Dawa za Kulevya: Wema adai Makonda anatembea na Agnes Masogange ndio maana hakamatwi

Dawa za Kulevya: Wema adai Makonda anatembea na Agnes Masogange ndio maana hakamatwi

Huyu alierekodi ni mnafiki na hamtakii mema Wema...kuna sehemu karudia rudia anamuuliza Wema boss nani, Wema anajibu boss m*t*k*! Sasa huyu Mange nae aliepost hii audio si kama anamgandamiza Wema?!!
Alikuwa anapiga umbea na Team Wema!

Walienda kumtembelea ndo akawa anaropoka hivyo..

Na hizo audio aliyezipata wa kwanza kazinunua laki moja IG..

Wema hana rafiki japo yy anapenda marafiki...
 
Makonda kawashika pabaya kwa hili akuna atakae muelewa naona Ana wasomesha namba wasanii mbaya zaidi kaanzia wasanii wakubwa huu mfumo nimeupenda makonda kwa hili tupo nyuma yako
 
Yaani mange ndio ziro brain

Katushiwa clip kaona masifa kuwa source of infomation kumbe anazidi kumponza mwenzie

Na aliyemrekodi atakuwa mtu wa karibu na wema ambaye wema anamuamini ndio maana akajiachia

Inasikitisha sana pale .....mtu wa karibu na wewe ndio anakuponza
Sio kina Junaither kweli waliomrecord manake ndo group lake sasa hivi...

Mwenyewe anajisifia eti wanampa magauni, vipidozi na viatu buree...

Watu wanafiki jamani khaaa!
 
Konda bana anampangia MASOGANGE masela Wanakula kiulaini bure Haaa kanda ya ziwa ina watu mi zezeta balaa
Hahahaha,
Wanapenda ile wezere ukimtupia na rangi kidogo ya carollite hawanaga ujanja
 
Sikuhizi Uhuru wa kusema chochote imekuwa issue. Wema hajafanya makosa kutumia uhuru wa kuongea jinsi anavyo mfikiria Makonda. Makonda ni binaadam na ana mapungufu kama wengine. Kama kusema anatembea au kumpangia nyumba mwanamke fulani ni kosa. Basi, Tanzania tunaelekea kubaya zaidi katika freedom of speech.
Na hasa, je kuna ushaidi wa kutosha kuwa Wema Sepetu anajiusisha na unga? Au ndiyo mkuu akisema ndiyo ushaidi tayari wasiyo na hatia kutiwa ndani! Je Wema amekutwa na madawa au uonevu tu? Wacha hayo wakina Makonda! Serikali haiendeshwi kwa ubabe, lazima mfwate Sheria na haki, siyo kukulupuka tu.
 
Mchanganuo wa video clip hii kwa nionavyo:-

1. Wema hajakanusha kwamba hahusiki na madawa yakulevya -moja kwa moja yuko guilty!.

2. Anategemea favor, influence ya mfumo kumweka huru. .

3. Anasema wazungu wameachiwa mbona wao ndio wamebaki, kwa hiyo anataka aachwe huru waendelee kama watakavyo.

4. Anataja na mateja wengine "Agness".

5. Nimegundua shule ni ufunguo wa maisha.

a) mtu gani mweye elimu yake japo kidogo angesema "tumesikia anataka uwaziri....". Huu si ujuhan sana? Kutaka uwaziri kwa mtu na kushindwa kujitetea kwa mtuhumiwa kuna husiana nini? Kwa hiyo aachwe tu aendelee kuua watu kwa sababu hakuna kiongozi anayeonyesha kujali? Uwaziri wa Makonda utakuja kwa kazi zake, lakini hakuna uzalendo wa mtu utathibitiska kwa kuwaogopa waharifu kwa sababu wana macho ya kutisha.

b). Sijawahi kufikiria mtu katila level hii, anaweza kuwa na akili za kitoto kwamba fulani mbona kaachwa? Akidhani kwamba kwa kuwa mwingine hajakamatwa kwa kuwa ni "mwanamke wa rc na kamjengea nyumba sijui kampangishia nyumba makongo", kutapelekea kumwondolea hatia ya mashitaka.

Nani washauri wa Wema? Mbona mnawamcha anaangamia huku mkiona? Mpeni maarifa na hekima basi japo kidogo. Au na wshauri wake ni wa kiwango cha ngono, kujionyesha na kugombana tu?

Pole kwa Watanzania wote!
wacha uongo kuna mtu hajui masogange hakushikwa south africa
 
Sikuhizi Uhuru wa kusema chochote imekuwa issue. Wema hajafanya makosa kutumia uhuru wa kuongea jinsi anavyo mfikiria Makonda. Makonda ni binaadam na ana mapungufu kama wengine. Kama kusema anatembea au kumpangia nyumba mwanamke fulani ni kosa. Basi, Tanzania tunaelekea kubaya zaidi katika freedom of speech.
Na hasa, je kuna ushaidi wa kutosha kuwa Wema Sepetu anajiusisha na unga? Au ndiyo mkuu akisema ndiyo ushaidi tayari wasiyo na hatia kutiwa ndani! Je Wema amekutwa na madawa au uonevu tu? Wacha hayo wakina Makonda! Serikali haiendeshwi kwa ubabe, lazima mfwate Sheria na haki, siyo kukulupuka tu.

Umejiuliza ni kwanini Wema na sio wewe au mimi? Makonda anajua anachokifanya.
 
hivi kumbe watanzania wengi hatujui nini maana ya chini ya ulinzi wa polisi....... ukiwa mahabusu au popote ili mradi ni chini ya ulinzi usiongelee tatizo lako ovyoovyo itakusaidia kujiweka katika safe side sasa uko chini ya ulinzi bado unakashifu mamlaka . siamini kama ni yeye labda mtu kaigiza... kama ni yeye anapaswa kupewa councelling ya namna ya kushughulikia tatizo lake anapaswa kusaidiwa usicheze na chombo kinachoitwa dola.
 
Ingekua mimi ni Wema ningekaa kimya hata mtu akija akiniuliza chochote nisingejibu isipokuwa pale ninapohitajika kufanya hivyo na vyombo vya sheria, ila nimejiuliza kwanini wamiliki wa Elements na Qbar wameachiwa?? Kwann wamenyima dhamani hawa wakina wema?? Makonda hataweza kweli kuwakamata mapapa na sio hivi vidagaa?
Mwisho wa hili sakata ni nini?? Nilitegemea leo watapelekwa mahakamani ila mpaka sasa kimya. Ngoja tuendelee kuangalia hii sinema mwisho wake ni nini
 
Back
Top Bottom