Dhana ya udini, ukabila na ukanda wa CHADEMA

Dhana ya udini, ukabila na ukanda wa CHADEMA

Mimi Muhehe naipenda CHADEMA lakini sijulikani hata na kiongozi mmoja wa chama nipewe vipi huo uongozi ndani ya chama??tatizo sio uhehe wangu,au Dini yangu au labda kanda ninayotoka..ila ni mimi kama nataka uongozi ktk chama nitajiunga rasmi na nitapitia muda wa kujifunza na kujipambanua halafu taratibu nitaaminiwa nitateuliwa au nitagombea nami nitaongoza. Na Hapa nasisitiza wakati wote sifa za mtu zitampa nafasi, NI SIFA ZAKE PEKEE.!!!
Kwa hiyo ZZK hajulikani? Hana sifa kama wewe mhehe?
 
Chama hiki kimejipambanua kuwa ni cha wachaga kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
1. Viongozi wakuu wa juu hawakuchaguliwa kwa sifa bali ni kwa kabila lao. M/kiti, mtunza fedha akina mnyika. Makatibu wengi wa mikoa ni akina kilewo, munisi, kiwia
2. Kati ya wabunge 25 wa kuteuliwa hakuna wanaotoka mikoa ya kusini ya mtwara na lindi kama wapo tutajie
3. Asilimia kubwa ya wabunge wa kuteuliwa ni wachaga au watu wanaousiana na big fish kama vile rose kamili, dada yake lisu n.k.

Kwanza ni uongo wa hali ya juu, Mnyika sio Mchaga, pili sio viongozi wote wa juu ni wachaga! zaidi ya Mbowe na Komu...

Uteuzi wa wabubge wa kuteuliwa, kwa chadema ulizingatia mchango wa mhusika katika kura za junmla, mdio maana wanawake wengi kwenye nafasi hizo ni wale waliogombeua ubunge majimboni na kukosa, lakini kura zao na effort zao zilichangia CDM kuwa na alama za kutosha kupata wateuliwa wengi wa nafasi hizo.

Kama ni chama cha kifamilia, CCM ndio inaongoza, hata JK aliwahi kutamka kuwa URAIS wake ni WAFAMILIA, ndio maana anawatumia wanae na mke wake katika kampeni. Angalia viongozi wa CCM wote, vijana, wazazi wao walikuwa viongozi CCM, Sitta na Mkewe(mama sita), January makamba, Nchimbi, Malima, Nape, Jerry Slaa..n\a wengine wengi! Hizo sio familia, au wewe unasikiliza propaganda za Nepi nakuzileta hapa....

No research, no right to speak!
 
Mkuu jmushi1,
Naomba kama utaweza, define kwanza, UKABILA NI NINI, kisha tuendelee na mjadala. Otherwise, kila mtu akiwa na definition yake hatutafikia conclusion. Ni kwa sababu watu wengine wana chuki tu mioyoni mwao na wachagga, laiti wangekuwepo wamakonde watupu ngazi za juu CDM isingekuwa tatizo hata kidogo. So, tuanzie kwanza na definition, plse!
Ukabila itakuwa ni kuwapendelea wananchi wa kabila lako.Kwa wanaopandikiza chuki,wanazungumzia uongozi wa chadema,na ndiyo maana nimeuliza swali lakini hadi usawa huu hamna mtu anajibu kwamba kama tukiwa na mwenyekiti mgogo basi chama kitakuwa cha kigogo?
 
Last edited by a moderator:
Mimi Muhehe naipenda CHADEMA lakini sijulikani hata na kiongozi mmoja wa chama nipewe vipi huo uongozi ndani ya chama??tatizo sio uhehe wangu,au Dini yangu au labda kanda ninayotoka..ila ni mimi kama nataka uongozi ktk chama nitajiunga rasmi na nitapitia muda wa kujifunza na kujipambanua halafu taratibu nitaaminiwa nitateuliwa au nitagombea nami nitaongoza. Na Hapa nasisitiza wakati wote sifa za mtu zitampa nafasi, NI SIFA ZAKE PEKEE.!!!
Wahehe subirini mkwawa arudi ndio mpate uongozi lakini cdm mmmmmhhhh
 
Haya ni miongoni mwa mambo yenye kudhihirisha udini uliopo katika chama chenu cha KANISA.
1. Mbowe katika kikao kimoja cha kamati kuu alivyopishana kimaneno na Zitto alijisahau na kutoa ya moyoni kwakumuambia zitto "mh zitto si uende huko CUF kwa waislamu wenzako?".
2. Mchungaji Msigwa aliwatukana waislamu Bungeni tena wakiwa katika ibada tukufu ya funga ndani ramadhani. Kwa kuzingatia umuhimu wa maneno hayo Mbowe akamkubali na leo amekaimu kama Naibu katibu mkuu wa chama. Mtei ameshatoa kauli za kidini ktk mchakato wa katiba. Ni mengi sana na sina haja kuandika sana kilichobakia ni kazi ya kuwaelimisha watanzania kilichoko behind the scene ya CDM.
Huu ni uongo,uko kwenye kamati kuu?Na uliweza kuingia kwenye kikao hicho kwasababu wewe ni mchagga ama mkristo?Zitto alisema nini hadi akaambiwa maneno hayo na Mbowe?Ccm mna mpaka viongozi waganga wa kienyeji.Wengine walikamatwa wakiwanga bungeni,kwahiyo tuseme basi ccm ni chama cha kichawi.
 
Kwa hiyo ZZK hajulikani? Hana sifa kama wewe mhehe?

Zito aliikuta CDM, alijiunga nayo na alipata huo muda wa kujifunza na kujipambanua uwezo wake na aliaminiwa na uongozi uliokuwepo..aliteuliwa kushika nyazifa kubwa na aligombea pia akaaminiwa akachaguliwa na amedumu kwa muda mrefu katika nafasi hizo. Kweli kwa muda mrefu, amefanya mambo mazuri mengi. Hakupata hizo nafasi kwa sababu yeye ni Muha au Muislam au Kanda aliyotokea bali sifa na weledi aliokuwa nao. Lakini Zito sio Malaika, kakengeuka kapoteza sifa za kuendelea kuwa ktk hizo nafasi. Utaratibu mzuri kabisa wala hakuna ugomvi wala Chuki ni utaratibu tuu ukikosea unaadhibiwa.
 
Wahehe subirini mkwawa arudi ndio mpate uongozi lakini cdm mmmmmhhhh
Kwani wahehe hawana kiongozi wa chadema?Ama unazungumzia uongozi gani?Huwezi kuwa na wenyeviti 50 kwa wakati mmoja,na sidhani kama kuna taratibu za kuongoza kutokana na kabila.
 
Kuna watu wanafurahia Mh Mbowe kuondoka kwenye nafasi ya Uenyekiti,kuna wanaotaka hata kuandamana ili aondoke,je chama ni cha kikabila kwasababu tu kwamba mwenyekiti ana kabila?Kwahiyo mwenyekiti akiwa mgogo basi cha ni cha kigogo?

Kuna anayeweza kuniambia ukabila uko wapi kwenye chama cha cdm?Je ni kweli kuwa mwenyekiti mchagga akiondoka ndo chama kitakuwa si cha wachagga?Ili linanitatiza sana tu!

Acha kabisa wachaga tuna kazi ndani ya nchi hii, Lipumba ni mwenyekiti wa pili wa CUF baada ya mzee Mapalala hadi sasa hamna anayehoji, achilia mbali akina cheyo, mtikila, maalim seif na wengineo wenye tiketi za kudumu za kuongoza vyama vyao lakini kosa ni kuwa mchaga!
 
nina ubhakika kuna watakaokuja na kuweka kujibu baadhi ya maswali yako hapo juu,however Lissu ni mchagga?chama ni cha kifamilia kwasababu tu kuna wenye uhusiano ambao wako ndani ya chama?je ccm ni chama cha kikwere kwasababu mwenyekiti na familia yake wana nfasi ndani ya chama?je chama hicho ni cha kifamilia?

Ni chama cha koo. Kuna koo za Kikwete, Malecela, Mzindakaya,Mwinyi, Kawawa nk. Mle hutamkuta Kalumanzila, Mabula, Omulangira waitu, Kiseryi, Mgonja nk, akina Masawe na Nnko kwa kuliona hili na kuanzishia mahali ambapo na sisi tupate pakujiliwazia inakuwa ni nongwa? Khaaa!
 
Acha kabisa wachaga tuna kazi ndani ya nchi hii, Lipumba ni mwenyekiti wa pili wa CUF baada ya mzee Mapalala hadi sasa hamna anayehoji, achilia mbali akina cheyo, mtikila, maalim seif na wengineo wenye tiketi za kudumu za kuongoza vyama vyao lakini kosa ni kuwa mchaga!
Ndo maana waafrika tunabaki nyuma,chuki mbaya sana.Inakwamisha maendeleo.
 
Acha kutoa maneno ya uwo moja ya katibu alyetimuliwa ambaye ni zitto si ni mtu wakigoma,na huyo dada yake lisu ni mnyaturu wa singida..slaa muiraq sasa wewe uchaga unatoka wapi hapo...ntakupa wengne bdaye.
 
Hakuna ukabila kwenye Chadema ni maneno ya watu wavivu kufikiria. Kuna viongozi wengi wa kaskazini kwasababu kuna wabunge wengi kaskazini. Zitto mafano wakati anaingia Chadema alikuwa kijana kidogo na hakuwa na kitu hivyo sio ukabila vilevile wanaosema Chadema ni chama cha Wachagga ni wana Chama au? kwasababu huwezi kuwa kiongozi kama si mwanachama. Sugu, Msigwa, Lissu, mbunge wa Mwanza wote hawa hawajatokea kaskazini!. Kama unataka kukosoa chama jiunge kwanza huwezi kuchagua watu tu wa Lindi wakati hawako kwenye harakati.

Natumaini ulichokiongea hapo juu ndio msingi mkubwa wa hii mada.
Mfano: huwezi kuchagua mbunge viti maalum kutoka kusini wakati hata wanachama hawapo. Tumeshuhudia juzijuzi tu ktk harakati za m4c ndio kusini imefunguka.....kulikuwa hakuna wanaharakati wa chadema......mnaotaka kusini kuwe na wabunge wa viti maalum wangechaguliwa wanaccm/cuf. Muwe mnafikiria sio mnakurupuka tu.
Hata dini zetu tunazoziamini zina 'origin' zake, MASHARIKI YA KATI. Je, tuzikatae kwa sababu zina asili huko......
 
Huu ni uongo,uko kwenye kamati kuu?Na uliweza kuingia kwenye kikao hicho kwasababu wewe ni mchagga ama mkristo?Zitto alisema nini hadi akaambiwa maneno hayo na Mbowe?Ccm mna mpaka viongozi waganga wa kienyeji.Wengine walikamatwa wakiwanga bungeni,kwahiyo tuseme basi ccm ni chama cha kichawi.
..kwanza siku zote hapo ndio munapo kosea hakuna chama kinacho weza kujilinganisha na ccm kwa lipi mpaka unajilinganisha na ccm..chama kinachojilinganisha na ccm kinajipa nafasi isio iweza ccm ina zaidi ya kila sifa aidha sifa nzuri au mbaya.ccm ina kila aina tofauti ya makundi lipo kundi kubwa la wasomi lipo kundi kubwa la mabumbu kama ww .lipo kundi la wadini lipo kundi la wakabila lipi kundi hata la mashoga lipo kundi la maskini na la mtajiri..sasa nyie cdm munamashoga wanahesabika mjengoni sijui muna wangapi vile? Ndio maana wabunge wa ccm wakaanza kuwagobea mpaka wakaanza kutumia waganga wakienyeji.
Musijilinganishe hata kitu kimoja na ccm nyie jilinganisheni na wenzenu cuf nccr tlp nk sio ccm mutakuwa munajidanganya
 
Acha kabisa wachaga tuna kazi ndani ya nchi hii, Lipumba ni mwenyekiti wa pili wa CUF baada ya mzee Mapalala hadi sasa hamna anayehoji, achilia mbali akina cheyo, mtikila, maalim seif na wengineo wenye tiketi za kudumu za kuongoza vyama vyao lakini kosa ni kuwa mchaga!

Umenena, jmushi.......mti wenye matunda lazima upihwe mawe!
 
kuna watu wanafurahia mh mbowe kuondoka kwenye nafasi ya uenyekiti,kuna wanaotaka hata kuandamana ili aondoke,je chama ni cha kikabila kwasababu tu kwamba mwenyekiti ana kabila?kwahiyo mwenyekiti akiwa mgogo basi chama ni cha kigogo?

Kuna anayeweza kuniambia ukabila uko wapi kwenye chama cha cdm?je ni kweli kuwa mwenyekiti mchagga akiondoka ndo chama kitakuwa si cha wachagga?ili linanitatiza sana tu!

kwa hiyo ccm ni ya wazanaki na wakristu?ni upambavu na ujinga kuwa namawazo ya namna hiyo.wachaga wanayo haki sawa na watz wengine,ukabila haufaidii chochote tunataka uwezo na sifa za mtu kuongoza sio porojo.mimi pamoja na wanaserengeti tunaunga mkono maamuzi ya kamati kuu.zito angelikuwa na nia njema huo udhaifu anaousema alisaidiaje kuurekebisha kama hana nia ovu ya kutumiwa na wasira kuiua cdm.
 
Acha kutoa maneno ya uwo moja ya katibu alyetimuliwa ambaye ni zitto si ni mtu wakigoma,na huyo dada yake lisu ni mnyaturu wa singida..slaa muiraq sasa wewe uchaga unatoka wapi hapo...ntakupa wengne bdaye.

Waambiehao wavivu wa kufikiri-wenye mawazo mgando!
 
..kwanza siku zote hapo ndio munapo kosea hakuna chama kinacho weza kujilinganisha na ccm kwa lipi mpaka unajilinganisha na ccm..chama kinachojilinganisha na ccm kinajipa nafasi isio iweza ccm ina zaidi ya kila sifa aidha sifa nzuri au mbaya.ccm ina kila aina tofauti ya makundi lipo kundi kubwa la wasomi lipo kundi kubwa la mabumbu kama ww .lipo kundi la wadini lipo kundi la wakabila lipi kundi hata la mashoga lipo kundi la maskini na la mtajiri..sasa nyie cdm munamashoga wanahesabika mjengoni sijui muna wangapi vile? Ndio maana wabunge wa ccm wakaanza kuwagobea mpaka wakaanza kutumia waganga wakienyeji.
Musijilinganishe hata kitu kimoja na ccm nyie jilinganisheni na wenzenu cuf nccr tlp nk sio ccm mutakuwa munajidanganya
Wewe ni Chenge ama Maji Marefu?maana umechukulia personal.
 
Back
Top Bottom