Dhana ya udini, ukabila na ukanda wa CHADEMA

Dhana ya udini, ukabila na ukanda wa CHADEMA

HOJA Y KUINGIA MSITUNI AISEE NAHISI BADO IPO.
MIE MWAKANI NASEPA ZANGU HATA RWANDA.

JAMAA KISHAAPA Lazma aingie porini© hata kitambi kikinasa kwenye miiba
 
wenye chama wenyewe wanajijua, pole yako ndugu,

asante
 
wenye chama wenyewe wanajijua, pole yako ndugu,

asante

Huyo mleta mada ndo kilaza mbowe mwenyewe hivyo usishangae anavyokuja kutoa povu hapa. Anataka kutufanya vipofu kana kwamba hata kupapasa hatujui. Wewe mbowe tuondolee shombo la ukabila wenu hapa.
 
Kuna Propaganda nyingine za Kitoto kbs na sijui km wanaozitoa wana "akili timamu". Mtu anatoka mapovu kupotosha CHADEMA ni chama cha wachaga.. hivi kweli amereason?

Chama kina wabunge kila kona ya nchi lakini kinaitwa cha wachaga. Chama kina wabunge Musoma, Mwanza, Arusha, Mbeya, Singida, Dar, Kigoma, Iringa kinaitwa cha Wachaga. Chama kina madiwani Songea, Shinyanga, Singida, Moshi, Tanga, Morogoro, Pwani, Geita, Simbawanga, Mpanda eti still ni cha wachaga.

Uchaguzi mdogo wa udiwani uliopita CHADEMA ilishinda kiti cha Idiwani Njombe mjini kilichokuwa chini ya CCM. Eti bado kinaitwa cha wachagga. Hivi hadi wabena nao siku hizi ni wachaga? Akili ndogo bhana.!!

Mbona hamsemi UDP ni chama cha wasukuma kwa sababu kipo Bariadi tu?? M/kiti UDP- John Cheyo (Bariadi), Makamu Isaac Cheyo (Bariadi), Viongozi wa juu wote wa Bariadi..

Chama kina mbunge mmoja tu wa Bariadi, chama kina madiwani wilaya moja tu ya Bariadi, Structure iliyokamilika ya chama iko eneo moja tu Bariadi,

Chama kina kiongozi mmoja tu wa Halmashauri Bw.Benjamin Stephen wa Bariadi....Mtaji mkubwa wa chama kwenye uchaguzi mkuu na chaguzi ndogo upo Bariadi...

Mbona pamoja na hayo yote hamsemi UDP ni chama cha Wasukuma, mnang'ang'ana tu kuwa Chadema ni cha wachaga?? Hivi ukiwa CCM lazima uwe na akili ndogo ya kushindwa kureson hata vitu vyepesi hivi?? Shameee.!!

wewe acha upuuzi hapa, umeandika nini??

hauoni kuwa wewe ndie unaeendeleza hizo propaganda?

wanaosema ni cha kikabila huwa wanatoa hoja gani? umezijibu? zimeishajibiwa na chadema??

uko tayari kusikia??
 
Yaani kwa jinsi tulivyoichoka CCM na drama zake Tupo tayari kuchagua CHADEMA & UKAWA... Wawe wachaga, wamasai, wamang'ati sisi tutachagua tu kuliko kuchagua CCM,,, yaani kama CUF vile PEMBA, ukiweka JIWE na CCM wao wanachagua JIWE...
CCM NI JANGA... yaani mnatia hata kichefuchefu kusikiliza drama zetu.. eti wachaga,,, mimi ni ------ na ntachagua tu CHADEMA,, sijawahi kupiga kura nchi hii ila Inshallah 2015 panapo majaliwa kura yangu ipo UKAWA...
 
Maisha ya kisiasa ya CHADEMA ni ya kiuvumilivu na ya kuendelea mbele kutimiza malengo. Lengo ni kutwaa dola. Chama hiki kimekuwa kikiandamwa na visa na mikasa toka ndani na nje yake. Lakini,kinasonga mbele.

Nyuma kidogo, CHADEMA walikejeliwa kama chama cha udini,ukabila na ukanda. Ikasahauliwa kipropaganda kuwa hata waasisi walikuwa mchanganyiko wa kidini,kikabila na kikanda. Hata Mbunge wa kwanza hakutoka Kaskazini. Alitoka Kigoma,yaani,Dr. Amani Walid Kaborou.

Chama hiki kiliathiriwa kwa kiasi fulani na propaganda hizi lakini kikasonga mbele. Walipotimua wanachama wasio watiifu chamani,CHADEMA ilikejeliwa kwa kejeli ya kwanza. Mambo yakaendelea mbele. Nidhamu sasa yaweza kuwepo chamani. Kejeli ya kuwa CHADEMA ni chama cha magaidi nayo ilisemwa na kupita kwa kukosa mashiko.

CHADEMA walipounda Baraza la Mawaziri Vivuli Bungeni peke yao,wakakejeliwa kipropaganda kama wabaguzi na wapenda madaraka. Lilipoundwa Baraza la Mawaziri Vivuli wa vyama vya CHADEMA,CUF na NCCR Mageuzi,kejeli hazikuisha. Ikasemwa kuwa CHADEMA wamevaa koti la vyama vingine kusurvive.

Kufuatia Makubaliano ya Jangwani ya kusimamisha mgombea mmoja wa UKAWA katika ngazi za uongozi,kejeli zikarudi. Wakaitwa wasakatonge,yaani,wasaka madaraka.

Kimsingi,kejeli hizi zote ni propaganda tu za kisiasa. Hazina mantiki lakini zina lengo. Watoa kejeli ni wa kupuuzwa. Watoaji wanaweweseka na jinsi chama hiki kinavyojiimarisha kwa mbinu na mikakati mbalimbali. Wanaamini kejeli zaweza kupunguza kasi ya kutimiza lengo. CHADEMA songeni mbele kwakuwa kejeli dawa yake jeuri!
 
Kejeli muda mwingine hugeuka na kutengeneza nguvu kubwa kwa wahusika
 
Mleta mada, mbona huweki chadema walipokuwa wakiwakejeli CUF? au umesahau?

jana kuna mtu alikiri humu ndani kuwa CHADEMA ni wadini na sera zao za UKANDA zinaweza kuliangamiza taifa huku akiwaasa UKAWA kumpa LIPUMBA nafasi ya kupeperusha bendera yao 2015, sijui mleta mada jana alikuwa wapi. Tena ile mada ya jana iliwekwa na mfuasi wa CHADEMA aliyeiva.
 
maneno yenu hata siamini kabisa, hivi kuna vyama vimekejeliana kwenye siasa za Tanzania kama CDM na CUF? leo mbona mmeungana? basi malumiane wenyewe huko huko UKAWA.
 
Back
Top Bottom