Tatizo la vijana wa Tanzania wakisifu wanasifu mpaka kupitiliza, mpaka unajiuliza kunanini? Hivi kafulila kazaliwa leo Tanzania?Ndugu zangu Watanzania,
Mheshimiwa David Kafulila Ameamsha hisia, kuwagusa waheshimiwa wabunge na kuwarejesha mbali sana kihisia. Chuma Kafulila kaliteka Bunge, kalitetemesha na kalitikisa kwelikweli. Hii ni baada ya kutambulishwa Bungeni kama Mkurugenzi wa PPP na Mheshimiwa Speaker Dkt Tulia Acksoni Mwansasu.
Ambapo Bunge zima na wabunge wote na kwa Umoja wao wamempatia heshima kubwa na ya kipekee sana utafikiri utambulisho wa Mfalme wa Uingereza ndani ya Bunge. Ambapo imeshuhudiwa meza zoootee za waheshimiwa Wabunge zikilindima kwa kishindoo cha makofi ya kumpigia na kumpatia heshima ya kipekee Mheshimiwa Kafulila.
Bila shaka waheshimiwa wabunge wote bado wana kumbukumbu vichwani mwao juu ya alama alizoziacha za kizalendo, alizoziacha mzalendo huyu na mchapakazi aliyetukuka wakati wa ubunge wake 2010-2015.ambapo ni yeye amewahi kuweka historia ya kulifanya Bunge likafanya na kuendelea na shughuli zake mpaka saa Tano usiku katika Historia ya Bunge letu wakati wa sakata la Escrow.
Imeonyesha bunge zima na waheshimiwa wabunge wote wana kiu kubwa sana na kumhitaji Mheshimiwa Kafulila ndani ya Bunge, wanatambua uwezo wake, mchango wake na sauti yake kuwa bado inahitajika sana Bungeni wanaona ni kama kuna kitu kimepungua Bungeni kwa kutokuwepo kwa Mwamba huyu wa kigoma David Kafulila.
Waheshimiwa wabunge wanaona kuwa mtu huyu asiye na makandokando, Mzalendo wa dhati, mpole, mtulivu, makini, jasiri, shupavu, hodari, Madhubuti, imara, mnyenyekevu na mwenye misimamo ya dhati katika kutetea Taifa letu bado mchango wake unahitajika ndani ya Bunge letu.
Waheshimiwa wabunge wanaona kuna kazi Mheshimiwa Kafulila anatakiwa akasaidiane nao ndani ya Bunge ndio sababu ya heshima kubwa walioweza kumpatia,ndio sababu ya mapokezi mazito walioweza mpatia,ndio sababu ya kuguswa kwa wabunge wengi baada ya utambulisho wake, ndio sababu ya kumshangilia na kumpigia makofi bila kukoma ,ndio sababu ya kumheshimisha na kumpa thamani yake.
Waheshimiwa wabunge waliokuwepo na ambao hawakuwepo wakati wa sakata la Escrow wanakumbuka na wanakumbukunbu nzuri juu ya kazi kubwa, ya kishujaa na kizalendo kwa Taifa letu iliyofanywa na mheshimiwa David Kafulila aliyekuwa amejitolea maisha yake kupigania Taifa letu bila kujali vitisho kutoka kwa mtu yeyote yule.
Waheshimiwa wabunge wametuma kwa Vitendo ujumbe mzito sana juu ya Hazina hii kwa Taifa letu kuwa Bado sauti ya Mheshimiwa David Kafulila inahitajika sana Bungeni.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa. Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.View attachment 3017339View attachment 3017339
Kafulila ahama NCCR, ahamia Chadema Ijumaa, Desemba 16, 2016
SAFARI YA KISIASA YA DAVID KAFULILA BADO YAENDELEA, AIHAMA TENA CHADEMA
November 22, 2017
KAFULILA AHAMIA CCM
Baada ya kutangaza kujivua uanachama wa CHADEMA siku Jumatano, David Kafulila leo amekabidhiwa kadi ya CCM.
Kafulila amekabidhiwa kadi ya CCM na Katibu Mwenezi wa CCM, ndg Humphrey Polepole katika mkutano wa kumnadi mgombea wa udiwani wa chama hicho, Kata ya Mbweni jijini Dar es salaam.
Hapo awali Kafulila aliwahi kuwa mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendelo kisha kufuzwa baadae akajiunga na Chama cha NCCR Mageuzi ambapo alifanikiwa kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini mwaka 2010-2015 na baadaye kurudi tena Chadema 2016 na hapo juzi jumatano alitangaza kukihama chama hicho kwa madai upinzani hauna nia ya kupambana na ufisadi.