Miaka ya 2000's niliumwa malaria nikanywa amodiaquine ziko kama tatu hazizidi tano ila sitakaa nisahau ile experience ilikua unachungulia kaburi ile dawa iliongeza maumivu maradufu bora mchana usiku ndo maamuvi yaanapewa greenlight hulalali mwili ulichoka na nguvu zote ziliniishia
Week hii mwanzoni nimeumwa malaria nikasema acha ntumie mseto aisee mpaka sahivi najuta kwanini nilikubali mseto ni masaa 24 tokea nimalize mpaka sahivi
- Mwili umechoka
- Sina hamu ya kula yaani kula ni kwa mbinde
- Mdomo mchungu kupita maelezo
- Nikihema natoa harufu ya dawa za mseto
Hapana aisee hii dawa ipigwe marafuku kama ilivyokua kwa chloroquine na amodaquine ambazo hazitumiki tena
Ni bora ningekunywa quinine sio kwa mateso haya
Kwenye medicine kuna kitu kinaitwa pharmacovigiliance dawa ikishakuwa approval inafuatiliwa kama kuna severe side effects ambazo hazikuwa notice kipindi cha clinical trials ndo maana leo hii chloroquine au amodaquine hazitumiki tena