Depression inanimaliza, sina muda mrefu wa kuishi

Ningekuwa nimejiondoa muda mrefu sana mkuu. Nilifanya suicidal attempt tatu lakin nashukuru Mungu aliyeniokoa katika zote izo mkuu
 
Pole sana ndugu yetu, hii hali uisikie tu kwa wenzako, naamini hapa utaipata msaada na usipuuzie kabisa.
Katika pita pita zako za maisha lazima kuna mambo umeyapitia na ndio chanzo, Kuna kushindwa kwa baadhi ya mambo na unashindwa kukubaliana na hiyo hali.
Kwanza kubaliana na kila badiliko au anguko la vitu ambavyo hukutarajia kukutokea, kumbuka hata unaowataminia au unachokitamani kiwe kilishawahi kupitia magumu.
Jichanganye na watu wennye maono na fanya Ibadan sana kwa imani yako.
Mwisho ukiweza badilisha mazingira, hama mji ukutane na watu wapya.
 

Haujasema shida yako! Tatizo lako ni nini? Linalosababisha hayo mawazo na stress?
 
Kwanza Unafaida Gani kwenye Jamii inakuzunguka na Taifa Kwa ujumla, tuanzie hapa, yaani wewe ni Mwalimu, Daktari, Nesi, Askali, Mkulima, Mfanyabishara, je una familia? Tuambie fani yako na inatumikaje kunufaisha Jamii. Bila hivyo kama wewe ni reject, yaani kibaka, mvuta bange, mla rushwa, jambazi, muuza unga au mla sembe, tukutakie punziko la mapema. Si vyema kutoa ushauri Kwa mtu alijikataaa mwenyewe.
 
Join kwenye gym yoyote iliyo karibu na ww itabadilisha uwezo wako wa kufikiria

Jikamue asubuhi na jioni

Huna kazi nenda gym
Umeachwa nenda gym
Unatatizo financially nenda gym

Akili imara huanza na mwili imara dawa sio solution la tatizo lako mindset na perspective ndio shida kwako switch the bend
 
Mkuu natamani sana baada ya Ujumbe huu uliouandika nenda kahudhurie Msiba mmoja tu na uage sura ya mwisho. Itakusaidia kujua Mwanadamu akishalala haamki tena. Tuwapiganie wenzetu wakiwa hai kabla hawajapoteza hamu ya kuishi. Haikupunguzii chochote kumtamkia mema huyu Jamaa.
 
Hongera sana Mkuu kwa kutokata Tamaa na kurejesha hamu ya kuishi! Vijana wenzio tunakuahidi kusimama nawe urejeshe kila kilocholiwa na Nzige katika Maisha yako. Mungu akujalie usimame tena na kutimiza Ndoto yako katika sekta ya Afya. Hakika utakuwa Mtaalamu Bora wa Afya kwa kuwa umepitia Maisha hayo. Naomba kufahamu uko Mkoa gani kila inapotokea nakuja Mkoa huo nifike kukutembelea walau kushare nawe kidogo Mungu anachotubariki kwenye utafutaji.
 
Ulitakiwa upate na folic acid na wangekuongezea muda wa kulala kwa amytriptiline. Hapo pia, ungepata na sehem ya kupoa na kusocialize na watu wazuri wanaofariji na kukufanya kua active hasa kiuchumi na kijamii kwenye michezo, burudani, mipira.

Unafanya kazi gani?
 
Una kazi au shughuli ya kukuingizia kipato. Depression sio ugojwa ni dalili za tatizo au matatizo yaliyo shindikana kutatuliwa. Kutibu dalili bila kujuwa chanzo cha tatizo hakuwezi kuponya tatizo. Swali la kujiuliza nini chanza cha depression. Mfano chanzo kinaweza kuwa kutoridhika hali yako ya maisha . Hali ya maisha mara nyingi inahusisha vitu vingi ikiwemo aina ya kazi, biashara, au shughuli inayo kuwezesha kupata kipato. Pia inahusisha mahusiano ya familia na jamii inayo kuzunguka. Hivyo ni baadhi ya maeneo ambayo unahitaji kushughulikia kabla ya kutumia dawa.
 
Pole sana Mkuu, Mungu asikuache na usiache pia kufatilia Kuna member wawili hapo mwanzo wapo tayari kukusaidia.
 
Ahsante sana mkuu.. kiukwel nimefarijika sana kuona kuna watu wanaoelewa hali hii.. binafsi nipo mkoa wa Rukwa nasoma chuo huku. Pia nitakutumia mawasiliano yangu inbox tuzidi kufahamiana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…