Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

(waebrania 12:14)

Tafuteni Kwa bidii kuwa na Amani na watu wote na huo utakatifu ambao HAPANA atakayemwona Mungu asipokuwa nao.

Dhambi ya UZINZI huwezi pata Amani ukitubu gizani mwenyewe, lazima utafute namna ya kuweka mambo sawa,

Ndomana mtumishi wa Mungu wa Kweli lazima ahusike.

Amen
Umepata wapi hili
Maana tunachotaka ni kile Mungu anachoagiza katika neno lake na sii hisia za mtu.
Hakuna ambaye yupo tayari kupotea. Dhambi zote ni sawa na inapaswa zitubiwe.
Kama kuna iliyotofautishwa kwa mujibu wa neno la Mungu ni dhambi ya kumkufuru roho mtakatifu.
Sasa haya makosa mengine yanayopangwa mafungu mafungu ni wapi yameainishwa katika neno?
Tuanzie hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umepata wapi hili
Maana tunachotaka ni kile Mungu anachoagiza katika neno lake na sii hisia za mtu.
Hakuna ambaye yupo tayari kupotea. Dhambi zote ni sawa na inapaswa zitubiwe.
Kama kuna iliyotofautishwa kwa mujibu wa neno la Mungu ni dhambi ya kumkufuru roho mtakatifu.
Sasa haya makosa mengine yanayopangwa mafungu mafungu ni wapi yameainishwa katika neno?
Tuanzie hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Rudi kusoma thread, nimeweka maandiko,
 
Wapenda showoffs hao, wao kujionyesha ndio fahari yao na mara nyingi watu wa kaliba ya mleta mada hupenda kujikweza. Kuna baadhi ya watu hawaridhiki ikiwa jamii inayowazunguka haijaona / shuhudia mtu huyo kafanya jambo fulani.

Maombi ni uhuru wa bendera, ukombozi wa fikra ni uhuru wa maendeleo.
Nakubal kamanda
 
HATIA itaendelea kuwepo Hadi uwatafute watumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi
Yohana 5:45
Msidhani kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba; yuko anayewashitaki, ndiye Musa, mnayemtumaini ninyi.
 
Kama kuna mtu angekua amewahi kufa na kufufuka kutuelezea yaliyojiri baada ya kwenda huko ingekua noma sana. Mnaabudu watumishi kuliko wanavyostahili
 
Kama kuna mtu angekua amewahi kufa na kufufuka kutuelezea yaliyojiri baada ya kwenda huko ingekua noma sana. Mnaabudu watumishi kuliko wanavyostahili
Soma " Live Kutoka kuzimu - Rabbon"
 
Imeandikwa tukiziungama dhambi zetu yeye ni mwaminifu navwa haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote, haijasema ukienda kuombewa kwa mtumishi fulani, utoe na sadaka.
Msamaha wa Mungu tunaupokea bure kwa njia ya imani ya Yesu Kristo. Hakuna msamaha leo hii unaopatikana kwa kutoa sadaka, huo ni wizi na udanganyifu tu.
Yesu Kristo alikwisha lipa gharama ya dhambi za wanadamu wote. Hatuhitaji tena kutoa sadaka au dhabihu kwa ajilibya maovu tunayofanya.
Mwanadamu utatoa sadaka gani itakayozidi ya Yesu kujitoa uhai wake mwenyewe ili wewe usamehewe?
Kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi zako ni kuidharau dhabihu ya Yesu kwamba haitoshi. Yaani hivyo vihela vyako unavifanya kuwa bora kuliko damu au uhai wa Yesu uliotolewa kwa ajili yetu?
Leo tunatoa sadaka kama shukrani tu ya wokovu tuliopewa bure, sio kwa ajili ya kutafuta msamaha wa dhambi.
Njoo kwa Yesu upokee msamaha wa dhambi zakobzote bure, kwa njia ya imani tu
 
Imeandikwa tukiziungama dhambi zetu yeye ni mwaminifu navwa haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote, haijasema ukienda kuombewa kwa mtumishi fulani, utoe na sadaka.
Msamaha wa Mungu tunaupokea bure kwa njia ya imani ya Yesu Kristo. Hakuna msamaha leo hii unaopatikana kwa kutoa sadaka, huo ni wizi na udanganyifu tu.
Yesu Kristo alikwisha lipa gharama ya dhambi za wanadamu wote. Hatuhitaji tena kutoa sadaka au dhabihu kwa ajilibya maovu tunayofanya.
Mwanadamu utatoa sadaka gani itakayozidi ya Yesu kujitoa uhai wake mwenyewe ili wewe usamehewe?
Kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi zako ni kuidharau dhabihu ya Yesu kwamba haitoshi. Yaani hivyo vihela vyako unavifanya kuwa bora kuliko damu au uhai wa Yesu uliotolewa kwa ajili yetu?
Leo tunatoa sadaka kama shukrani tu ya wokovu tuliopewa bure, sio kwa ajili ya kutafuta msamaha wa dhambi.
Njoo kwa Yesu upokee msamaha wa dhambi zakobzote bure, kwa njia ya imani tu
Hujaelewa thread. Rudia tena kusoma Hadi mwisho.
 
Mchawi akitubu mwenyewe anasamehewa, Damu ya Yesu Ina samehe wote,

Ila kujitenga na maagano ya kuzimu ya shetani ya kichawi Ili yasimfuatilie tena, mtumishi lazima ahusike.

Msibishe.
Mzee unachopaswa ni kuijenga imani yako kupitia kushirikiana na wengine na kuunganika katika maombi ya pamoja, thats why ukishatoka kwenye hayo masuala ni ngumu kusimama mwenyewe kwani unaiuwa haujajua kuomba

Lakini sio unachosema ya kuwa mpaka mchungaji awepo kuvunja maagano, ni wewe binafsi kuvunja hayo maagano

Ikiwa unang'ata na kupuliza yataendelea kujirudia
 
Mzee unachopaswa ni kuijenga imani yako kupitia kushirikiana na wengine na kuunganika katika maombi ya pamoja, thats why ukishatoka kwenye hayo masuala ni ngumu kusimama mwenyewe kwani unaiuwa haujajua kuomba

Lakini sio unachosema ya kuwa mpaka mchungaji awepo kuvunja maagano, ni wewe binafsi kuvunja hayo maagano

Ikiwa unang'ata na kupuliza yataendelea kujirudia
Ubarikiwe.
 
Cain alipomuua Abel ilikuwa wivu tu. Sasa Cain alipohukumiwa kwenda kutangatanga huko duniani. Mnadhani nyie ni kizazi gani? Kama unahangaika wewe ni wa Cain, na hayata-isha. Kama unakula kivulini wewe ni wa Abel kula na kunywa raha milele, wenye wivu wajinyonge.
Haya mambo sometimes mi naona siasa tu hizi.
 
Cain alipomuua Abel ilikuwa wivu tu. Sasa Cain alipohukumiwa kwenda kutangatanga huko duniani. Mnadhani nyie ni kizazi gani? Kama unahangaika wewe ni wa Cain, na hayatisha. Kama unakula kivulini wewe ni wa Abel kula na kunywa raha milele, wenye wivu wajinyonge.
Haya mambo sometimes mi naona siasa tu hizi.
Neno la Mungu ni HALISI.

BIBLIA ni Pumzi ya Mungu katika maandishi.

Ubarikiwe.

Amen
 
Salaam shalom.

INTRODUCTON.

Imeandikwa, Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote.( 1 Yoh 1:9).

Dhambi ni kutotii, kwenda kinyume na maelekezo ya Mungu. Na Roho mtakatifu yupo kutukumbusha dhambi zetu Ili tuzitibie Ili tuendelee kuwa WATAKATIFU.

DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:


1. ZINAA NA UASHERATI.

UASHERATI ni kufanya Tendo la zinaa na mtu nje ya NDOA asiye mkeo au mumeo.

UZINZI ni kufanya tendo la uchafu, zinaa kabla ya Kuoa au Kuolewa.

Ukizini na mke wa mtu au mume wa Mtu, usijidanganye kuwa ukitubu sirini utasamehewa, HATIA itaendelea kuwepo Hadi uwatafute watumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. Watumishi Wana BUSARA ya kusuluhisha dhambi hiyo pande zote mbili Ili ufunguliwe.

Kuzini na mke wa mtu, faini ya juu ni kulipa Mahari aliyotoa muoaji Ili akusamehe, kushirikisha mtumishi ni kutumia BUSARA ya Mungu Ili muibiwa mke aridhie kukusamehe kutomlipa, au akupunguzie faini.

(Mithali 6:20-35,) UZINZI hufunga NAFSI, Amri ya Mungu usizini (Kumbukumbu la torati 5:1-21)

2. USHOGA.

Ikiwa uliwahi kuwa shoga, ukaamua kuacha, kamwe usitubu sirini na kuishiwa hapo, USHOGA huambatana na mapepo na kufungwa NAFSI, mfungwa kamwe hawezi jifunguanpingu mwenyewe, unawahutaji watumishi wa Kweli Ili UOMBEWE na kuwekwa huru, sadaka ni LAZIMA Ili itolewe huko. ( Mwanzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke makusudi Ili asizae na mke aliyepewa.

3. USAGAJI.

Mwanamke pia aliyewa kufanya dhambi hiyo, huwezi kufunguliwa na Utumwa na HATIA hiyo pekeako Kwa kutubu sirini, nenda Kwa watumishi wa Kweli, Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. mwanzo 38:9-10, Onani aliuwawa Kwa dhambi hiyo, ( kumbukumbu la torati 5:1-21) Amri za Mungu Usiue.

4. PUNYETO/ KUJICHUA.

Ikiwa uliwahi kujichua, ukaamua kuacha, unahitaji kwenda Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi Ili ufunguliwe, Mpiga PUNYETO ni mfungwa, ni mke au mume wa Roho chafu katika Ulimwengu wa Roho, hivyo kufunguliwa ni LAZIMA utoe sadaka, uvunje NDOA chafu hiyo ya kiroho na hati ya NDOA chafu ya kiroho iondolewe, usipofanya hivyo, unajidanganya. Mbinguni huingii ng'o!! (Mwanzo 38:1-25) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke Ili asizae na mke wa marehemu kaka yake.
Neno Hilo hapo juu ni ROHO. Amen.

5.MWANAMKE KUOA MWANAMKE/MWANAUME KUOA MWANAUME MWENZIE.

Kutubu dhambi hii sirini bila watumishi wa Mungu ni kujidanganya. Chukua sadaka, nenda Kwa mtumishi, Sema Kweli Ili UOMBEWE na kufunguliwa, NDOA haramu ivunjwe na ufungwa wako kiroho uondolewe. ( Mwanzo 38:9-10, (Mithali 6:20-35)Amen.

6. ORAL SEX.

Ikiwa uliwahi kushiriki oral sex, kunyonya au kuramba Kwa mdomo sehemu za Siri za mwanamke au Mwanaume na ukatambua ni DHAMBI, ukaacha, Bado u kifungoni.

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli wa Mungu ufunguliwe na Mungu.

(1 Wakorintho 6:9-11), (Ufunuo wa Yohana 21:8) (Mzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda Tendo la NDOA kinyume.

7. ABORTION./ UTOAJI MIMBA/ KUFUNGA UZAZI/ KUTUMIA VIDONGE VYA KUPANGA UZAZI.

Kimbia haraka Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli ,beba sadaka kulingana na uwezo wako, UOMBEWE ufunguliwe.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Usiue ni Amri ya Mungu.

Ukipuuza Utakataliwa GETI la Mbinguni.

9. IKIWA ULIWAHI TUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME/ KIKE.

(Mwanzo 38-9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda kinyume na Utaratibu wa Tendo la NDOA na taratibu za UZAZI alizoweka Mungu.


Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.

10. MAUAJI.

Ikiwa uliwahi kuua bila kukusudia ,ukahukumiwa JELA ukatoka, ikiwa uliua Kwa Siri na hukubainika, ikiwa ulishiriki kuua, usijidanganye kuwa unaweza kutubu sirini, HATIA Ili ikuondoke uwe na Amani, Tafuta kiongozi wa Mungu wa Kweli mwenye BUSARA za Mungu, akuongoze Cha kufanya, utoe pia sadaka ya Ukombozi. ( Acts 9:3-6) Sauli alikuwa mwuaji, Yesu alimwelekeza aende Kwa mtumishi.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Mungu ameamrisha " Usiue".

11. IBADA ZA SANAMU, KUSHIRIKI IBADA ZA WAFU NA KUTOA SADAKA KWA MIZIMU KIMILA NK NK.

Kushiriki Ibada za KIMILA na Kutoa sadaka Kwa Roho za kishetani za Mababu, ni DHAMBI pia, ni kufungwa ni Utumwa ambao huwezi kujifungua pekeako.

(Mithali 6:20-35) kifungo Cha NAFSI sababu Ibada ya sanamu ni UZINZI kiroho mbele za Mungu, ( UFUNUO 21:8, (1 korinthians 6:9-11) watendao uchawi na Ibada ya sanamu watatupwa Jehanum.

Ukiamua kuacha na kuokoka, hatua inayofuata ni kushirikisha watumishi kukusaidia kukutenga na madhabahu hizo.

Sadaka ni LAZIMA, sababu, Ulimwengu wa Nuru na Giza sadaka ni inevitable. Amen

HITIMISHO.

Dhambi nilizotaja hapo juu, ni baadhi tu ya dhambi ambazo huwezi tubu pekeako, zimetajwa sawasawa na Ruhusa ya Roho mtakatifu Kwa mtumishi wake sawasawa na ufunuo wake apendavyo.

NB: Si DHAMBI zote zinahitaji kuona mtumishi wa Kweli kukusaidia kufunguliwa pingu za dhambi, ni baadhi ya dhambi ambazo Zina vifungo na attachment na maagano ya kipepo na kishetani.

ANGALIZO: Sadaka tutoazo Si Kwa ajili ya kununua Muujiza, au kununua Msamaha wa Mungu, Yesu msalabani alikwisha maliza yote Kwa Damu yake msalabani. Sadaka tunatoa kama shukrani tu na kuonyesha Upendo Kwa Yale Mungu alikwisha tutendea.

Mungu awabariki.

Source: Nabii Justine Ibrahim, U-Tube., Promover Tv channel U-Tube.

Ikiwa hujampokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wako, fuatisha Sala hii,

EE YESU, NINAKIRI KWAKO KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU,ULIANDIKE KATIKA KITABU CHA UZIMA, NINAOMBA UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI, NIWEZESHE NIISHI MAISHA MATAKATIFU.

Ameen
Kati ya hizo 10 ulizoandika, huyo mtumishi unayeenda kutubu kwake, ana mojawapo
 
Rudi kusoma thread, nimeweka maandiko,
Unajua fundisho la kikristo kibibilia liko hivi.
Mdhambi huziungama dhambi zake kwa Mungu hadharani lakini kisiri na kubatizwa ambapo sasa hilo humfanya kuwa mmoja wa waamini aliyepokea vipawa vya roho mtakatifu.
Sasa ndani ya waamini kama mtu atahafilika na kutenda ndivyo sivyo inaelekezwa :
Moja, jamba la dhambi alilofanya ikiwa wewe mwamini umemwona mfuate na kumweleza error yake akitubu , umempata laa hakutaka kutubu, mchukue ndg mwine pamoja nawe na akitubu mmempata.
Lakini akikaidi liharifu kanisa(uongozi).
Ataitwa na kuulizwa na akikubali kughairi uovu wake mmempata lakini akikaidi basi mhesabuni kama mmataifa kwa maana kwamba mmemkabidhi kwa shetani amfundishe.
Sii kwamba mmemfukuza kwa Mungu kwani mtu huyo baada ya kipigo anaweza kurudi kutengeneza na kumrudia Bwana.
Hakuna mahali katika ukristo palipoagizwa muamini kwenda kwa kasisi kufanyiwa upatanisho kwa kulipa chochote kama mbadala wa dhabihu.
Dhabihu ni moja tu iliyokwisha tolewa nayo ni damu ya mwana kondoo Kristo Yesu.
Yanayozidi hapo yanatoka kwa wale makristo ambao maandiko yanakiri yatawapoteza wengi hata yamkini( kama ingeliwezekana) wateule.
Uzuri mteule haiwezekani kwake kupotezwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua fundisho la kikristo kibibilia liko hivi.
Mdhambi huziungama dhambi zake kwa Mungu hadharani lakini kisiri na kubatizwa ambapo sasa hilo humfanya kuwa mmoja wa waamini aliyepokea vipawa vya roho mtakatifu.
Sasa ndani ya waamini kama mtu atahafilika na kutenda ndivyo sivyo inaelekezwa :
Moja, jamba la dhambi alilofanya ikiwa wewe mwamini umemwona mfuate na kumweleza error yake akitubu , umempata laa hakutaka kutubu, mchukue ndg mwine pamoja nawe na akitubu mmempata.
Lakini akikaidi liharifu kanisa(uongozi).
Ataitwa na kuulizwa na akikubali kughairi uovu wake mmempata lakini akikaidi basi mhesabuni kama mmataifa kwa maana kwamba mmemkabidhi kwa shetani amfundishe.
Sii kwamba mmemfukuza kwa Mungu kwani mtu huyo baada ya kipigo anaweza kurudi kutengeneza na kumrudia Bwana.
Hakuna mahali katika ukristo palipoagizwa muamini kwenda kwa kasisi kufanyiwa upatanisho kwa kulipa chochote kama mbadala wa dhabihu.
Dhabihu ni moja tu iliyokwisha tolewa nayo ni damu ya mwana kondoo Kristo Yesu.
Yanayozidi hapo yanatoka kwa wale makristo ambao maandiko yanakiri yatawapoteza wengi hata yamkini( kama ingeliwezekana) wateule.
Uzuri mteule haiwezekani kwake kupotezwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ikirudi kusoma thread na comments zangu ZOTE Kwa utulivu, Wala hata hakipo Cha kubishana, zaidi ya kutii na kulifanyia KAZI.

Soma Kanisa la kwanza lolivyoenenda kitabu Cha Matendo ya mitume, watumishi walivyoshiriki kulijenga Kanisa nk nk, ,,
 
Ikirudi kusoma thread na comments zangu ZOTE Kwa utulivu, Wala hata hakipo Cha kubishana, zaidi ya kutii na kulifanyia KAZI.

Soma Kanisa la kwanza lolivyoenenda kitabu Cha Matendo ya mitume, watumishi walivyoshiriki kulijenga Kanisa nk nk, ,,
Hakuna dhabihu iliyopelekwa kwa hao mitume kwa ajili ya upatanisho.
Kama ipo nionyeshe nipate kupona.
Mimi ni mwanafunzi daima

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hujaelewa thread. Rudia tena

Hujaelewa thread. Rudia tena kusoma Hadi mwisho.
Nimeelewa sana. Kwenye post yako umeweka orodha ya dhambi ambazo unasema mtu akizifanya hataweza kusamehewa mpaka amwone mtumishi wa Mungu, tena akiwa na sadaka ya ukombozi. Mimi nasema hivi, hiyo sio kweli. Mtu yeyote akiamua kumrudia Bwana Yesu, hata kama awe amefanya maovu ya namna gani, Bwana Yesu ATAMSAMEHE BURE, bila ya kuhitaji kuombewa na mtu mmoja. Neno la Mungu linafundisha kuwa, mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ni mmoja tu, naye ni YESU. Kama mpatanishi ji Yesu tu, huyo mtumishi anayetaka watu wakamwone ni wa kazi gani?
Tunapokea msamaha wa dhambi bure kwa njia ya imani tu. Hiyo sadaka ya ukombozi ni ya kazi gani wakati Yesu alishajitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi za watu wote, pamoja na hizo ulizozitaja.
Kwa hiyo unataka kutuambia kuwa dhabihu ya Yesu haiwezi kumfanya mtu akasamehewa dhambi ya uzinzi au ushoga? Mwanadamu atatoa shilingi ngapi ili izidi thamani ya uhai wa Yesu?
 
Back
Top Bottom