anasema kuwa baadhi ya maeneo ya nchi yetu hasa maeneo ya mipakani gharama ya kuzalisha, kusafirisha na kufikisha umeme maeneo hayo ni kubwa pengine kuliko gharama ya kuuvuta na kuununua umeme toka nchi za jirani.

Kafulila anadanganya, kazi yake ni kupiga debe sio kusimama katika ukweli.

Katika nadhariia ya umeme power loss ni kitu kisichokwepeka na kinachokubalika ni sawa na Lori linalotembea kuna vyuma na parts vinasagika hivyo baada ya muda huwa vinabadilishwa. Hivyo mwenye gari anapochaji gharama za uchukuzi wa miizigo anaweka pia gharama za uchakavu ili baadae aweze kununua speak pale zitakapokuwa zimechakaa.

Umeme unaposafirishwa hata ndani ya wilaya moja au toka nyumba moja kwenda nyumba nyingine kuna power loss inatokea ambayo kitaalamu ni ( I squared times R). Ni kweli jinsi umbali unavyoongezeka ndivyo power loss nayo inaongezeka lakini ni kwa kiasi kidogo sana.

Kukabiliana na hilo la power loss, umeme unapozalishwa hatua ya kwanza unapandishwa juu sana mfano kutoka 33 KV zilizozalishwa kwenda 220 KV kwa kutumia step up transformer kabla ya kusafirishwa; hivyo unasafirishwa katika very high voltage; kitendo hiki kinasababisha current( I) ipungue sana hivyo kushusha power loss kitaalamu ( kumbuka formula ya power loss kihesabu za umeme ni (I times I times R). Umeme ukifika unakoenda unashushwa voltage kwa kutumia step down transformer hadi kiwango kidogo cha voltage mfano 11 KV katika sub stations, nao unasafirishwa ndani ya mji hadi majumbani na kushushwa tena kwa kutumia step down transformer zilizoko katika nguzo za umeme ili kuwa 415 Volts. Kitendo cha kupunguza voltage hupandisha current ( I ). Hizi ndio technique zinazotumika kudhibiti power loss kitaalam.

Ndio maana miaka yote huko nyuma umeme wa kidatu ulisafirishwa hadi Mwanza, Mbeya na maeneo ya mipakani kama Tarime ambapo ni zaidi ya km 1300 lakini tulikuwa hatusikii hizi ngonjera za power loss. Jiulize kwa nini sasa Kafulila na wengine wanapigia kelele ngonjera za power loss.

Mfumo wa tarrif wa kutoza gharama za.matumizi ya umeme unazingatia gharama zote kuanzia uzalishaji, usafirishaji, usambazaji, matengenezo, uchakavu,. Pia gharama walizotozwa watumiaji zililingana. TANESCO tangu mwaka 1991 imekuwa ikikumbwa na ubadhirifu mbalimbali unaotokana na mikataba isiyozingafia maslahi ya nchi na hiyo ndiyo ilifanya gharama za umeme ziwe juu kulinganisha na nchi zingine

Kafulila aelewe hata kuutoa umeme toka kwenye nguzo hadi ofisini au nyumbani kwake kuna power loss pia. Ni kama nilivyoeleza juu kwa kutumia mfano wa gari ya mizigo inapobeba mizigo.

Kingine, umeme unapozalishwa toka vyanzo mbalimbali unachanganywa katika grid ya Taifa ni kama maji yanavyochanganyika na kuwa kitu kimoja kwa sababu dunia nzima umeme unazalishwa katika makundi matatu tu yanayoitwa kitaalamu three phases huwa zinakuwa labelled Red, blue & yellow phases. Sasa wanaposema tunauza umeme wa mpakani sio sahihi kwa sababu umeme unakuwa umechanganyika kama maji huwezi kuutenga kuwa huu ni umeme wa pangani na huu ni wa kidatu na huu ni wa Rusumo nk hivyo ninauza umeme wa Rusumo siuzi umeme wa kidatu.

Hivyo concept ya power loss inayotumiwa sasa ni vehicle tu ya kuhalalisha maamuzi mabovu na ni hoja mufilisi.
 
Vp ethiopia ambaye umeme wake umefika mpk TZ?
Ni mjinga?
Sasa kama wa Ethiopia umefika Namanga kwani sisi tuingie gharama kubwa kuutoa umeme Rufiji kwenda Namanga Tena. Kwanini wa kwetu tusiwapelekea Mozambique na Mombasa.
 
Umeme wa ziada tutauuza nchi jirani zilizo karibu kama tumekuwa tukiwauzia Kenya kupitia Tanga miaka yote. Hivyo, ndivyo uchumi unavyoenda.
Serikali yetu ya sasa haiko tayari kuachana na dhana ya kuwa tegemezi. Mawazo ya JPM na mwelekeo wa kujenga nchi isiyotegemea sana misaada imejithibitisha hapa kuwa na kundi linaloona ni bora kuendelea kupokea misaada sio kwenye umeme tu, lakini pia kwenye bajeti zetu za nchi.
Swali ni :
Je pesa zinazokusanywa kama kodi zinafanya kazi gani kama tunategemea wahisani kutoka nje?
Je umeme wa ziada tunaozalisha tutautumia wapi wakati hatuna miundombinu ya usafirishaji ulio bora kiasi cha kulazimika kununua kwa jirani ambapo ni bei rahisi ?

View: https://x.com/dr_dash250/status/1899544053043073071?t=C-HOd-vz8f4WNDGrAybDYg&s=19
 
Ulifika sababu ethiopia alikuwa anampelekea umeme mteja wake anaempa mahela mengi

Ethiopia kafikisha umeme namanga sababu anauuza nchi nyingii..

Hajaupeleka kwa ajili ya kuhudumia mkoa mmoja
Obviously Ethiopia kabla hawajafikisha umeme Kenya na hizo nchi nyingi zinazo wapa mahela mengi,waliifikia kwanza mikoa yao yote ya ndani, swali ni je! waliwezaje na sisi tumeshindwa?
 
Kafulila yupo sahihi.. ni ujinga kusafirisha umeme kutoka rufiji mpaka kagera. Maelfu ya kilometa.

Huku ukiwa kagera unaweza kununua umeme uganda ukafika kagera kwa urahisi maana pafupi sana
Huo wa Uganda unazalishwa karibu na ka Gera?!
 
Kwa hiyo Kenya inalipa transmission costs za kuutoa Ethiopia hadi Namanga (1200Km+) halafu iwauzie nyie kwa bei chee ya hasara?

Au umeme wa Ethiopia hauna transmission costs kama wa kwenu?
Acheni kukaza mafuvu. Mmeamka uchambuzi umefanyika na imeonekana kununua umeme wa Ethiopia ambao tayari upo Namanga ni rahisi zaidi kuliko kuusafirisha wa kwetu kutoka Rifiji hadi Arusha.

Hapo mnakaza mafuvu ya nini Sasa. South Afrika inanunua umeme kutoka Msumbuji lakini inauzwa umeme wake kwenda Namibia na Botswana.
 
Naona chawa wanatumia nguvu nyingi kujustify uupuzi wa nyumbu mwenzao.
 
Wewe ndo hujaenda Shule. Ethiopia umeme wanawauzia Kenya muda, upo hadi hapo Namanga upande wa Kenya, njia za kuusafirisha umeme kwenda Kenya zilishakuwepo. Hawajengi njia Kwa ajili yetu. Wana umeme wa ziada, sisi tunanunua hiyo ziada.

Mbona na sisi tunanunua umeme kutoka Uganda miaka mingi na tunauza umeme kwenda Mombasa miaka mingi.

Sasa tukiutumia huo uliopo Namanga tayari then wa kwetu tukaupeleka mikoa kusini na nchi zilizo jirani upande wa kusini tatizo lipo wapi?
Singing shule Hawa mnaenda kufanya nini ikiwa hata haya mambo madogo yanawashinda, yaani kuusafirisha umeme kutoka Ethiopia mpaka Arusha I’ve rahisi kuliko kuutoa Rufiji kwenda Arusha?

Then unaletwa ufafanuzi wa kipuuzi kabisa kwamba ujenzi wa miundombinu ni gharama kutoka Rufiji na kuona bora kununua kutoka Ethiopia! Stupid kabisa!

Na wewe umetoka nyumbani kwako kwa heshima ya baba kabisaaaa, lakini kichwani ndo pako hovyo namna hii!!!!
 
Tz hauchukulii umeme ethiopia

Tz tunachukulia umeme wa ethiopia Namanga kenya . Ambapo kuna substation ilijengwa wakati ethiopia anamuuzia umeme kenya.

Hivyo kutoka Namanga to Arusha ni pafupi sana
Jamani mbona huwa mnapokea vitu bila kutafakari? Hebu kwanza niambie logic ya kujenga Namanga substation ya umeme toka Ethiopia kwenda Kenya.

Ni sawa na kusema wasafiri wa basi toka Dar kwenda Tanga wakapate chakula pale Mombo!
 
Miaka yote ipi? Ethiopia imepata umeme mwingi wa ziada majuzi tu baada ya Bwawa lao kubwa lilitaka kuleta vita baina yao na Misri kuanza kuzalisha umeme. Hadi Sasa Hilo bwawa lao halijajaa to full capacity, ipo 78%. Siku ikijaa wanaweza kuwauzia hata South Afrika maana njia za kusafirisha ni hizi hizi zilizopo, siyo lazima wajenge njia mpya, wanaweza kupanga kwenye njia zetu zilizopo wakatulipa Kodi ya Pango.

Hata hizo njia zilizo ufikisha Namanga Nina uhakika ni za Shirika la umeme la Kenya.
Tuna shida kubwa sana, tuseme wako sahihi, miaka yote tunapata shida ya migao ya umeme nchi nzima hawakujua kuwa kuna umeme wa kununua Ethiopia?
 
Kafulila yupo sahihi.. ni ujinga kusafirisha umeme kutoka rufiji mpaka kagera. Maelfu ya kilometa.

Huku ukiwa kagera unaweza kununua umeme uganda ukafika kagera kwa urahisi maana pafupi sana
Kama ni gharama ya mara moja tu ya kuweka miundombinu kutoka Rufiji hadi Kagera wala sio ujinga in the long run hizo pesa zitafidiwa baada ya muda fulani.
Utaona ni ujanja kununua nchi jirani kama unaangalia leo tu ila miaka ya baadae hao wanaowauzia wakigoma kuwauzia umeme kwa sababu zao binafsi utafanyaje?
 
Jamani mbona huwa mnapokea vitu bila kutafakari? Hebu kwanza niambie logic ya kujenga Namanga substation ya umeme toka Ethiopia kwenda Kenya.

Ni sawa na kusema wasafiri wa basi toka Dar kwenda Tanga wakapate chakula pale Mombo!
Ethiopia anauza umeme nchi nyingi.. hivyo substation kaziweka sehemu tofaut tofaut ambazo ni centre ya kufikia wateja wake wengi..

Ethiopia yeye alishaamua kwamba kuuza umeme ni biashara yake.. ndio maana kajenga miradi ya kuzalisha umeme mingi.. na pia kajenga transmission lines nyingi
 
Umeme wa ziada tutauuza nchi jirani zilizo karibu kama tumekuwa tukiwauzia Kenya kupitia Tanga miaka yote. Hivyo, ndivyo uchumi unavyoenda.
Nadhani uchumi wa Tanzania ndio unavyoenda kienyeji hivyo. Ziada hutafutiwa ufumbuzi baada ya tosheleza mahitaji ya ndani, unaanzaje kuwaza kuuza wakati hujakamilisha miundombinu yote ya usambazaji? Ukwepe kuwekeza makusudi kwa kuogopa gharama ukitegemea uhitaji wa jirani? Akijitosheleza utaufanya nini umeme unaozidi mahitaji yako? 😲
 
Ethiopia anauza umeme nchi nyingi.. hivyo substation kaziweka sehemu tofaut tofaut ambazo ni centre ya kufikia wateja wake wengi..

Ethiopia yeye alishaamua kwamba kuuza umeme ni biashara yake.. ndio maana kajenga miradi ya kuzalisha umeme mingi.. na pia kajenga transmission lines nyingi
Kwa hiyo Ethiopia alijenga sub-station ya Namanga hesabu zake ilikuwa kutuuzia sisi Tanzania? Sasa huoni kama ni hivyo mvuto wa kununua umeme ni mkakati wake zaidi ya kuwa mkakati wetu? Kwamba atakuwa anafanya kila njia ili tununue, pamoja na kuwapa watu wetu kitu kidogo wapitishe hilo? Hiyo tunaita "red flag" ya rushwa!
 
Kama ni gharama ya mara moja tu ya kuweka miundombinu kutoka Rufiji hadi Kagera wala sio ujinga in the long run hizo pesa zitafidiwa baada ya muda fulani.
Utaona ni ujanja kununua nchi jirani kama unaangalia leo tu ila miaka ya baadae hao wanaowauzia wakigoma kuwauzia umeme kwa sababu zao binafsi utafanyaje?
Angalia suala na kuuziana umeme kati ya USA na Canada. Tutauziana umeme na Rwanda siku nyingine mnajikuta mnazipiga huko DRC, Tanzania upande wa DRC na Rwanda upande wa M23. Mnaanza kukatiana umeme

Why would our Country allow another Country to supply us with electricity, even for a small area? Who made these decisions, and why? And can you imagine Canada stooping so low as to use ELECTRICITY, that so affects the life of innocent people, as a bargaining chip and threat?" Trump vented on his Truth Social app.

Canada inauza umeme kwa kaya karibu milioni 1.5 huko USA katika miji ya Minnesota, Michigan na New York.
 
Back
Top Bottom