S.M.P2503
JF-Expert Member
- Nov 25, 2008
- 2,421
- 4,344
Na vipi kuhusu metadata za radio call zao au hata metadata za simu zao za mikononi? Nazo hamna?Central pana CCTV camera pale??? Bombay la maji hamna itakuwa CCTV camera??
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na vipi kuhusu metadata za radio call zao au hata metadata za simu zao za mikononi? Nazo hamna?Central pana CCTV camera pale??? Bombay la maji hamna itakuwa CCTV camera??
Mama naye ni bonadamu huenda alipewa taarifa zilizipikwa kwa ustadi wa Siro, huenda naye akili ikamrudi baada ya kuona mwenendo wa kesi halisi.Kesho kama kawaida Yake
Yaan niivi , Hawa MAJAJI wanajua kabisa utetezi wako sahihi toka kesi ndogo ya Mwanzo na mapingamizi yalofata..
Mama yenu Samia aliiambia Dunia, wenzake na Mbowe wameshashitakiwa kwa Ugaidi...
Kwamba haonewii. Ni gaidiii..
Sasa ndugu zangu.. MAHAKAMA gani hayo nitakuja kuwapa ushindi akina Mbowe ??
Yaan RAIS AONEKANE HAKUA NA TAARIFA SAHIHI?? ALIDANGANYWA??
Yaan Rais Mzima , Dunia ijue hilo??
Thubutuu..MBOWE NA WENZAKE WATAKUTWA NA HATUA.
NA WATAFUNGWA !!.
Umeandika kwa hisia kali sana mkuu. Nawaza hapa kuhusu imani iliyokuwepo katika jamii zetu za Kiafrika.Nikupe siri moja ambayo watu wengi hawaifatilii.
Wakiendelea kufanya uonevu wa kiwango hiki wanachofanyiwa akina Mbowe.
Tena kwa kiburi,na zaidi kwa kutumia na kutegemea nguvu za dola,fedha ama mabavu waliyonayo.
Naye unayemuonea akawa hana namna ya kujitetea kwa namna yoyote ile.
Nakuhakikishia kwa kiapo.HAKI YA MUNGU,Mungu mwenyewe huingilia Kati kuja kujibu kwa niaba ya wanaoonewa..
Kwa kuthibitisha hilo la mtu "kumshudia" mtu mwingine uongo,yaani kutoa ushahidi wa uongo. Kama wafanyavyo hao mawakili wa serikali,majaji,mashahidi na Mapolisi.
Mungu alitunga Sheria kali(amri) isemayo usishuhudie uongo au usiseme uongo.
Kwa kuwa Wana nguvu watajiona hawajali,lakini subiri majibu ya Mungu.
Na bahati nzuri askari wamekiri kwamba walikuwa wanawasiliana wenyewe kwa wenyewe toka huko Rau madukani Mpaka Dar... ni kuiomba mahakamani itoe order kwa makampuni ya mitandao na mawasiliano ku release hizo metadata toka huko moshi... mienendo yote itajulikana tu...Hicho ndicho Jaji alipaswa kufanya. Ni muhimu haki kuonekana ikitendeka.
Mawakili wa utetezi wangeweza kupata ushahidi huo Tigo, Airtel, Vodacom, au Halotel for the sake of justice.
Kupokelewa kwa mtuhumiwa kituo tofauti au kutopewa chakula kwa wakati,bado hakufuti kosa la msingi kama limethibitika kutendwa na mhusika hizi zingine ni chenga kama za mpira, cha msingi na kinacholeta ushindi ni magoli.Kesi hii inayovutia hisia za wengi, zaidi ya weledi ilihitaji uhuru stahiki wa mhimili wa mahakama na uthubutu wa Jaji katika kutoa haki tupu na kwa mujibu wa sheria.
Pungufu ya hivyo tunakoelekea mahakama haitaweza kukwepa lawama.
Mezani tulipo kuna pingamizi ambalo kigezo chake kikuu ni kuwa mshitakiwa hakuwahi kufikishwa central police Dar.
"Detention register ya mahali ambapo mshitakiwa anadai hakuwahi kufikishwa ina thamani gani mahakamani katika hatua hii?
Katika hali kama hii, inapokelewa vipi kama ushahidi?
Katika hali kama hii inapokelewa kuthibitisha nini, kabla ya Jaji kujiridhisha kwanza ukweli halisi ni upi?
Katika hali kama hii Jaji anajiridhisha vipi nani anasema kweli kuhusu central police baina ya upande wa mashtaka na upande wa washitakiwa?
Haki ikitendeka itaonekana.
Haki ikiporwa kupitia visingizio pia itaonekana ikiporwa kama Mh. Jaji ataamua iwe hivyo.
Changamoto hizi zitufungue macho zaidi kuona tunahitaji katiba ya namna gani kwa hakika ili kuepukana nazo kabisa.
Kupokelewa kwa mtuhumiwa kituo tofauti au kutopewa chakula kwa wakati,bado hakufuti kosa la msingi kama limethibitika kutendwa na mhusika hizi zingine ni chenga kama za mpira, cha msingi na kinacholeta ushindi ni magoli.
Tuache porojo kama tuhuma ni ya kweli tusubiri mwisho wa kesi.
Na bahati nzuri askari wamekiri kwamba walikuwa wanawasiliana wenyewe kwa wenyewe toka huko Rau madukani Mpaka Dar... ni kuiomba mahakamani itoe order kwa makampuni ya mitandao na mawasiliano ku release hizo metadata toka huko moshi... mienendo yote itajulikana tu...
Kama Hilo haliwezekani, magari ya polisi yana kitabu cha mizunguko , ni kiasi cha kuomba hicho kitabu kujua kwamba lilitoka wapi kwenda wapi...
Pia gari lazima lijaze mafuta vituo vya mafuta, huko pia kuna cctv za kutosha ...
Ukija njiani kuja huku mbweni, au hata kwenda posta, kuna nanma nyingi tu kupata hizo data za ushahidi wa kisayansi..,
Hii kesi - utetezi wajumlishe sayansi na mazagazaga mengineyo... Pandora box lilisha funguliwa na prosecution kwa kumleta yule wa Tigo kuongelea miamala na wao utetezi lazima walete mtu wao ili tuione hiyo simu ilipokuwa inafanya hiyo miamala ilikuwa wapi- ndio umuhimu wa metadata...na tutajua tu siku hiyo huyo Mbowe pia alikuwa wapi... ni masuala ya ulinganifu tu... Sayansi ya simu za mikononi na metadata- yapaswa sasa zinyambuliwe ipasavyo- si mambo haya ya makaratasi na diary hadi mahakamani....