Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Si alisema hatoenda Central ? ile misuli mbele ya waandishi wa habari imeishia wapi? ikiwa kama hajakutwa na madawa si ndio uzuri au wewe ulitaka akutwe na madawa? Muppet
Malumumba kilanga kimewashuka
 
Kuwa mpole, pale kuna mabishano ya kisheria, hayahitaji wingi wa watu.
Kibatala na jopo lake wanashughulika nalo
 
Amachosema Kimweri ni kweli, kila kitu manual manual

Polisi wameshafanya makosa, hawapaswi kufanyia kazi tuhuma kwa majina ya watu hadharani.
Kitendo hicho tu kinatosha kuvuruga uchunguzi na ushahidi

Kutaja watu bila kuwa na ushahidi ni kosa. Katika nchi za wenzetu watu wangevuna mabilioni

Tatu, Mbowe ni kiongozi wa kisiasa Bungeni, katika vyama n.k. Kumfikia kwa simu bila kuanza kutangaza jina lake ni sehemu ya weledi. Kwanini hawakufanya hivyo

Kulikuwa na sababu gani za Sirro kwenda kwenye TV ikiwa Polisi ina intelejensia zote?

Alichokifanya kina sura ya kudhalilisha na kinachukua sura ya kisiasa? Kwanini!

1. Mbowe aliandamwa na Bilicana
2. Akafuatiliwa Hotel zake huko Machame

Yote hayo yalifanyika yakibeba hisia za ''political motivations'' nyuma yake

Leo hata kama Mbowe atakikutwa na lolote tayari kuna makosa yamefanyika

Kosa la kwanza ni hilo la Polisi kuvuruga uchunguzi wao wenyewe.

Huwezi kumtuhumu mtu kabla ya kumpekua.

Hivi kama Mbowe ana kidhibiti si atakuwa ameshaharibu ushahidi kama ni hivyo!
Polisi wanatangaza katika TV halafu wanakwenda kumpekua mtuhumiwa! Jamani! Real

Polisi walitakiwa kufanya kazi zao kimya kimya na kitaalam si kupitia TV kama wanasiasa

Kwa namna yoyote suala zima limechukua sura ya kisiasa na ni ngumu mtu kuamini Mbowe ana makosa hata kama anayo. Polisi wameshafanya kosa na suala zima sasa ni la kisiasa zaidi ya tuhuma

Haya yanafanyika kwa nini? ndio maana wengine tuna hofu kubwa na mustakabali wa Taifa

Upendo, haki utu na ubinadamu sasa ni zawadi tu.
Kinachoonekana ni chuki, visasi na vinyongo. Hakuna taratibu zinaoztuongoza bali utashi tu wa watu

Nakumbuka habari ya kamanda mmoja wa Dar aliyetumika sana kisiasa.
Kesi ilipomkuta akabaki mwenyewe. Wenzake wakihukumiwa kifo alitoka mahakama kuu utadhani siye

Siku hizi ni muumini mzuri sana wa dini, pengine akitubia na kujutia aliyofanya
Kiongozi huyo leo huwezi kumwambia lolote kuhusu haki au dhulma, halali au batili

Sisi si wamoja tena, tumegawanyika, hatuaminiani. Tunaangaliana kama ''maadui'' na si wananchi

Leo akitokea adui wa nje, ni rahisi sana kutuvuruga. Tayari hatuna mshikamano

Tumekuwa Taifa la watu waliobeba vinyongo, chuki na inda vifuani.

Tumekuwa Taifa lisiloheshimu haki za watu, taifa lisilojali upendo. Taifa lisilothamini haki za binadamu

Hatutembei vifua mbele kama Watanzania wa Nyerere, tunatembea vifua vilivyoinuka kwa kujaa chuki, vinyongo, visasi.

Tukae chini na kujiuliza hatma ya haya ni nini? Tunakiachia kizazi kijacho nchi gani?
 
Nimewadharau sana Jeshi la Polisi walitumia nguvu kubwa sana bila sababu za msingi. Sirro na Makonda mjiandae kuitwa mahakamani.
Ofisa habari wa chama hicho, Tumaini Makene ameithibitishia Mwananchi Digital taarifa za kuachiwa mwanasiasa huyo kuwa ni za kweli.
 
Madawa ya kulevya ni issue mbaya kuliko lugumi, escrow, epa
 
Wale hata walikuwa cyo watafuta Ngada ila kuna mambo mengine kabisa waliyokuwa wanayatafuta ila yamekosekana ndo maana wamemuachia huru.Issue ya NGADA ni danganya Toto tuu.
Pole sana Mh.Aikael Freeman Mbowe kwa usumbufu waliokupa hawa jamaa.
Inasemekana kuna nyaraka za chama wameondoka nazo
 
WABADILISHE RASIMU HIYO IWE UNGA. huchelewi kusikia tulitaka atusaidie upelelezi
HAHAHAHAHAHAHA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…