Elections 2010 DC Igunga ni mkristo mkatoliki; Kwanini hajasema kitu?

Unazungumzia heshima ya uislamu au ya uarabu?? Bakwata wamewazalilisha nyie baadhi ya waisilamu mnaosupport Bakwata na mama Joseph Kimario.
 
Bakwata wamewazalilisha nyie baadhi ya waisilamu mnaosupport Bakwata
Umejuaje mimi Muislam?

Nimesema, ukimvua Mwanamke hijab umedhalilisha alama ya Uislam na umemnyanyasa mwanamke, hata kama itakuja kugundulika kwamba aliyevaa vazi hilo si Muislam.

Kama ambavyo, kwa mfano, ukimkuta mtu amebeba Biblia, ukampokonya ukaikanyaga, umedhalilisha nguzo na alama ya Ukristo na Wakristo, hata kama itaja gundulika baadae kwamba aliyekuwa amebeba biblia ile si Mkristo.

Una upeo wewe wa kujibu hiyo hoja rahisi bila kukimbilia kusema mimi ni Muislam?
 
hiyo ndoa ya joseph na fatuma haina uhusiano na dini yake.....mama ni muislamu tena swala tano!hiyo haihitaji evidence ninamfahamu

evidence ni ufugaji wake wa mdudu aka kitimoto
 

DC Fatuma alikua amevaa mtandio, na sio hijab....hijab ni kama hii

Au kama hii....


Sasa huyu DC Fatuma alikua amevaa ipi kati ya hizo kama si siasa uchwara za CCM!?!?
 
Hata kama ni "mkristo mkatoriki" mfuga nguruwe, hai-justify yule mama kuwa-manhandled kama alivyofanyiwa yote sababu kavaa hijab. Ama baada ya kunena hayo, protests za BAKWATA kuhusu prejudices dhidi ya Waislamu bado zinabaki kwa halali, usanii wa yule mama notwithstanding.
 
DC Fatuma alikua amevaa mtandio, na sio hijab....
Wenye mamlaka ya kusema Fatuma alikuwa amevaa hijab ya Kiislam au vinginevyo, kisheria, kwa Tanzania, ni BAKWATA.

BAKWATA wamesema Fatuma alikuwa amevaa, na akavuliwa, hijabu. Lakini wamekosolewa kwamba mvaa hijabu alikuwa Mkatoliki. Ikawa mada yetu hapa, kwamba mvaa hijab kumbe alikuwa Mkatoliki.

Nikasema, ukimvua Mwanamke hijab, Mkatoliki au M-Sunni, umedhalilisha alama ya Uislam, Uislam wote, na Waislam, hali kadhalika umenyanyasa faragha ya Mwanamke. Hata kama aliyekuwa amevaa hijab ya Kiislam ni Mkatoliki.

BAKWATA wamesimama kutetea tamko la sheria na Katiba ya Tanzania, inayomtaka kila raia kuheshimu dini za Wananchi wenzake, zikiwemo alama na nguzo za imani za dini hizo, japo Tanzania haina dini ya Taifa, au dini ya serikali, ambayo kila Mtanzania lazima aifuate.
 
Kuna vitabu vingi vimeandikwa na Wasanii waliotumia nyenzo lukuki kama rangi bandia za ngozi (aka make-up), nywele bandia (aka false hairpieces or wigs) pamoja na symbolisms kibao kama namna ya mavazi na lafudhi ya lugha ili kujifanya wao ni Weusi au Wahamiaji kwenye nchi fulani, ili kuweka wazi upeo wa ubaguzi na udhalilishaji dhidi ya matabaka fulani ya watu kwenye jamii. Jee, wa kulaumu ni Wasanii husika au jamii kwa ujumla kuhusu matokeo ya social experiments za dizaini hii?
 
Nyandaigobeko

Huna mamlaka ya kudefine hijab ni nini kuwashinda Shura ya Maimam au Bakwata.

That being said, Fatuma Kimaro awe dini yoyote ile aliyo, alifanyiwa udhalilishaji kwa kuvuliwa nguo zake ambazo kwayo mwenyewe anapata stara (hijab). Bakwata wana haki ya kumtetea kudhalilishwa kwa mwanamke anae represent alama za dini inayoisimamia hata Kama aliyefuata alama hizo si Muislam

Kutetea udhalilishaji kwa vile umefanywa na Chadema ni kukosa fikra sahihi. Kesho keshokutwa Chadema kitakuwa madarakani, kikiendelea na udhalilishaji na upindishaji wa haki za msingi, tutakosa pa kukimbilia.

Penye kufaa kukemewa tukemee hata kwa wale tunaowapenda.
 
Kama tungepata picha yake wakibatizwa, akiwa kanisani, kwenye misa jumuia ndogo ndogo nk itakuwa poa zaidi
 
[
Ni kweli kabisa usemalo ila mwisilamu anapobatizwa anakuwa ametoka katika ile dini yake ya asili ya adam. Kwani kwa asili kila mwanadamu anapozaliwa huwa amerithi dini ya asili ya Adam na ndiyo maana bila ya ubatizo hujawa mkristo na hata kama utakata roho kabla ya ubatizo ili uzikwe kama mkristo lazima ubatizwe.

Uchaguzi wa Igunga umeidhalilisha sana safu ya uongozi wa bakwata kuwa hawawajui kondoo wao. Swali la kujiuliza ni je huyu mama huwa anasali msikiti wa Igunga?, na je kwa nini wakati wa sala ya Al-dhuhul alikuwa anafanya mkutano badala ya kusali?, Je mtu kama huyu ni worth kumtetea wana Bakwata?. Huu ni wakati sasa wa kuwaweka katika nafasi za uongozi wa kiislam vijana wenye elimu zote siyo elimu ya dini tu. Kilichowaponza masheikh ni njaa. watakuwa wamepewa 20K kila mmoja na kurukwa na akili na kuanza kumtumikia shetani bila kujijua.
Ni muda muafaka sasa waache KALA LAHU TAALA kwa ajii ya matumbo. Hii yote laana, maana hata wakiletwa tende za msaada na nyama za ngamia na kondoo wa hija watoe bure wao wanauza. Masilahi mbele mwenyezimungu baadae.

Ukitaka kujua hawa bakwa ni Laanatul Llah fika pale mtaa wa Lumumba kwenye ofisi yao ndogo au pale Kinondoni muslim uone jinsi walivyo. Kuna Dada yangu alikuwa anahitaji klatasi ya Bakwata ili aipeleke Mahakamani kwa ajili ya ku-file divorce na mumewe mkorofi fulani ikabidi akawaone wale wazee wa baraza pale, Wallah badala ya kumsaidia wakaanza kumtongoza, hii si laana hii?. Ndiyo maana mimi hata mahakama ya Kadhi naona haina faida kwa watu wasio na maadili ya mwenyezi mungu kama hawa BAKWATA. Wanainajisi dini ya mwenyezi mungu na kuchafua jina la uislam kwa kukubali kutumiwa kisiasa na CCM.
 
Ilichobaki sasa ni Bakwata kwenda kwa msajili wa vyama vya siasa na kusajili huu umoja kuwa ni chama kisha then kitaungana na CCM, CUF kwenye Muafaka.....................
 

Yaani kwa hoja hizi bado tunajiuliza ni kwanini watanzania mpaka leo hatuendelei? Too low to believe it came from one's brain.
 

wakiristo hatukuja kuipigania dini YESU alishamaliza pale msalabani kazi ni kwako kumfuata au LA! Choma kanisa,uwa mkirsto au chana chana biblia atuwez kuandamana sisi tu mavumbi na kila nafsi itaonja mauti na ukumu itafuhata.lakini yesu alikufa then akafufuka na yupo hai kuhukumu wanadamu.YESU aitaji pesa zako wala nguvu zako bali moyo wako tu.wakati yesu anasulubiwa walimdhalilisha sana alitemewa mate.yesu alishamaliza kazi msalabani kazi ni kwako kumfuata.
 

Wewe nawe unachanganya watu hapa,
Biblia inajulikana ni Biblia,
Na mshafu unaulikana msahafu.
Hijabu ni mpaka mvaaji awe ana lengo la kujisetiri mwili wake ndio itakua hijab, sio vazi fulani ndio hijab.
Kwa mwanamke WA KIISLAMU hata akichukua, kanga, kitenge, nk akaisetiri mwili wote inakua ni hijab, mradi kanga/vitenge hivyo havina maneno au marembo mabaya.
Hijab kama vazi maalum la kiislamu ili liitwe hijab sharti mvaaji aliamini kua ndilo la kumsetiri, sasa sidhani kama imani ya kikristo inaamini katika uvaaji wa kuziba mwili mzima na kuacha viganja na sura tu!!
Hijab hata ukiikuta hutaijua kama ni hijab kwani hakuna vazi (nguo) maalum inayoitwa hijab, bali ule uvaaji wake ndio unaotofautisha hijab na isiyo hijab, wewe nao hao bakwata wako mnachemka tu.
Baraza kuu la WAISLAMU tanzania na huyu mkristo wapi na wapi?
Labda liitwe Baraza kuu la Waislamu na wasio waislamu Tanzania.
 

Nawafahamu watu ambao walikuwa waislam wamebatizwa lakini wameendelea na majina yao ya kiislam. shida ni kuwa utambulisho wake wa kila cheti uko kwenye hilo jina la kiislam. kwa hiyo wanaona ni usumbufu tu kuanza jina jipya let say una miaka 45 au zaidi. Kwani jina ndio imani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…