Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Nikamwambie mtu uhusiano wangu na Khadija ili anichore sababu ikiwa nini? Anitangaze madhabahuni? Yeye ni msafi kiasi gani? Najua anatembea na wangapi?
 
Si Kila dhambi.

Dhambi tajwa Zina maagano, masharti na NDOA za kipepo, dhambi hizo zinamweka mtenda kuwa mfungwa aliyenunuliwa, hivyo mtumishi ni muhimu ahusike.
Nakuelewa sana mkuu, na wala hauna nia ovu kama wengi wanavyodhani.....changamoto unachosema hakijaandikwa kwenye biblia.

pia kuna wengi ambao wanajua mabaya mengi ya watumishi kuelewa hizi hoja bila kuweka vifungu itakuwa shida.
 
Kuna mstari wowote unazungumzia punyeto?
(Mwanzo 38:1-25)

Mungu alimwua mtu mume aliyeitwa Onani, kosa lake ni kumwaga manii nje Ili asimpe mimba mke wa kakaye aliyefariki bila uzao.

Dhambi ya PUNYETO inaanguka katika category hiyo, ni kumwaga nje ya uke, kumwaga manii nje ya sehemu husika.

Zingatia maelekezo ya Mungu.

Ubarikiwe.
 
Nikamwambie mtu uhusiano wangu na Khadija ili anichore sababu ikiwa nini? Anitangaze madhabahuni? Yeye ni msafi kiasi gani? Najua anatembea na wangapi?
Mungu ameelekeza kumwona mtumishi wa Mungu wa Kweli aliyeokoka, mwenye BUSARA.

Ikiwa mtumishi wako ni mhunni, hama hapo haraka, anawapeleka KUZIMU wote mnaoabydu hapo.

Amen
 
Nakuelewa sana mkuu, na wala hauna nia ovu kama wengi wanavyodhani.....changamoto unachosema hakijaandikwa kwenye biblia.

pia kuna wengi ambao wanajua mabaya mengi ya watumishi kuelewa hizi hoja bila kuweka vifungu itakuwa shida.
Jini mahaba Si hadithi ni HALISI, kumwondoa once and for all, mtumishi lazima ahusike, dhambi tajwa nyingi hapo zinahusiana na zinaa,

Nikikupa maandiko utaamini?

Mada hii imeleta mtikisiko sana humu, inaonekana, wengi wanafanya mambo hayo na hawaambiwi KWELI huko wanakoabudu!!!
 
Mungu ameelekeza kumwona mtumishi wa Mungu wa Kweli aliyeokoka, mwenye BUSARA.

Ikiwa mtumishi wako ni mhunni, hama hapo haraka, anawapeleka KUZIMU wote mnaoabydu hapo.

Amen
Kwa mswahili wa bongo utampima kwa kipimo gani kuwa ameokoka na ana busara? Injili ya leo imebaki usanii na wizi, ungamo la kweli liko mokonomi mwako, kajifungie chumbani mwako muombe msamaha Mungu kuliko kuigiza kwa hao matapeli
 
Kwa mswahili wa bongo utampima kwa kipimo gani kuwa ameokoka na ana busara? Injili ya leo imebaki usanii na wizi, ungamo la kweli liko mokonomi mwako, kajifungie chumbani mwako muombe msamaha Mungu kuliko kuigiza kwa hao matapeli
WATUMISHI wanyoofu wakweli waliookoka wapo ingawa ni Wachache.

Mungu akitoa maelekezo, ni kutii basi!!

Uamuzi ni wako.
 
China wanatoa Kwa miungu Yao.

Sadaka ni Amri, Ulimwengu wa Nuru na Giza sadaka ni LAZIMA.

Uzuri umesoma ujumbe, ni uamuzi wako kutekeleza.

Amen
 
Hebu soma Warumi 3:23 inasema wote tumefanya dhambi na kupungukiwa utukufu wa Mungu.

Hamna sehemu inayosema nyie manabiì ndio mnaotuondolea dhambi. Yesu alikufa mtini kwa ajili ya ondoleo letu la dhambi.

Wewe sema tu unataka sadaka tukupe akanywe bia na wanawake zako
 
Yeye nani?ONGEA NA MUNGU IMEISHA.YEYE MWENYEWE ANA DHAMBI ZAKE.AJUE ZANGU ZA NINI?
Message sent,

Tafuta mtumishi wa Kweli mtakatifu asiye mzinzi, wapo wengi!!

Ubarikiwe.
 
Hakuna Mahali nimeelekeza watu waje kwangu.

Nimesema tafuta mtumishi wa Mungu wa Kweli.

Yesu alikufa na Damu yake ni ondoleo la dhambi, ni Kweli.

Yesu hakuzuia watu wasitoe sadaka baada ya kufufuka, sadaka ni shukrani, pia sadaka Si lazima utoe pesa kama huna, toa moyo wako mnyoofu ikiwa huna pesa, ni sadaka pia.

Ubarikiwe.
 
Sasa kama ukihifadhi kwenye kopo halafu baadae unamwagia kwenye uke inakuwaje?
 
Sadaka ni kawaida, ni shukrani tu, ni msisutizo tu, kuwa tusiende nyumbani mwa BWANA mikono mitupu. Lakini ikiwa huna, moyo wako mnyoofu ni sadaka pia.sadaka Si mbadala wa Damu ya Yesu.

Usichanganye mambo mtumishi.
 
Neno la Mungu linasema tumuombe Mungu kupitia Yesu Kristo. Hayo ya watumishi wa Mungu ni yako.
 
Neno la Mungu linasema tumuombe Mungu kupitia Yesu Kristo. Hayo ya watumishi wa Mungu ni yako.
Yesu alivyomtokea Sauli, alimwelekeza aende Kwa mtumishi.

Yesu aliacha mitume na viongozi wa Kanisa Ili wawasaidie wachanga kiroho kukua.

Asomaye na afahamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…