Pre GE2025 DC wa Longido aliyesema alihusika kutengeneza mazingira ya Madiwani kushinda 2020 atenguliwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hata Iddy Amin tunamkumbuka.
Mkuu 'Tindo', nilipo soma tu taarifa za huyu DC, mara hiyo hiyo nikakukumbuka wewe...; unajuwa sababu. Na huyu aliyo yasema ndiyo yanayo halalisha kwa kila hali ile nadharia yako; ya kutojihangaisha kwenda kupanga mstari. Katika hali ya namna hii, hata mimi sina hamu ya kwenda kufanya hivyo.
Sasa nauliza: kwa nini hawa watu wame wadharau waTanzania kiasi hiki? Hawa wanao amua kubaki nyumbani kwa vile CCM na serikali yake wamekwisha maliza kazi ya kuwachagulia viongozi kwa nini wanaikubali hali hii bila kuhoji?.
 
Nimekwazika Sanaa....hivi hamna uwezekano Jeshi langu Pendwa
😭😭😭Nchii imeozaaa nimegundua. Tupambane na mambo mengine yanayowezekanaπŸ™ŒπŸ™Œ
Jeshi wameletewa Yutong za kutosha
 

Kwenye ile nadharia yangu sikosei nisemacho. Hii hadaa watu wajitokeze kushiriki uchaguzi ni ili kupata watu wengi kwa ajili ya kuhadaa umma na dunia kuwa wako madarakani kwa ridhaa ya wananchi wengi. Lakini kuwa wataheshimu maamuzi ya wananchi hilo sahau, maana wako kwenye mlo, na hawako tayari kuachia kwa njia ya amani. Bila machafuko ama mapinduzi ya kijeshi wataendelea kupindisha matokea ya kweli.
 
Alikuwa na confidence sana. Kuongea maneno yale? Weekend?

Hajui PDF zinatokaga weekend usiku?
 
Kwahiyo kosa lake ni nini hapo
Kuiba kura
Au kusema ukweli

Natumaini kesi hii itafika mahakaman
 
KUNA NABII AMETABIRI MPASUKO MKUBWA CHAMANI
Yamkini Ikawa hivyo
Kambi ya Nape, ndugai na makamba hiyo inaongezeka

Na NDIO vizuri sana
Ili tumpate magufuli ni lazima wavuruguke tu hawa
 

Alikuwa na confidence sana. Kuongea maneno yale? Weekend?

Hajui PDF zinatokaga weekend usiku?

Sijaiona mkuu itupie kama unayo tuluke nayoi

View: https://www.instagram.com/reel/C_YdnoQoxHzgVwcGirA_Z53CXVNNhbSoCCvlwA0/?igsh=MWVnaDIxbHcxYmpoMg==
 
Kiburi cha madaraka
 
Mh. Rais wetu safiiiii sanaaa, excellent, hawa viongozi wanaoongea hovyo hovyo na kujiona Miungu watu, dawa yao ndio hiyo, piga chini haraka sana, wala hakuna kelele ni kufukuza kazi tu, safi kabisa πŸ‘πŸ‘πŸ‘
Kwahiyo wewe unafurahia wizi wa kura na utekaji
 
Sasa hapa ndipo huwa napishana na wewe kila mara, na kila nikuliza maelezo huwa sipati.

Nadharia ni kwamba, "kwenda kupiga kura ni kupoteza muda". Kwa hiyo njia sahihi kwako na kwa wengine ni kususia kwa kila njia upigaji kura huo, kwa vile matokeo hutengenezwa na CCM kabla hata ya uchaguzi haujafanyika.
Nadharia inasubiri "machafuko toka kwa wananchi au jeshi". Swali ambalo huwa hutaki kujibu ni kwa nini kupiga kura huku kwa wananchi ndiyo isiwe sababu halali na nzuri kabisa ya kufanyika kwa machafuko?

Mimi mtazamo wangu ni kwamba, wananchi wanatakiwa wajitokeze kwa wingi wao kupiga kura zao, na hawa wapumbavu wakizichezea kura hizo moto uwawakie hapo hapo. Sasa sijui kwenye nadharia machafuko yaliyo anzishwa na wananchi hutegemewa yatokee wapi na vipi hasa!
Jeshi ni sehemu ya CCM. Jeshi letu hulelewa na CCM kama chama. Viongozi wake wanapo staafu hupata vyeo ndani ya CCM na serikalini. Kwa hiyo ina wawia vigumu kuukata mkono unaotegemewa kuwalisha. Labda kwa bahati itokee vijana wenye vyeo vya chini wanao sukumwa na uzalendo badala ya kushibisha tumbo.

Kwa hiyo, nawahimiza sana CHADEMA wafanye kazi na wananchi, kuwapa elimu na kuwaomba wajitokeze kwa wingi kupiga kura kuikataa CCM. Hao hao CHADEMA wawape mbinu wananchi kuzuia kura zao ziliharibiwe. Huo ndio msimamo wangu kabla sijajiunga na huko kwenye nadharia moja kwa moja.
 
Kiburi cha madaraka
Na "kiburi" kimejaa kweli kweli ndani ya CCM, toka juu kabisa hadi chini. Ni kama vile waTanzania ni mali yao, kama mifugo vile wanayo weza kufanya maamuzi yoyote wanayo taka wenyewe bila ya kuhojiwa na yeyote.
Hali hii anayo Samia mwenyewe, na wengine wote, kama akina Mwigulu, n.k., n.k..

Sijui waTanzania imekuwaje tukawa katika hali hii ya kutekwa namna hii bila hata ya kuonyesha dalili za kuikataa!
 
Ulitaka kwa siku ya leo cdm wafanye nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…