Dawa ya wadudu wanaokula mbao ni ipi?

Kwangu naona wamekula zile za pembeni, sijui wanaziita fishabodi........nilizopigia paa zenyewe nilinunua zile zilizo na dawa ambazo haziliwi na mchwa......pia inawezekana wameshindwa kuingia kula za kwenye paa kwa sababu nimeziba na PVC.....ngoja nijipange na kuzinusuru fishabodi zangu maana niliona wametoboa baadhi ya sehemu.
 

It coasted???? Duh! Hiyo ndiyo english ya shule za kamchape!
 
Tunamuita bulumuzi huyo jamaa anaetoboa mbao. Hivi kuna yeyote amewahi kusikia case ya mtu kung'atwa na huyo kiumbe?
 
Oil chafu
 
Nakumbuka nilihamiaga getto moja mabibo huyo mdudu alikua anakula mlango, with in few weeks nikaanza kumsikia anatafuna kabati langu la vitabu.

Aisee aliliharibu sana na anatembea ndani kwa ndani, nilikuja kuvunja ule upande wa kabati nikatoa ule ubao fundi akaweka mwingine ndo pona yangu, ila kitanda changu mninga alishindwa kutoboa.

Kwenye dari hapo fata ushauri wa oil chafu au mafuta ya taaa.
 
Kesi yako ni kama yangu niliamia nikakuta anakula mlango mmoja baadae ndio akaamia kwenye vitu vyangu.
Afadhali wewe kagusa kabati pekee mimi wanakula kila kitu yani kwa style hiyo nitavunja kila fenicha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…