Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Wanaonea sana sasa hivi mpaka hata mjinga unaona ipo siku yataisha tu kila jaribu lina mlango wakutokea, na MUNGU anakupa jaribu unaloliweza

We fuata taratibu na sheria zilizopo tuone kama utaonewa. Usipofanya hivyo lazima uonewe tu. Hamna namna
 
Huyu jamaa muongo sana mbowe hajakamatwa ila amejisalimisha mwenyewe kituo cha police. Source channel 10 habari ya saa 1:00
Ndio maana siku Hizi JF inazidi kukosa Hadhi kwa Mods kuacha thread kama hizi.....maana thread ina mapungu mengi basi hata wangeirekebisha.
 
::Usahihi: Mbowe Kaenda polisi mwenyewe,Katibu CHADEMA Dar athibitisha::

Waheshimiwa Viongozi na Wanachama wa Chadema Dar es salaam, Siku ya leo Mwenyekiti wa Chama Mhe.Freeman Mbowe akiwa Kwenye Mkoa wetu wa Dar es salaam, Ameamua kwenda Central baada ya kuwepo na Taarifa nyingi kwenye vyombo vya habari na Mitandao ya kijamii kuwa anahitajika nao.

Taarifa za kusema ya kwamba jeshi limemkamata na kumpeleka Central ni taarifa za uongo ambazo hatujui zinataka kulenga kitu gani...Taarifa sahihi ni Kwamba Mhe.Freeman Mbowe ameamua kwenda baada ya taarifa kuzagaa kuwa anatafutwa.

By H Kilewo
Katibu Mkoa wa Dsm
 
Updates : kukamatwa kwa Mhe.Freeman Mbowe

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Mhe.Edward Lowassa amekatisha mapumziko yake Kijijini Monduli na kurudi DSM kwa lengo la kumuwezesha kufuatilia kwa karibu suala la Mwenyekiti wake Mhe. Freeman Mbowe.

Lowassa alikuwa Monduli katika mapumziko mafupi. Anatarajia Kuwasili kesho jumanne asubuhi.
 
Sakata la kumkamata Mboe limekosewa sana kimkakati, ingetosha kupeleleza kujua yupo wapi na hati ya mashtaka iandaliwe haraka kisha mahakama ikae sawa. wakamatwe mateja kama saba halafu wasimamishwe nae pamoja kwenye kesi ya kutumia dawa za kulevya kisha bwana mkubwa awe katikati ili picha za magazeti zitoke vizuri na kumbukumbu iwekwe kwa marejeo baadae (siku za usoni)
sasa kitendo cha kumkamata jioni kitamuongezea nguvu, na huwenda kikaonekana cha kisiasa zaidi kuliko matarajio yaliyokusudiwa.
hapa AKILI KUBWA haikutumika.
MUNGU WA DAR KACHEZEWA.
Akili upande huo huwezi kuipata hata siku moja mkuu
 
Kaazi kweli kweli... Tanzania ya viwanda naona imegeuka Tanzania ya kukandamiza upinzani na Uhuru Wa kuhoji
 
Hivi akipatikana kwa mkemia mkuu kwamba ni mtumiaji wa hivyo vitu, itakuwa vipi?
 
Wanaonea sana sasa hivi mpaka hata mjinga unaona ipo siku yataisha tu kila jaribu lina mlango wakutokea, na MUNGU anakupa jaribu unaloliweza

We fuata taratibu na sheria zilizopo tuone kama utaonewa. Usipofanya hivyo lazima uonewe tu. Hamna namna
Tanzania sio eneo salama tena kwa wapinzani bora bora niendelee kuishi Congo.

Wew unaijua Congo au unaisikia?

Jaribu siku moja kusafiri kwa gari kutoka mashariki mwa Congo mpaka Kinshasa ndo utajua kuongea sio kutenda

Na hali hii ya Congo ilianza kwa kila mmoja kutenda anavyoona yeye inafaa. Akitaka kufisadi sawa, akitaka kuiba sawa, akitaka kubwia ngada poa. Lakini mwisho wa siku ni nchi isiyotawalika. Lazima tutii sheria
 
Huto..... mpaka hai. Mimi naamini anabwia. Kama alikuwa habwii nini kilikuwa kinamuogopesha? Mimi sipati picha mtu kuogopa kwenda kituo cha polisi. Sielewi kabisa jaman. Hasa kwa nchi kama yetu na hadhi ya mtu kama mbowe.
Mbona watu upumbavu hauwaishi? Mbowe kaogopa kwenda Polisi? Inamaana aliposema kama anahitajika polisi aitwe kwa utaratibu unaopaswa na sio hilo li Daudi litumie redio na tv kumuita. Hata Spika kasema hivyo, sasa hiyo habari ya kuogopa imetoka wapi? Mnadhani Mbowe ni fala kama nyie mnaoweza kuitwa hata kwa kupiga filimbi?
Haya mambo mnayoyatengeneza siku yakiwageuka mtalia na kusaga meno yetu yenye kutu.
 
Taarifa nilizopata kutoka kwenye chanzo changu cha kuaminika ni kwamba, Mwenyekiti wa CHADEMA, FREEMAN MBOWE ametiwa nguvuni na Jeshi la Polisi baada ya jitihada za kukimbia na kujificha kushindikana.

Mbowe amekamatwa maeneo ya Mikocheni ambako alienda kujificha ili asikamatwe na Jeshi la Polisi.

Kwa sasa wapo njiani kuelekea Central ambako atahojiwa kutokana na tuhuma za kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya pamoja na kulisababishia usumbufu na gharama jeshi la polisi.

Taarifa zaidi zinasema kuwa Mbowe amekamatwa akitolewa kwenye Appartment Moja kwenda nyingine akitumia gari Nyeusi, Tinted yenye namba za usajili T 830 DEW aina ya VX. Wamemkamata akiwa nje ya geti ya Appartment hiyo ambayo ni miongoni mwa majengo ya siri ( Safe House) yanayomilikiwa na CHADEMA


Kwa nini unaandika taarifa zisizo sahihi kwamba Mhe.Freeman Aikaeli Mbowe amekatwa wakati amehamua yeye mwenyewe kwenda polisi ?

Kwa nini unadanganya mtu mzima kwamba amekatwa Mikocheni wakati alitokea maskani yake Kawe kuelekea polisi ?

Kuanzia leo sitaamini habari zako hapa kwa kuwa vyanzo vya habari vya upoteshaji kwa uzoefu wako !
 
Wazalendo wote tunamuunga mkono Magufuli
Uzalendo au ushabiki? Una uzalendo gani zaidi ya uombaomba na kupiga mizinga pale Lumumba? Mtasifia sana kila upuuzi but the day shall come! Yes, ukiona Giza totoro ujue kupambazuka kunakaribia na siku mpya kuanza.
 
Huu ni mpango wa ccm kumwondoa magufuli 2020. angalia machinga Leo magu anasema hivi, utasikia kesho hivi. Namshauri Rais amalizane na wana ccm wenzie, nadhani wanasubiri asinzie wampore.
 
::Usahihi: Mbowe Kaenda polisi mwenyewe,Katibu CHADEMA Dar athibitisha::

Waheshimiwa Viongozi na Wanachama wa Chadema Dar es salaam, Siku ya leo Mwenyekiti wa Chama Mhe.Freeman Mbowe akiwa Kwenye Mkoa wetu wa Dar es salaam, Ameamua kwenda Central baada ya kuwepo na Taarifa nyingi kwenye vyombo vya habari na Mitandao ya kijamii kuwa anahitajika nao.

Taarifa za kusema ya kwamba jeshi limemkamata na kumpeleka Central ni taarifa za uongo ambazo hatujui zinataka kulenga kitu gani...Taarifa sahihi ni Kwamba Mhe.Freeman Mbowe ameamua kwenda baada ya taarifa kuzagaa kuwa anatafutwa.

By H Kilewo
Katibu Mkoa wa Dsm
Kuna mtu anaitwa Lizaboni, yeye kazi yake kutunga na watu wanafuata tuu uzushi wake bila kujiuliza. Ni mtu mnafiki haijapata kutokea na hata ndani ya chama chake anatabia ya kuwazushia wengine kwa manufaa ya kundi linalomtumia kama pedi
 
Safehouse means the house is supposed to be safe,sasa unakamatwaje nje ya geti?,

either jamaa walikuwa na inside information au ulifanyika uzembe sana,does it means countersurveillance ilikuwa NIL,

Ndo kusema hata hawakuwa na spotter wa kucheck usalama huko nje kabla boss hajachomoka ndani?,

maana hata kama imeleak information kuwa yuko hapo, a well placed spotters wangeona movements zisizokuwa za kawaida na wangeshituka

Unatetea kujificha ficha kwa mbowe wakat anatafutwa na polisi?
 
Kwa nini unaandika taarifa zisizo sahihi kwamba Mhe.Freeman Aikaeli Mbowe amekatwa wakati amehamua yeye mwenyewe kwenda polisi ?

Kwa nini unadanganya mtu mzima kwamba amekatwa Mikocheni wakati alitokea maskani yake Kawe kuelekea polisi ?

Kuanzia leo sitaamini habari zako hapa kwa kuwa vyanzo vya habari vya upoteshaji kwa uzoefu wako !
Huyo mtu ni hatari kwa uzushi hapa JF.
NAMTANGAZA RASMI Lizaboni KAMA MTU MUONGO KULIKO WOTE HAPA JAMIIFORUMS. Aadhibiwe kwa uongo huu.
 
mods nao wanapuuzia taarifa kama hizi.....sasa credibility ya JF inanipa ukakasi...kwann mods wasirekebishe heading ya mleta mada
Kwanini heading imeanza na madawa ya kulevya na bado mpaka sasa hawajabadili. mbona wengine wakitajwa mnafuta Uzi muda huo huo.
 
Mkuu, ikithibitika hizi taarifa si za kweli naacha kuitetea CCM na Serikali na nitajiunga na Team Lowasa kama ulivyofanya wewe

Kuwa mjinga sio mpaka ufungwe kengere! Kumbe hata ukiwa mwanaCCM yakubidi ujitoe ufahamu ili uweze kuwekwa kwenye payroll ya Lumumba buku ten kwani hali imekuwa ngumu sana tokea msukuma akabidhiwe usukani.

Inshort Mh. Mbowe hajakamatwa kama unavyotaka kuuaminishanumma wa JF ila imembidi kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi kwani upuuzi ukinyamazwa hugeuka ukweli. Na siku zote kadiri unapomkimbia adui yako ndio unamuongezea uhalali wa kukushutumu na hivyo kuiaminisha jamii kuwa wewe ni mkosefu.

Ikumbukwe kuwa ukiwa muongo ukumbuke ulipo anzia na mwisho wa siku muongo hutokomea na tusijue alipoelekea.

Kwa kuwa unatumia jina bandia huku ukizani kuwa hakuna anayekufahamu, pole yako! Tunakujua fika kuanzia ukoo wenu, wazazi wako, wewe mwenyewe na hata demu wako sasa sijui utajifichia wapi mwisho wa siku.

Mtoto mdogo muongo na mnafiki ukizeeka utakuwa Mchawi!
 
We fuata taratibu na sheria zilizopo tuone kama utaonewa. Usipofanya hivyo lazima uonewe tu. Hamna namna


Wew unaijua Congo au unaisikia?

Jaribu siku moja kusafiri kwa gari kutoka mashariki mwa Congo mpaka Kinshasa ndo utajua kuongea sio kutenda

Na hali hii ya Congo ilianza kwa kila mmoja kutenda anavyoona yeye inafaa. Akitaka kufisadi sawa, akitaka kuiba sawa, akitaka kubwia ngada poa. Lakini mwisho wa siku ni nchi isiyotawalika. Lazima tutii sheria
huijui historia ya congo wewe.
 
Huu ni mpango wa ccm kumwondoa magufuli 2020. angalia machinga Leo magu anasema hivi, utasikia kesho hivi. Namshauri Rais amalizane na wana ccm wenzie, nadhani wanasubiri asinzie wampore.
Mada/singo yenu mpya kwa sasa ni Machinga na Mama Ntilie mkuu!?
 
Back
Top Bottom