teh teh teh
"Holly ghost is code number of bible"
teh teh teh!...hallelujah
Heshima kwenu wadau,
Inawezekana hili swali likawa limejadiliwa sana hapa, ila nimejaribu kutafuta huo uzi nimeshindwa kuupata, swali langu ni hili hapa,
Je december 25 ambayo si siku ya chrismass ambayo twaambiwa alizaliwa kristo ni kweli alizaliwa siku hiyo au twaadhimisha tu kama kumbukumbu yake?
Kwa mujibu wa Biblia takatifu, Injili ya luka mtakatifu inasema " Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu.
28 Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.
29 Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
30 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.
kama maandiko matakatifu yanasema kuwa Maria mtakatifu alipata mimba mwezi wa sita manake tungetarajia kujifungua mwezi wa tatu au wa pili mwishoni.
Swali lingine ambalo ningependa kwa mwenye ujuzi ni je zamani walikua wanatumia kalenda gani kuhesabau siku? nadhani hapa ndipo ukweli wa mambo ulipo.
Naomba kufahamu kwa wenye ujuzi wa mambo ya kiroho na wanahistoria.
NA MUNGU AWABARIKI SANA.
Humu ndani mada kama hii huwa haipendwi kwa hiyo usishangae ikifungwa soon. Niliwahi kuleta mada kama hii kutoa elimu kwa upotoshaji mwingi unaofanywa kuhusu Christmass lakini topic ikaishia kufungwa. Lakini sio mbaya ujumbe ulifika na wengi wamepata elimu hii. Kiukweli hakuna ushahidi wowote wa maadiko kuhusu tar.25 dec kama ndiyo tarehe aliyozaliwa Yesu Kristo. Isipokuwa tarehe hiyohiyo 25 dec. ilikuwa ni sikukuu ya kipagani ya wababeli wakisherehekea kuzaliwa kwa mwana wa mungu wao Tamuz aliyeaminika kuwa mwana wa Nimrod ambaye alipokufa aliaminiwa kuwa alienda kwenye jua na mionzi ya jua ikamtia mimba malkia wa babeli aliyeitwa semiramis ndipo akamzaa tamuz( mungu mwana wa jua). Hii habari ya Nimrod kuishi kwenye jua ilienezwa na malkia baada ya mumewe kufa na baadae malikia akawa mjamzito. ili kuepuka hatia na aibu ya kuzaa nje ya ndoa ilibidi uongo utungwe kwa ustadi mkubwa kuwa Nimrod hakufa bali alienda kuishi kwenye jua na mionzi yake ndio iliyomtia mimba malkia semaramis na kumzaa mwana aliyepewa jina la tamuz. Hivyo wababeli na baadae rumi ya kipagani waliendelea kusherehekea siku ya kuzaliwa mungu mwana jua aliyeitwa tamuz katika tarehe 25.Dec. Hiyo ilikuwa sikukuu kubwa enzi hizo na katika siku hiyo wafalme walipewa mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa. rejea Yeremia 52:31-34.
Jambo la kusikitisha ni kuifanya sikukuu ya kipagani kuwa ni sikukuu ya kuzaliwa Mwana wa Mungu Mkuu Yesu Kristo. Kama ni kufuru, kizazi hiki kimepitiliza.
Tuanza kujibu swali moja moja..
Kuhusu mwezi wa sita (kwenye red hapo) unachojaribu kusema ni kuwa malaika alimtokea mwezi wa sita (kwa siku za leo tungesema june) so unadhani mpaka mwezi wa 12 mtoto atakua na miezi 6.. nimeona pia cc: LITONO nae amenguka kwenye huo mtego..
Miezi sita hapo siyo mwezi wa sita (june) au mwezi wa sita wa mwaka. ukitaka kueleweza anzia mlango wa 24 (luka 1:24) "Hata baada ya siku zile mkewe Elizabeth alichukua mimba akatawa MIEZI MITANO akasema..."
mwandishi anaendelea na tukio hilo la mstari wa 24, (limetenganishwa tu na mstari wa 25), ...baada ya kutawa miezi mitano, mwezi wa sita malaika akamtokea mariam.. kwa maana nyingine baada ya miezi 6 kupita tokea amtokee elizabethi" kwa kiingereza inasema in the sixth month..
kwa hiyo hapo uelewe kuwa siyo mwezi wa sita wa mwaka, ni mwezi wa sita baada ya tukio la eliza.. na ndio maana tunasema Yesu na Yohana mbatizaji wamepishana miezi 6.
Hakuna mtu/mkristo yeyote anayesema kuwa 25 ndiyo tarehe aliyozaliwa Yesu, utakua tu hujaelewa kama ambavyo watu wengi hawaelewi... hakuna mtu anayejua tarehe aliyozaliwa Yesu, hilo tunalifahamu.
kuhusu tahere 25. Ni kukumbuka siku ya kuzaliwa Yesu AU siku ya kukumbuka kuzaliwa kwa YESU.
to make it simple.... Wote tuna uhakika kuwa alizaliwa (nadhani hata ww unakubali) siku ndio hatujui, kwa hiyo tumeamua kutafuta siku moja ya Kuadhimisha au kukumbuka kuwa alizaliwa MASIHI (Mkombozi wetu) kwa sababu tuna uhakika kuwa kuna siku alizaliwa...
kwa mfano kama ingekua ni tarehe labda 10 october.. Je ungejali?? au pia ungekuja na theory nyingine
Labda kwa kukusaidia kama ww huamini katika kusherekea Christmas sio tatizo, wala sio amri wala sio shida, endelea tu na maisha,
Lakini pia hakuna sehemu yeyote inasema kuwa ni dhambi, sasa kwa nini wewe unakasirika na watu ambao wao wanasherekea
Yesu ajazaliwa Christmas ilo linajulikana sema dini yetu hii ni ya kipagani inaendana na mafundisho ya ki binaadamu ndio maana huwezi tofautisha na ushoga. Hakuna Mungu huku alikozaliwa yesu kwenyewe hakuna Ukristo iweje uwepo Roma ambapo hajawahi hata kufika?
Unaumwa.christmass,"the feast of the unconquered sun"
nini maana ya neno "christmas"?,christmass ni muunganiko wa maneno mawili "christ" na "mas"
christ ni kristo,lakini nini maana ya "mas"au mass?
mass:"
mass is service that is held to remember the death of any person for whom the mass is held"...
maana ya "mass" itakushangaza zaidi,kwahiyo unaposema merry christmass,unamaanisha "heri kifo cha kristo,..senseless!..tunafurahia kuzaliwa kwa yesu au kifo chake?...jibu ni kifo chake!
Asili halisi ya christmass ni hii;..Roman empire chini ya constantantine iliunganisha dini zote za kipagani pamoja na kikristo na kuunda kanisa linaloitwa Roman catholic,ili kuunganisha dini zote ilibidi waunganishe pia mafundisho yao,moja kati ya hayo mafundisho ni sherehe ya kifo cha mungu tammuzi ambaye alizaliwa 24-12 akafa usiku wa tarehe 25 december(ref;encyclopeda brittanica,volume 11)
SANTA =S-A-T-A-N,huyo ndiye father christmass,teh teh teh
zamani walikuwa wanatumia julian calender kabla ya gregorian calender!
Heshima kwako @RGforever
Naomba kabla hujachangia soma kwanza bandiko vizuri sana, Bible takatifu inasema bikira maria alipata mimba mwezi wa sita na yesu alizaliwa tarehe 25 december kwa maana ya miezi saba mbele baada ya kupata ujauzito bikira maria akajifungua mtoto yesu, nilichotaka kujua ni kwamba kwa sayansi mtoto anaezaliwa akiwa na miezi saba au sita ni ngumu sana kuishi sababu anakua ni njiti (hajatimiza miezi 9 )
Swali, Je tunasherehekea siku ambayo kweli yesu alizaliwa au ni watawala tu wa kale waliamua kuiweka hii siku kama kumbukumbu ya kuzaliwa kwake na haikuwa siku halisi?
Mkuu kama unaamini kwamba Bikra Mariam alibeba mimba bila kujamiana na mmewe kwa hiyo hakuna ajabu kuzaliwa kabla ujauzito haujafika miezi Tisa.
Hakuna mtu/mkristo yeyote anayesema kuwa 25 ndiyo tarehe aliyozaliwa Yesu, utakua tu hujaelewa kama ambavyo watu wengi hawaelewi... hakuna mtu anayejua tarehe aliyozaliwa Yesu, hilo tunalifahamu.
kuhusu tahere 25. Ni kukumbuka siku ya kuzaliwa Yesu AU siku ya kukumbuka kuzaliwa kwa YESU.
to make it simple.... Wote tuna uhakika kuwa alizaliwa (nadhani hata ww unakubali) siku ndio hatujui, kwa hiyo tumeamua kutafuta siku moja ya Kuadhimisha au kukumbuka kuwa alizaliwa MASIHI (Mkombozi wetu) kwa sababu tuna uhakika kuwa kuna siku alizaliwa...
kwa mfano kama ingekua ni tarehe labda 10 october.. Je ungejali?? au pia ungekuja na theory nyingine
Labda kwa kukusaidia kama ww huamini katika kusherekea Christmas sio tatizo, wala sio amri wala sio shida, endelea tu na maisha,
Lakini pia hakuna sehemu yeyote inasema kuwa ni dhambi, sasa kwa nini wewe unakasirika na watu ambao wao wanasherekea
Hakuna mtu/mkristo yeyote anayesema kuwa 25 ndiyo tarehe aliyozaliwa Yesu, utakua tu hujaelewa kama ambavyo watu wengi hawaelewi... hakuna mtu anayejua tarehe aliyozaliwa Yesu, hilo tunalifahamu.
kuhusu tahere 25. Ni kukumbuka siku ya kuzaliwa Yesu AU siku ya kukumbuka kuzaliwa kwa YESU.
to make it simple.... Wote tuna uhakika kuwa alizaliwa (nadhani hata ww unakubali) siku ndio hatujui, kwa hiyo tumeamua kutafuta siku moja ya Kuadhimisha au kukumbuka kuwa alizaliwa MASIHI (Mkombozi wetu) kwa sababu tuna uhakika kuwa kuna siku alizaliwa...
kwa mfano kama ingekua ni tarehe labda 10 october.. Je ungejali?? au pia ungekuja na theory nyingine
Labda kwa kukusaidia kama ww huamini katika kusherekea Christmas sio tatizo, wala sio amri wala sio shida, endelea tu na maisha,
Lakini pia hakuna sehemu yeyote inasema kuwa ni dhambi, sasa kwa nini wewe unakasirika na watu ambao wao wanasherekea
teh teeh teeeh eeeerh... .. .biblia ni moja na quran ni moja... .. . lakini kundi/dhehebu moja huona mafundisho yao ni bora kuliko ya wengine,
Hayo yote yalijulikana tangu awali ndio maana Bwana Yesu alitusihi tujiepushe na manabii wa uongo...kwa kuwa nao hutumia Biblia ila kwa kupotosha.
Heshima kwenu wadau,
Inawezekana hili swali likawa limejadiliwa sana hapa, ila nimejaribu kutafuta huo uzi nimeshindwa kuupata, swali langu ni hili hapa,
Je december 25 ambayo si siku ya chrismass ambayo twaambiwa alizaliwa kristo ni kweli alizaliwa siku hiyo au twaadhimisha tu kama kumbukumbu yake?
Kwa mujibu wa Biblia takatifu, Injili ya luka mtakatifu inasema " Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu.
28 Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.
29 Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
30 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.
kama maandiko matakatifu yanasema kuwa Maria mtakatifu alipata mimba mwezi wa sita manake tungetarajia kujifungua mwezi wa tatu au wa pili mwishoni.
Swali lingine ambalo ningependa kwa mwenye ujuzi ni je zamani walikua wanatumia kalenda gani kuhesabau siku? nadhani hapa ndipo ukweli wa mambo ulipo.
Naomba kufahamu kwa wenye ujuzi wa mambo ya kiroho na wanahistoria.
NA MUNGU AWABARIKI SANA.
Huna haja ya kuuliza watu, wewe sheherekea X-mass mwezi wa pili au wa tatu kama unavyoamini