Depression inanimaliza, sina muda mrefu wa kuishi

Depression inanimaliza, sina muda mrefu wa kuishi

Jaribu kuhama hiyo sehemu unayoishi,
Nenda mji mwingine ubadili upepo,pata new challenge kwenye maisha,

Relax,chukulia maisha simple tu,life is too short,hakuna haja ya kuwaza sana,
Ishi maisha yako,usiishi kuwafurahisha watu wala kuwaza,watu watanionaje?
Kua free na maisha yako,
Love the life u live
Live the life u love.
 
Pole sana Mkuu Kuna mambo mengi yako nyuma ya hiyo Depression.

Depression sio ugonjwa bali matokeonya jambo fulani ktk maisha yako.

Hayo hujayataja. Unahitaji Mtaalam atakayekupa muda wake mkazungumza kwa kina na kirefu zaidi.

Njoo Dar es salaam kutana na Wataalam wa afya ya akili.

Nenda kwa Dr Likindikoki pale Muhimbili au wengine.

Tunakuhitaji kama Taifa, we ni wa muhimi sana kwa Familia yako na jamii pia
Mwenyezi Mungu Akulinde na akubariki zaidi na zaidi, pia akusamehe pale ulipokosea. Hakika wewe bila shaka unaonekana ni mtu mwema, ni watu wachache sana wenye kufariji wenzao kwa maneno mazuri yenye kutia moyo na kuwaonesha mwanga maishani kwamba katika hali yoyote ile haujawa mwisho wa maisha.

BIG UP!
 
Weka namba yako ya simu au E-mail then nitakupigia simu na kukutafutia wataalamu Kwa gharama zangu mwenyewe .


Usjiue mkuu.
Mwenyezi Mungu Akulinde na akubariki zaidi na zaidi, pia akusamehe pale ulipokosea. Hakika wewe bila shaka unaonekana ni mtu mwema, ni watu wachache sana wenye kufariji wenzao kwa maneno mazuri yenye kutia moyo na kuwaonesha mwanga maishani kwamba katika hali yoyote ile haujawa mwisho wa maisha.

BIG UP!
 
Tangu 2019 mpaka sasa nasumbuka na msongo mkali wa mawazo, uoga ulipitiliza, panic attack, yaani nimekuwa kama mfu anaetembea, nilienda hospitali ya Mount Meru Arusha wakaniambia ni psychosis, wakanipa Haloperidol na Benzylhexol nikaanza kutumia ila zilinisaidia kwa wiki chache baada ya hapo hali ikawa mbaya zaidi ya mwanzo na nikawa nikitumia kichwa kinakuwa chepesi kupita kiasi kama nimelewa.

Nikaamua kuacha zile dawa kwa sasa naona sina muda mrefu wa kuishi, imechoka sana

Pole sana!

Pili, hongera sana kwa kuamua kushirikisha wengine haya unayoyapitia, ni mwanzo mzuri wa kutatua na kulimaliza tatizo hilo amini hivyo.

Depression ipo na inawatesa wengi. Matibabu yake kamili ni kubaini chanzo chake (kisababishi) na si kutumia dawa tu. Pia mbali na dawa kuna matibabu maalumu ambayo hutolewa na wataalamu wa psychology inaitwa psychotherapy.

Kutibu depression huchukua muda mrefu kidogo, wala siyo wiki au wiki mbili. Unahitaji kuhudhuria clinic au sessions kila mwezi nk

Kwa hiyo pamoja na msaada na ushauri ambao wenzangu wamekupa nami nikushauri pia:

-uweze kubaini chanzo (kisababishi) cha tatizo hili kwako kwani itasaidia sana kujua aina ya ushauri, msaada au tiba ambayo itakufanya uwe sawa.

-usikate tamaa: Kuna vingi unaweza kufanya hata kama kuna mahali pengine ulifeli au ulifanya vibaya.

-epuka kukaa pekeeako/kujitenga-shirikiana vizuri na wote wanaoonesha utayari wa kukusaidia

-rudi kwa madaktari wale waliokuandikia hizo dawa ili uwape mrejesho wa hali yako baada ya kuzitumia hizo dawa

Mwisho, hongera sana kwa kuomba msaada na kushirikisha changamoto hizi unazopitia kwa jamii, naamini kwa msaada na ushauri wa jamii hii utakuwa sawa mkuu.

You're a hero, you're a winner!
Kila la kheri.
 
Pole sana ila kumbuka kuna watu wanatamani maisha unayoishi maana wana hali mbaya kuliko wewe na hawajakata tamaa.

Usikubali Kukata Tamaa Kirahisi
 
Tangu 2019 mpaka sasa nasumbuka na msongo mkali wa mawazo, uoga ulipitiliza, panic attack, yaani nimekuwa kama mfu anaetembea, nilienda hospitali ya Mount Meru Arusha wakaniambia ni psychosis, wakanipa Haloperidol na Benzylhexol nikaanza kutumia ila zilinisaidia kwa wiki chache baada ya hapo hali ikawa mbaya zaidi ya mwanzo na nikawa nikitumia kichwa kinakuwa chepesi kupita kiasi kama nimelewa.

Nikaamua kuacha zile dawa kwa sasa naona sina muda mrefu wa kuishi, imechoka sana
Piga nyapi depresion itaondoka
 
Acha ku overthinking mawazo bila solution inapelekea depression so jitahid kuzungumza na watu mara kwa mara usikaee peke ako mdaa mwingi
Pole sana
 
Sina uhakika ila nadhan kufanya mazoezi na kuanza kutumia bangi kunaweza kukusaidia. Wenye experience on this, naskia bangi inawafanya watu waondokwe na msongo wa mawazo, kupotezea vitu na kupata solution kwenye nyakati ngumu. Just a thought though, don't take me serious
Mimi huwa nasema sana humu bangi iliokoa maisha yangu lakini watu hawachukulii serious
 
Tangu 2019 mpaka sasa nasumbuka na msongo mkali wa mawazo, uoga ulipitiliza, panic attack, yaani nimekuwa kama mfu anaetembea, nilienda hospitali ya Mount Meru Arusha wakaniambia ni psychosis, wakanipa Haloperidol na Benzylhexol nikaanza kutumia ila zilinisaidia kwa wiki chache baada ya hapo hali ikawa mbaya zaidi ya mwanzo na nikawa nikitumia kichwa kinakuwa chepesi kupita kiasi kama nimelewa.

Nikaamua kuacha zile dawa kwa sasa naona sina muda mrefu wa kuishi, imechoka sana
Tatizo haliwezi kutatuliwa bila kutibu chanzo. Kumbuka uhai ni muhimu kuliko kitu chochote.
Je; chanzo ni familiya; biashara; Cheo au mahusiano?. Ila yote Kwa yote; kumpata mwenye mapenzi ya dhati kwako atakupatia Tiba mbadala ya tija na utayasahau matatizo yote.
 
Tangu 2019 mpaka sasa nasumbuka na msongo mkali wa mawazo, uoga ulipitiliza, panic attack, yaani nimekuwa kama mfu anaetembea, nilienda hospitali ya Mount Meru Arusha wakaniambia ni psychosis, wakanipa Haloperidol na Benzylhexol nikaanza kutumia ila zilinisaidia kwa wiki chache baada ya hapo hali ikawa mbaya zaidi ya mwanzo na nikawa nikitumia kichwa kinakuwa chepesi kupita kiasi kama nimelewa.

Nikaamua kuacha zile dawa kwa sasa naona sina muda mrefu wa kuishi, imechoka sana


1735481133317.jpg


Huyu mwamba yupo kweli,,,,last seen yesterday. Ajitokeze haraka kuna wadau washajitoa kumsaidia kabisa.
 
Pole. Fanya meditation itakusaidia sana
Meditation inaleta suluhu ya kudumu ya suala lake..Tatizo la meditation ni kupata mtu wa kukuelekeza namna exactly inavyo fanyika..kazi ipo hapo.
 
Back
Top Bottom