Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Na Tundu Lissu usiku huu:

Waheshimiwa habari za usiku huu. Naomba kutoa updates juu ya kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Chama Mh. Freeman Mbowe. Mimi na Katibu Mkuu Dkt. Vincent Mashinji tumeshuhudia sehemu ya sachi iliyofanyika nyumbani kwa Mwenyekiti kati ya saa tatu unusu na saa sita usiku huu. Kama nilivyosema kwenye ujumbe wangu wa awali, hii sio vita dhidi ya wafanya biashara ya madawa haramu bali ni vita ya kisiasa dhidi ya sisi wapinzani wa CCM na Rais Magufuli. Kwa uthibitisho wa kauli yangu naomba niwapatie orodha ya vitu walivyokamata polisi nyumbani kwa Mwenyekiti Mbowe. Vitu hivyo vimeorodheshwa kwenye fomu na. DCEA 003 inayoitwa 'Hati ya Ukamataji' iliyotolewa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kama ifuatavyo:
(1) Hati moja ya CHADEMA CHASO kwenda kwa Mwenyekiti ya tarehe 16/7/2013
(2) Picha mbali mbali nane za matukio ya uhalifu - picha za wahalifu wanaoharibu mali
(3) Hati moja ya Rasimu ya Kwanza ya CHADEMA kuhusu uundwaji wa Red Brigade
(4) Hati moja ya kurasa 13 inayoongelea mambo ya Muungano.

Hivi ndivyo vielelezo vilivyokamatwa nyumbani kwa Mwenyekiti vinavyothibitisha kwamba yeye ni muuza unga!!! Kama isingekuwa ukweli kwamba hivi ninavyoandika Mwenyekiti wangu yuko mahabusu Central, hiki kingekuwa kichekesho cha mwaka. Lakini Mwenyekiti anasota mahabusu usiku huu. Huu ndio ushahidi ambao Kamanda Sirro na polisi wake wamekuwa wanamtafutia Mwenyekiti wetu kwa amri ya Paul Makonda. Hatuna budi, katika hali hii, kuomboleza - kama alivyofanya Mwalimu katika kitabu chake 'Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania' - juu ya mahali ilikofikishwa nchi hii yetu. Nitawatumia picha ya orodha hiyo shortly.

Update: Mwenyekiti Mbowe aachiwa

Kama tulivyowajuza kwamba iwapo itatokea jambo lolote la umuhimu kujuzana kabla ya asubuhi tutafanya hivyo, tunapenda kuwatangazia wanachama wetu,wadau,wapenzi, na wapenda haki,amani na demokrasia ya kwamba Mwenyekiti Freeman Mbowe ameachiwa huru punde tu mnamo majira ya SAA saba na robo usiku huu.

Tunawashukuri wote kwa sala,maombi na subira na hivyo kuhitimisha salama SAA KUMI za Mwenyekiti wetu kuwa chini ya Jeshi la Polisi nchini katika kituo kikuu cha Polisi jijini Dar es salaam.

Taarifa za ziada juu ya jambo hili zitatolewa kesho.

Salum Mwalim
Naibu Katibu Mkuu
Chadema
Kuna wakati Tundu Lisu huwa una-behave kama mtoto hivi! Unapenda kuhemka kuliko uhalisia
 
nda tanzaniza imekuwa tatizo mana sahivi kilakona madawa ya kulevya tunaoba tuungane kwa pamonja na hili njanga la madawa ya kulevya ili tulitokomeze na ibaki histolia mana ndo yaibu sana
 
We huna Akili, eti hii vita ya madawa ni ya chadema! Unataka kutuambia akina Wema, TID, Manji(diwani wa ccm) hao wote ni chadema? Uwe unatumia angalau sehemu kidogo ya ubongo wako iliyobakia kuacha mihemko na kuwa mkweli. Ovyo sana wewe.




Kati ya hao uliowataja hakuna hata mmoja anayeweza kutolewa kama mfano wa ufanisi wa vita dhidi ya mihadarati nchini.Wema Sepetu kosa lake ni kukutwa na msokoto wa bangi wenye thamani ya sh.300/,TID yeye anatumika kama mahamasishaji baada ya kukiri kutumia dawa za kulevya,Mh.Manji yeye ni teja tajiri aliyegundulika kuwa anatumia Dawa za kulevya.

Sasa kati ya hao ni yupi anaweza kutumia kama mfano dhidi ya vita hii ya madawa ya kulevya?
 
Hata ulichokiandika haukijui
Soma vizuri basi hii apa.. wewe na Chadema(Mbowe) hukumu yanu ipo kwa shetani ? kama hujui kosema ni kosa la wazee wako usitubebeshe sisi misalaba.
 
Umemtafuta mtu kwa zaidi ya week moja. Trend inajulikana kwamba ukimpata, unaenda kwake kumsearch. Anajileta baada ya siku 10 then unaenda kumpekua kwake.

Even my 7 year old Son will never ever do such stupid act. John, tumbua huyu Zerro. Hatoshi.
 
Soma vizuri basi hii apa.. wewe na Chadema(Mbowe) hukumu yanu ipo kwa shetani ? kama hujui kosema ni kosa la wazee wako usitubebeshe sisi misalaba.
Mmeumbuka sasa Mbowe hakukutwa na madawa
 
hawa wanaotaka watanzania wawaombee wakati wao wanawatndea maovu wenzao hakika moto wa jehanamu ni halali yao
 
Tundu kawa mtetezI wa ujinga
Unajua kumjua mwenye akili na hata kujua mambo yaliyo na maana na umuhimu ni lazima uwe na akili timamu. Usipokuwa na akili unaweza kuyaona yaliyo ya maana si lolote, na yasiyo ya maana ukayaona ndiyo ya muhimu. Yumkini taahira huweza kuacha hela lakini akakimbilia kopo.

Bahati mbaya wagonjwa wa akili huwa hawajitambui, na huwa wanaamini kuwa ni wazima.
 
Bila shaka wameenjoy kuona nyumbani kwa Mbowe kulivyo na hadhi ya juu kuliko kwa mawaziri wengi, ndicho walichotaka kuona
 
Si alisema hatoenda Central ? ile misule mbele ya waandishi wa habari imeishia wapi? ikiwa kama hajakutwa na madawa si ndio uzuri au wewe ulitaka akutwe na madawa? Muppet
Hata kuandika hujui
 
Huu ni unyanyasaji uonevu .na ukandamizaji wa demokrasia na haki za binadamu.hivi huyu kamanda sirro anafikiri haya anayo fanya yanautashi kwelu ndani yake?.Ipo siku yake what goes around comes around
 
Back
Top Bottom