DC Kiteto aenda kusikiliza Wananchi wa Ndaleta kuhusu mgogoro wa Ardhi, Wenyeji wailalamikia Halmashauri

DC Kiteto aenda kusikiliza Wananchi wa Ndaleta kuhusu mgogoro wa Ardhi, Wenyeji wailalamikia Halmashauri

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Wananchi wa Kijiji cha Ndaleta Wilayani Kiteto Mkoani Manyara wameilalamikia Halmashauri ya Wilaya hiyo wakidai imehusika kuhujumu Wananchi kwa kiwango kikubwa katika masuala ya mgogoro wa ardhi yanayoendelea.

Wameeleza kuwa wamefikisha malalamiko yao mara nyingi kuhusu mgogoro wa ardhi lakini hatua zinazochukuliwa ni zile ambazo zinakandamiza Wananchi.

Wakizungumza katika Mkutano wa Hadhara ulioongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Remidius Mwema wamedai kuwa hata mgogoro unaohusisha Hifadhi ya Indema WMA ambayo pia imekuwa ikijiita MAKAME WMA umetokana na baadhi ya viongozi wa Halmashauri kutotenda haki dhidi ya Wananchi wa kawaida.

Julius Tajiri, ambaye ni Mkulima amesema “Moja ya michezo inayofanywa na Viongozi wa Halmashauri ni kuwa kukitokea mgogoro wa ardhi, wanaomba Hati ya mwananchi, wakiiona wanatengeneza nyaraka nyingine za kuonesha huyo wanayemtetea alipewa nyuma ya yule aliyewaonesha Hati.

Ameongeza kuwa baadhi ya viongozi wamefanya migogoro kama njia ya kujiingizia maslahi kwao.

Joseph Michael, Mkazi wa Kijiji cha Ndaleta naye amesema Viongozi wa Halmashauri wanaelewa kinachoendelea lakini wanakwepa kutoa maelezo sahihi.

Kamanda wa Polisi Kiteto, SSP Paulo Mashimbi amewataka Wananchi kutumia mabaraza ya ardhi kumaliza migogoro mapema ili kuepusha misuguano ambayo inaweza kuwapa hasara Zaidi.

Akizungumza migogoro inayoendelea, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Remidius Mwema amesema “Nitaenda maeneo yenye changamoto ikiwemo lile lenye mgogoro wa Hifadhi ya WMA pamoja na Wanakijiji kujionea mwenyewe, nijue ninapofanya uamuzi wa kutamka tuwe na uhakika wa tunachokizungumza

Hata Rais akiniuliza kama nimefika maeneo husika niwe na majibu nisikune kichwa, tukibaini kuwa kuna makosa yalifanyika, watu wamechukuliwa maeneo yao na maeneo mengine yalikuwa mashamba ya Watu utaratibu wa kufidia utafanyika.

“Serikali haiwezi kumnyonya mtu yeyote Haki yake ya msingi, pia ispobainika tuwe tayari kuyakubali majibu hayo, naombeni mnipe nafasi, mwezi mmoja kuanzia leo tutakutana hapa, nitakuja kutoa maamuzi.”

Chanzo: EATV

Pia soma:
~ Wakulima 27 Wilayani Kiteto washikiliwa na Polisi kutokana na mgogoro wa Ardhi

~ Manyara: Wakulima Kiteto warejea kwenye mashamba waliyoondolewa, watuma ujumbe kwa Rais Samia wakidai wameporwa Ardhi yenye mashamba yao

~ Polisi Kiteto wamekamata Wakulima, wanawatesa na kuwanyima dhamana
 
Back
Top Bottom