Diamond aachia wimbo mpya "Acha nikae kimya"

Diamond aachia wimbo mpya "Acha nikae kimya"

Ugomvi wa Baba na Mama mtoto kaa pembeni...ndo diamond alichomaanisha maana ikitokea umlalia pande moja afu suluhu ikapatikana na wew ulijifanya kumponda mmojawapo afu ukweli ukajulikana...wew ndo utageuka adui.
 
The silence of our friends hurts more than the noise made by our enemies
 
Naona wanaume wenye mahaba ya dhati na diamond walivopovuka kule instagram mange alivomtukana na kumpa facts ... ila ukwel lazima ujulikane na usemwe kwamba
Diamond platnumz anatumika full stop. Na zaidi anatafuta kiki na utajiri wa haraka kupitia matatizo ya watu. Kanyimbo kake sio tu kwamba ni ka kinafiki bali hata anafanya matatizo ya watu makubwa kama source of income, nyimbo unainunua 300 si bora hio 300 nkale karanga ?
Mnafiki sana...ingekua ni latifa sjui ametoweka angefanyaje ama zari ametekwa ingekuaje angeitoa hio nyimbo kwamba atakaa kimya ....nyambaff
 
Ninachosikitika siasa zimetugawa, yaani imekuwa kama uadui, na hii sumu wanaisambaza watu wa upinzani ni sumu mbaya sana, itafika kipindi utashindwa kumsaidia mtu tu kisa itikadi zenu tofauti, sasa kosa la diamond platnumz lipo wapi, hii inchi kila mtu yupo free kuchagua anachokitaka ili mradi asivunje sheria, diamond kawasilisha maoni yake kupitia mziki. Kuwa na itikadi tofauti isiwe tatizo, ila Ninachosikitika sana wanasiasa na mitandao ya kijamii inatugawa vibaya sana, mpaka inafikia Kipindi tunaomba mabaya yatokee kwa nchi yetu, ili kuikomoa serikali, yaani mpaka kwenye kusifia tunakosoa na kwenye kukosoa tunasifia.Watu wanaomponda diamond platnumz ndio hao wanalalamika kila siku inchi haina demokrasia, lkn hawajui diamond platnumz ametumia haki yake ya msingi ya demokrasia kawasilisha mawazo yake kupitia mziki wake. Tanzania kwanza, tusilichukulie hili swala la ROMA kisiasa eti ni la upande fulani. Nammlaani sana kimambi, kwani hii sumu anayoisambaza, haina tofauti na kile kituo cha radio Rwanda kilichorusha habari za kibaguzi, mwisho wake kukawa na mauwaji ya Kimbari. Watanzania tuwe makini sana tusiruhusu mitandao ya jamii na wanasiasa watugawe.
Huyu Mange anakoelekea atatugawa Sana watz, yaani daah inasikitisha sana
 
Hili taifa kuna wasanii wanazan uzalendo ni kuimba nyimbo za mapenzi. Domo anaona bora akae kimya asiongee ishu znazoligusa taifa. Yeye anawaza nyimbo za ngono tu.
 
Huyu Mange anakoelekea atatugawa Sana watz, yaani daah inasikitisha sana
inaonekana umemjua sasa hivi huyo mange!
Ungemfatilia kipindi cha uchaguzi usingeandika hayo maneno!
Na wenye mamlaka walinogewa kweli na maneno yake
 
Hii movie wanaicheza vizuri kweli..


Nasikia wameenda nyumbani kwa makonda
 
Jambo moja kubwa ni kuwa Chibu anakili na kutambua kuwa hali ya nchi ni tete. Hofu imetanda na yeye imemkumba hivo amechagua kukaa kimya (because he is a coward).
 
inaonekana umemjua sasa hivi huyo mange!
Ungemfatilia kipindi cha uchaguzi usingeandika hayo maneno!
Na wenye mamlaka walinogewa kweli na maneno yake
Sijaanza kumjua leo, ila nachojua kuhusu huyu Dada ni mvurugaji tu na kigeugeu. That's all
 
Sahihi kabisa mkuu huu wimbo ni mzuri na hauna shida isipo kuwa wengi hawajauelewa wao wamebeba dhana moja tu ya nikae kimya wamesahau ndani ya huo ukimya wake yameongelewa mambo indirectly.
Itabidi warudi tena Darasani wakajifunze
Kuhusu Fasihi..
Then wachambue wimbo wa Diamond
 
Kwenye ufafanuzi wake sijamuelewq amasema sijui kuna watu wanaishi nje na wanajifanya wanapigania haki warudi tuje tupiganie wote hapa!
Sijui tatizo elimu au nini.....

Wangapi viongozi wa africa walipigania uhuru wa mataifa yao wakiwa nje?

Kuweka picha ya baba wa taifa naona kama theme ya wimbo na hiyo picha kama haviendani, kwaasababu baba wa taifa hakuwahi kukaa kimya pale mambo yalipokuwa yanaharibika na alikemea vikali........
Sijamuelewa kwa kweli
 
Back
Top Bottom