ITR
JF-Expert Member
- Sep 22, 2022
- 6,096
- 16,390
Kama kichwa cha mada husika kinavyo sema hapo juu, siku hizi kuna dhana inayo sema eti kabla ya kuoana ni lazima kuchunguzana ili mjuane ndo muoane eti ndo ndoa yenu itakuwa imara,kwa jina lingine tuite uchumba sugu.
Lakini cha kushangaza kwenye huu ulimwengu wa kisasa ambao watu wana chunguzana miaka kabla ya kuoana ndo kipindi ambacho ndoa zetu zimejaa kila aina ya upuuzi na uchafu kuliko wakati wowote.
Mm ninacho amini mme au mke sahihi huwa ana kuja automatically kwenye maisha yako, na uchumba sugu hauna mahusiano yeyote na kupata mtu sahihi, na ndio maana kuna watu walioana baada ya kujuana ndani ya miezi 3 tu na ndoa zao ni imara na zenye furaha mpaka sasa,hali yakuwa kuna wengine walidumu kwenye uchumba miaka 5 lakini baada ya kuoana ndoa hata mwaka haikumaliza.
Hili suala la uchumba sugu mabinti ndo wahanga wakubwa, kiufupi lime waliza mabinti wengi lakini cha kushangaza hawajifunzi,wanaume wamekuwa wakitumia kisingizio cha tuchunguzane tujuane kuwageuza mabinti za watu kuwa kipozeo cha nyege zao yaani sex toy.
Siku hizi imekuwa kawaida sana kukuta kijana amekaa na binti wa watu kwenye mahusiano zaidi ya miaka 3,4,5,6 hataki kumuoa wala hataki kumuacha kwa kusingizio cha kumchunguza,lakini akitaka kuoa ana muacha huyo aliye dumu naye miaka kwa madai ya kumchunguza anaenda kuoa mwanamke mwingine ambaye wamekutana miezi 2 tu iliyo pita na ambaye wenda hata kumtongoza hakumtongoza bali aliunganishiwa na ndugu zake.
Binti hakuna mwanaume anaye kupenda atakuweka uchumba sugu bila sababu za msingi.
Ukiona umekaa kwenye mahusiano na mwanaume mwaka mzima bila kuonesha dalili yeyote ya kutamani kuishi na ww hiyo ni alam ya hatari kwako ,ukiwa mjinga atakula mbususu yako miaka zaidi ya 5 alafu utakuja kusikia ameoa binti kutoka kwenye nyumba ya jirani ambaye hata mbususu yake hajawahi kuiona.
Alafu utabaki kulaumu na kuita wanaume mbwa kumbe ww ndo mjinga na mpumbavu.
Madhara ya uchumba sugu yapo sehemu zote lakini nimeangazia upande wa wanawake kwa sababu wao ndo waathika wakubwa katika hili, lakini pia kuna wanaume nao wamelizwa na huu uchumba sugu japo ni kwa uchache.
Mfano mwanaume unaweza kuta una mpenda mwanamke na unawekeza kwake kwa kuamini atakuwa mkeo lakini kila ukigusia suala la kuoana ana ruka km100 kumbe yupo kwako kwa misheni maalumu tu ikisha kamilika anakimbia na kwenda kuolewa na mwanaume wa ndoto zake ana kuacha kwenye mataa na majuto makubwa.
Kiufupi kabla ya kuanza mahusiano ambianeni ukweli lengo la mahusiano yenu ili mtu kama ana kubali ajue anakubali mahusiano ya aina gani na sio mtu unadanganya kumbe ww una lengo lingine tofauti na makubaliano yenu.
Mkifanya hivyo mtaepusha visasi vya kurogana na kuuana.
Lakini cha kushangaza kwenye huu ulimwengu wa kisasa ambao watu wana chunguzana miaka kabla ya kuoana ndo kipindi ambacho ndoa zetu zimejaa kila aina ya upuuzi na uchafu kuliko wakati wowote.
Mm ninacho amini mme au mke sahihi huwa ana kuja automatically kwenye maisha yako, na uchumba sugu hauna mahusiano yeyote na kupata mtu sahihi, na ndio maana kuna watu walioana baada ya kujuana ndani ya miezi 3 tu na ndoa zao ni imara na zenye furaha mpaka sasa,hali yakuwa kuna wengine walidumu kwenye uchumba miaka 5 lakini baada ya kuoana ndoa hata mwaka haikumaliza.
Hili suala la uchumba sugu mabinti ndo wahanga wakubwa, kiufupi lime waliza mabinti wengi lakini cha kushangaza hawajifunzi,wanaume wamekuwa wakitumia kisingizio cha tuchunguzane tujuane kuwageuza mabinti za watu kuwa kipozeo cha nyege zao yaani sex toy.
Siku hizi imekuwa kawaida sana kukuta kijana amekaa na binti wa watu kwenye mahusiano zaidi ya miaka 3,4,5,6 hataki kumuoa wala hataki kumuacha kwa kusingizio cha kumchunguza,lakini akitaka kuoa ana muacha huyo aliye dumu naye miaka kwa madai ya kumchunguza anaenda kuoa mwanamke mwingine ambaye wamekutana miezi 2 tu iliyo pita na ambaye wenda hata kumtongoza hakumtongoza bali aliunganishiwa na ndugu zake.
Binti hakuna mwanaume anaye kupenda atakuweka uchumba sugu bila sababu za msingi.
Ukiona umekaa kwenye mahusiano na mwanaume mwaka mzima bila kuonesha dalili yeyote ya kutamani kuishi na ww hiyo ni alam ya hatari kwako ,ukiwa mjinga atakula mbususu yako miaka zaidi ya 5 alafu utakuja kusikia ameoa binti kutoka kwenye nyumba ya jirani ambaye hata mbususu yake hajawahi kuiona.
Alafu utabaki kulaumu na kuita wanaume mbwa kumbe ww ndo mjinga na mpumbavu.
Madhara ya uchumba sugu yapo sehemu zote lakini nimeangazia upande wa wanawake kwa sababu wao ndo waathika wakubwa katika hili, lakini pia kuna wanaume nao wamelizwa na huu uchumba sugu japo ni kwa uchache.
Mfano mwanaume unaweza kuta una mpenda mwanamke na unawekeza kwake kwa kuamini atakuwa mkeo lakini kila ukigusia suala la kuoana ana ruka km100 kumbe yupo kwako kwa misheni maalumu tu ikisha kamilika anakimbia na kwenda kuolewa na mwanaume wa ndoto zake ana kuacha kwenye mataa na majuto makubwa.
Kiufupi kabla ya kuanza mahusiano ambianeni ukweli lengo la mahusiano yenu ili mtu kama ana kubali ajue anakubali mahusiano ya aina gani na sio mtu unadanganya kumbe ww una lengo lingine tofauti na makubaliano yenu.
Mkifanya hivyo mtaepusha visasi vya kurogana na kuuana.